Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Ishara-ya-utambulisho. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Ishara-ya-utambulisho. Onyesha machapisho yote

Jumapili, 4 Februari 2018

Mamlaka ya Mungu | 4. Amri ya Mungu kwa Shetani

4. Amri ya Mungu kwa Shetani

Ayubu 2:6 Naye Yehova akasema kwa Shetani, Tazama, yeye yuko katika mkono wako; lakini uuhifadhi uhai wake.
Umeme wa Mashariki, Kanisa la Mwenyezi Mungu, Biblia,
Shetani hupendeza kwa Ayubu katika jaribio hilo

Shetani Hajawahi Kuthubutu Kukiuka Mamlaka ya Muumba, na Kwa Sababu Hiyo, Vitu Vyote Vinaishi kwa Mpangilio

Mwenyezi Mungu alisema, Hili ni dondoo kutoka katika Kitabu cha Ayubu, na “yeye” katika maneno haya inaashiria Ayubu. Ingawaje imeandikwa kwa muhtasari, sentensi hii inaelezea masuala mengi. Inafafanua mabadilishano fulani kati ya Mungu na Shetani kwenye ulimwengu wa kiroho, na inatwambia kuwa kiini cha maneno ya Mungu kilikuwa Shetani. Pia inarekodi kile kilichozungumziwa mahususi na Mungu. Maneno ya Mungu yalikuwa amri na shurutisho kwa Shetani.