Watu wengi walio na imani kwa Bwana wanasadiki kwamba ufalme wa mbinguni uko mbinguni. Je, hivyo ndivyo ilivyo kwa kweli? Sala ya Bwana inasema: "Baba yetu uliye mbinguni, Jina lako litukuzwe. Ufalme wako uje, Mapenzi yako yatimizwe, hapa duniani kama huko mbinguni" (Mathayo 6:9-10). Kitabu cha Ufunuo kinasema, "Falme za dunia zimekuwa falme za Bwana wetu, na za Kristo wake" (Ufunuo 11:15). "Mji mtakatifu, Yerusalemu mpya, ukishuka kutoka kwa Mungu mbinguni, … maskani ya Mungu yako pamoja na wanadamu" (Ufunuo 21:2-3). Hivyo, ufalme wa mbinguni uko mbinguni au ulimwenguni?
I
Kusudi la hukumu ya Mungu ni kuhimiza utiifu wa mwanadamu;
kusudi la adabu ya Mungu ni kuruhusu mbadiliko wa mwanadamu.
Ingawa kazi ya Mungu ni kwa ajili ya usimamizi Wake,
hakuna kitu Anachofanya kisicho kizuri kwa mwanadamu.
Mungu anataka nchi mbali na Israeli watii jinsi Waisraeli walivyofanya,
kuwafanya kuwa wanadamu wa kweli,
ili katika nchi mbali na Israeli wafuasi wa Mungu watapatikana.
Huu ni usimamizi wa Mungu.














