Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Uzima-wa-Milele. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Uzima-wa-Milele. Onyesha machapisho yote

Jumatatu, 24 Septemba 2018

Kuzaliwa Upya Kupitia Neno la Mungu(II)

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, maombi

Kuzaliwa Upya Kupitia Neno la Mungu(II)

Wang Gang Mkoa wa Shandong
Baada ya kurudi kwa kile chumba kidogo, nilichubuliwa na kugongwagongwa sana, maumivu yalikuwa yasiyovumilika. Moyo wangu haukuweza kujizuia kuzalisha hisia ya huzuni na udhaifu: Kwa nini waumini wanapaswa kuteseka jinsi hii? Nilihubiri Injili na nia njema za kuwaruhusu watu kuutafuta ukweli na kuokolewa, na bila kutarajia nimepitia mateso haya. Katika kufikiri juu ya hili, nilihisi zaidi kuwa nilikuwa nimekosewa.

Jumatano, 9 Mei 2018

"Imani katika Mungu" (4) - Je, Kuamini katika Biblia ni Sawa na Kuamini katika Bwana?



"Imani katika Mungu" (4) - Je, Kuamini katika Biblia ni Sawa na Kuamini katika Bwana?

Utambulisho


Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, Biblia,Watu wengi zaidi katika ulimwengu wa dini huamini kwamba Biblia ni kanuni ya Ukristo,kwamba mtu lazima ashikilie Biblia na kuweka msingi wa imani yake katika Bwana kwenye Biblia kabisa, na kwamba mtu hawezi kuitwa muumini akipotoka kutoka kwenye Biblia. Hivyo imani katika Bwana na imani katika Biblia ni sawa? Uhusiano kati ya Biblia na Bwana ni upi hasa? Bwana Yesu aliwakaripia Mafarisayo wakati fulani kwa maneno haya, “Tafuta katika maandiko; kwa kuwa ndani yake mnadhani kuwa mna uzima wa milele: na hayo ndiyo yananishuhudia. Nanyi hamtakuja Kwangu, kwamba mpate uhai." (Yohana 5:39-40). Biblia ni ushuhudawa Mungu tu, lakini haina uzima wa milele. Mungu pekee ndiye ukweli, njia na uzima. Kwa hivyo, tuiangalie Biblia vipi kwa njia ambayo inakubaliana na mapenzi ya Bwana?

Jumapili, 11 Februari 2018

Best Swahili Christian Worship Song “Maisha Yetu Sio Bure”


Best Swahili Christian Worship Song “Maisha Yetu Sio Bure”


Utambulisho

Maisha yetu sio bure. Maisha yetu sio bure.

Leo tunakutana na Mungu, tunapitia kazi Yake.
Tumemjua Mungu katika mwili, wa utendaji na wa hakika.
Tumeiona kazi Yake, nzuri na ya ajabu.
Kila siku ya maisha yetu sio bure.
Tunamshuhudia Kristo kama ukweli na uzima!
Kufahamu na kukumbatia fumbo hili.
Nyayo zetu ziko katika njia ng’avu zaidi ya hadi katika uzima.
Hatutafuti tena, yote yako wazi kwetu.
Mungu, tutakupenda Wewe milele bila majuto.
Tumepata ukweli, uzima wa milele tutapata.
Maisha yetu sio bure, sio bure.
Maisha yetu sio bure. Maisha yetu sio bure.

Jumapili, 26 Novemba 2017

Ni Kristo Wa Siku za Mwisho Pekee Ndiye Anayeweza Kumpa Mwanadamu Njia ya Uzima wa Milele

Ni Kristo wa Siku za Mwisho Pekee Ndiye Anayeweza Kumpa Mwanadamu Njia ya Uzima wa Milele

Mwenyezi Mungu alisema, Njia ya maisha si kitu ambacho kinaweza kumilikiwa na mtu yeyote tu, wala hakipatikani kwa urahisi na wote. Hiyo ni kwa sababu maisha yanaweza kuja tu kutoka kwa Mungu, ambayo ni kusema, Mungu Mwenyewe tu ndiye Anamiliki mali ya maisha, hakuna njia ya maisha bila Mungu Mwenyewe, na hivyo Mungu tu ndiye chanzo cha uzima, na kijito cha maji ya uzima kinachotiririka nyakati zote. Kutoka Alipoumba dunia, Mungu amefanya kazi kubwa inayoshirikisha uhai wa maisha, Amefanya kazi kubwa ambayo huletea mwanadamu maisha, na Amelipa gharama kubwa ili mtu aweze kupata uzima, kwa kuwa Mungu Mwenyewe ni uzima wa milele, na Mungu Mwenyewe ni njia ambayo kwayo mtu hufufuliwa.