Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Kazi-na-Kuingia. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Kazi-na-Kuingia. Onyesha machapisho yote

Jumanne, 20 Machi 2018

Umeme wa Mashariki | Kazi na Kuingia (4)

Umeme wa Mashariki | Kazi na Kuingia (4)

Mwenyezi Mungu alisema, Ikiwa mwanadamu anaweza kuingia kabisa kulingana na kazi ya Roho Mtakatifu, maisha yake yatachipuka haraka kama mmea wa mwanzi baada ya mvua ya majira ya kuchipua. Kwa kuangalia kimo cha sasa wa watu wengi, hakuna mtu hata mmoja anayetilia mkazo umuhimu wa uzima. Badala yake, watu wanaweka umuhimu katika baadhi ya mambo ya juujuu yasiyokuwa na umuhimu. Au wanakimbia huku na kule na kufanya kazi bila malengo na ovyoovyo bila mwelekeo, hawajui waende njia gani na zaidi kwa ajili ya nani. “Wanajificha wenyewe katika unyenyekevu.” Ukweli ni kwamba, ni wachache miongoni mwenu mnaojua makusudi ya Mungu kuhusu siku za mwisho. Ni wachache sana miongoni mwenu wanaojua nyayo za Mungu, na wachache zaidi wanajua utimilifu wa mwisho wa Mungu utakavyokuwa. Halafu kila mtu, kwa utashi tupu, anakubali kufundishwa nidhamu na kushughulikiwa na wengine, kana kwamba wanajitayarisha[1] na kusubiri siku ambayo hatimaye wamekwishaifanya na wanaweza kustarehe. Sitatoa maoni yoyote juu ya “maajabu” haya miongoni mwa watu, lakini kuna hoja moja ambayo wote mnapaswa kuielewa. Kwa sasa watu wengi wanaelekea katika hali isiyo ya kawaida,[2] hatua zao za kuingia tayari zinaelekea mwisho kabisa.[4] Pengine watu wengi wanafikiri kwamba mwanadamu anatamani “Shangri-La” (‘bonde la utulivu’), wakiamini kuwa ni “sehemu ya uhuru.” Kimsingi, sivyo ilivyo. Mtu anaweza kusema kwamba watu wamekwishapotoka tayari. Lakini bila kujali kile watu wanachokifanya, bado Nahitaji kuzungumza juu ya kile ambacho mwanadamu anapaswa kuingia ndani. Ustahilifu na kasoro za umati sio mada ya msingi ya majadiliano haya. Natumaini kwamba ndugu wote wataweza kupokea maneno Yangu kabisa na kwa usahihi na sio kuelewa visivyo nia Yangu.

Umeme wa Mashariki | Kazi na Kuingia (6)

Umeme wa Mashariki, Kanisa la Mwenyezi Mungu, siku za mwisho,
Kazi na Kuingia (6)

Umeme wa Mashariki | Kazi na Kuingia (6)

Mwenyezi Mungu alisema, Kazi na kuingia kwa uhalisia ni vya kiutendaji na vinarejelea kazi ya Mungu na kuingia kwa mwanadamu. Mwanadamu kukosa kabisa uelewa juu ya sura halisi ya Mungu na kazi ya Mungu kumesababisha shida kubwa katika kuingia kwake. Leo hii, watu wengi bado hawajui kazi ambayo Mungu anatimiza katika siku za mwisho, au kwa nini Mungu Anastahimili fedheha kubwa kupita kiasi kuja katika mwili na kusimama na mwanadamu katika makovu na majonzi. Mwanadamu hajui chochote kuhusu lengo la kazi ya Mungu, wala kusudi la mpango wa Mungu kwa ajili ya siku za mwisho.

Ijumaa, 16 Machi 2018

Umeme wa Mashariki | Kazi na Kuingia (10)

Umeme wa Mashariki, Kanisa la Mwenyezi Mungu, kumjua Mungu,
Kazi na Kuingia (10)

Kazi na Kuingia (10)


Mwenyezi Mungu alisema, Kwa wanadamu kuendelea mbele kiasi hiki ni hali isiyo na kigezo. Kazi ya Mungu na kuingia kwa mwanadamu vinaendelea bega kwa bega, na hivyo kazi ya Mungu, pia, ni tukio kubwa lisilo na kifani. Kuingia kwa mwanadamu hadi sasa ni ajabu ambayo kamwe haijawahi kufikiriwa na mwanadamu. Kazi ya Mungu imefikia upeo wake—na, kufuatia, "kuingia" kwa mwanadamu[1] pia kumefikia kilele chake. Mungu amejishusha kwa kadiri Anavyoweza, na kamwe Hajawahi kuwalalamikia wanadamu au vitu vyote katika ulimwengu.