Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Mpendeni-Mungu. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Mpendeni-Mungu. Onyesha machapisho yote

Jumatano, 14 Machi 2018

Umeme wa Mashariki | Tamko la Thelathini na Mbili

    Mwenyezi Mungu alisema, Watu wanapokusanyika pamoja na Mimi, moyo Wangu unajawa na furaha. Mara moja, Ninatoa baraka zilizo mkononi Mwangu miongoni mwa binadamu, ili watu waweze kukusanyika kwa mkutano na Mimi, na kutokuwa maadui wanaoniasi lakini marafiki wanaotangamana na Mimi. Hivyo, Mimi pia ni wa dhati kwa mwanadamu. Katika kazi Yangu, mwanadamu anaonekana kama mwanachama wa shirika la ngazi ya juu, hivyo Ninamzingatia zaidi, kwa maana daima amekuwa kusudi la kazi Yangu. Nimeweka imara mahali Pangu katika mioyo ya watu, ili mioyo yao iweze kuniheshimu—ilhali wanabaki wasiojua kabisa kwa nini Ninafanya hili, na hawafanyi lolote ila kusubiri. Ingawa kuna mahali ambapo Nimeweka imara katika mioyo ya watu, hawahitaji kwamba Niishi hapo. Badala yake, wanamsubiri “Mtakatifu” katika mioyo yao kuwasili ghafla. Kwa sababu utambulisho Wangu ni duni sana, Sifikii mahitaji ya watu na hivyo Naondolewa na wao. Kwa sababu wanachotaka ni “Mimi” ambaye ni mwenye majivuno sana—ilhali Ninapokuja, Sikuonekana kwa njia hii kwa mwanadamu, kwa hivyo aliendelea kuangalia mbali, akimsubiri aliye moyoni mwake. Ninapokuja mbele ya watu, wananikataa mbele ya umma.

Jumatano, 13 Desemba 2017

Wanaompenda Mungu Wataishi Milele Katika Mwangaza Wake

Umeme wa Mashariki,  Kanisa la Mwenyezi Mungu,  Kanisa,
Umeme wa Mashariki | Wanaompenda Mungu Wataishi Milele Katika Mwangaza Wake

Wanaompenda Mungu Wataishi Milele Katika Mwangaza Wake

Mwenyezi Mungu alisema,Kiini cha imani ya watu wengi katika Mungu ni imani za kidini: Hawana uwezo wa kumpenda Mungu, na wanaweza kumfuata Mungu tu kama roboti, bila kuweza kumtamani Mungu, ama kumwabudu. Wanamfuata tu kimyakimya. Watu wengi wanamwamini Mungu, lakini wapo wachache sana ambao humpenda Mungu; wanamheshimu tu Mungu kwa sababu wanaogopa majanga, au hata wanamstahi Mungu kwa sababu ni Mwenye nguvu na aliye juu—lakini katika kumheshimu na kuvutiwa kwao hakuna upendo au kutamani kwa kweli. Katika matukio wanayoyapitia wanataka chembe za ukweli, au hata miujiza fulani isiyokuwa na maana.