Kazi ambayo Yehova Alifanya kwa Waisraeli ilianzishwa miongoni mwa binadamu mahali pa asili pa Mungu hapa ulimwenguni, pahali patakatifu ambapo Alikuwepo. Hii kazi Aliiwekea mipaka miongoni mwa watu wa Israeli tu. Kwanza, hakufanya kazi nje ya Israeli; badala yake, Alichagua watu Alioona kwamba walifaa ili kuwawekea mipaka upana wa kazi Yake. Israeli ndipo mahali ambapo Mungu Aliwaumba Adamu na Hawa, na kutoka kwenye vumbi la mahali hapo, Yehova Alimwumba mwanadamu; ndio msingi wa kazi Yake ya hapo ulimwenguni. Waisraeli, ambao ni kizazi cha Nuhu na Adamu, ndio waliokuwa msingi wa kazi ya Yehova ulimwenguni.
Jumatatu, 6 Agosti 2018
Umeme wa Mashariki | Yule Anayeshikilia Ukuu // Juu ya Kila Kitu
✨Some feelings about God destroying this world by flood in the documentary the One Who Holds Sovereignty Over...
由 Annie Lee 發佈於 2018年7月18日星期三
Some feelings about God destroying this world by flood in the documentary the One Who Holds Sovereignty Over Everything
Due to God’s sovereignty, various birds and beasts could enter the ark orderly according to God’s instruct. There were big elephants, dainty rabbits, fierce tigers, meek sheep and various insects and so on. They could live in harmony in the ark and no longer slaughtered and fought with each other even they were natural enemies before. At that moment, they could conduct properly and didn’t cross the line. What a big miracle it was! Just as it goes in the hymn, “His deed is everywhere, His power is everywhere, His wisdom is everywhere, and His authority is everywhere.” Let’s see God’s wonderful deeds and realize His sovereignty!
Jumapili, 27 Mei 2018
"Jina la Mungu Limebadilika?!" (2) - Je, ni Kweli kuwa Jina la Mungu Haliwezi Kubadilika?
"Jina la Mungu Limebadilika?!" (2) - Je, ni Kweli kuwa Jina la Mungu Haliwezi Kubadilika?
Utambulisho
Wachungaji na wazee wa ulimwengu wa kidini mara nyingi huhubiri kwa waumini kuwa jina la Bwana Yesu haliwezi kamwe kubadilika na kuwa ni kwa kutegemea tu jina la Bwana Yesu ndio tunaweza kuokolewa. Je, mtazamo wa aina hii unaambatana na kuweli? Yehova Mungu alisema, "kabla yangu hakukuwa na Mungu aliyeumbwa, wala hakutakuwa baada yangu. Mimi, hata mimi, ni BWANA; na isipokuwa mimi hakuna mwokozi" (Isaya 43:10-11). Katika Enzi ya Neema, Mungu mwenye mwili alichukua jina la Yesu.
Jumatatu, 5 Februari 2018
Tabia ya Haki ya Mungu | (II)Ubinadamu Hupata Kibali cha Huruma na Uvumilivu wa Mungu Kupitia kwa Toba ya dhati
![]() |
| Neno la Mungu lilimjia Yona kwa mara ya kwanza |
(II) Ubinadamu Hupata Kibali cha Huruma na Uvumilivu wa Mungu Kupitia kwa Toba ya dhati
Kinachofuata ni hadithi ya biblia ya “Wokovu wa Mungu kwa Ninawi.”
(Yona 1:1-2) Basi neno la BWANA lilimjia Yona mwana wa Amitai, likisema, Inuka, uende Ninawi, mji ule mkubwa, upige kelele juu yake; kwa maana uovu wao umepanda juu mbele zangu.
(Yona 3) Neno la BWANA likamjia Yona mara ya pili, likisema, Inuka, uende Ninawi, mji ule mkubwa, uhubiri habari Ninayokuamuru. Basi Yona akainuka, akaenda Ninawi, kulingana na amri ya BWANA. Basi Ninawi ulikuwa mji mkubwa mno, ukubwa wake mwendo wa siku tatu. Yona akaanza kuuingia mji mwendo wa siku moja, akapaza sauti, akasema, Baada ya siku arobaini mji wa Ninawi utaangamizwa. Basi watu wa Ninawi wakamwamini Mungu, wakatangaza kufunga, wakavaa nguo za magunia, kutoka Yule aliye mkubwa hadi aliye mdogo.
Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee II | Tabia ya Haki ya Mungu
![]() |
| Bwana atashuka juu ya moto wa sulfuri na Sodoma1 |
Umeme wa Mashariki | Tabia ya Haki ya Mungu
Mwenyezi Mungu alisema, Kwa vile sasa mumesikiliza kikao cha ushirika uliopita kuhusu mamlaka ya Mungu, Ninao ujasiri kwamba mumejihami vilivyo na mseto wa maneno kuhusu suala hili. Kiwango unachoweza kukubali, kushika, na kuelewa vyote hivi vinategemea na jitihada zipi utakazotumia. Ni tumaini Langu kwamba utaweza kutazamia suala hili kwa dhati; kwa vyovyote vile hufai kulishughulikia shingo-upande! Sasa, je, kujua mamlaka ya Mungu ni sawa na kujua Mungu kwa uzima wake? Mtu anaweza kusema kwamba kujua mamlaka ya Mungu ndiyo mwanzo wa kumjua Mungu mwenyewe kwa upekee wake, na mtu anaweza kusema pia kwamba kuyajua mamlaka ya Mungu kunamaanisha kwamba mtu tayari ameingia kwenye lango kuu la kujua hali halisi ya ule upekee wa Mungu Mwenyewe. Ufahamu huu ni sehemu moja ya kumjua Mungu. Sehemu ile nyingine ni nini, hivyo basi? Hii ndiyo mada ambayo Ningependa tuweze kushiriki pamoja leo—tabia ya haki ya Mungu.
Jumapili, 4 Februari 2018
Mamlaka ya Mungu | 4. Amri ya Mungu kwa Shetani
4. Amri ya Mungu kwa Shetani
Ayubu 2:6 Naye Yehova akasema kwa Shetani, Tazama, yeye yuko katika mkono wako; lakini uuhifadhi uhai wake.
![]() |
| Shetani hupendeza kwa Ayubu katika jaribio hilo |
Shetani Hajawahi Kuthubutu Kukiuka Mamlaka ya Muumba, na Kwa Sababu Hiyo, Vitu Vyote Vinaishi kwa Mpangilio
Mwenyezi Mungu alisema, Hili ni dondoo kutoka katika Kitabu cha Ayubu, na “yeye” katika maneno haya inaashiria Ayubu. Ingawaje imeandikwa kwa muhtasari, sentensi hii inaelezea masuala mengi. Inafafanua mabadilishano fulani kati ya Mungu na Shetani kwenye ulimwengu wa kiroho, na inatwambia kuwa kiini cha maneno ya Mungu kilikuwa Shetani. Pia inarekodi kile kilichozungumziwa mahususi na Mungu. Maneno ya Mungu yalikuwa amri na shurutisho kwa Shetani.
Jumatano, 24 Januari 2018
Kazi ya Mungu, Tabia ya Mungu, na Mungu Mwenyewe II | Kuhusu Ayubu
![]() |
| Matoleo ya kuteketezwa mapema asubuhi |
Kuhusu Ayubu
Mwenyezi Mungu alisema, Baada ya kusikia namna Ayubu alivyopitia majaribio, kunao uwezekano kwamba wengi wenu watataka kujua maelezo zaidi kuhusu Ayubu mwenyewe, hasa kuhusiana na siri iliyomfanya akapata sifa za Mungu. Hivyo basi leo, hebu tuzungumzie kuhusu Ayubu!
Katika Maisha ya Kila Siku ya Ayubu Tunaona Utimilifu, Unyofu, Kumcha Mungu, na Kujiepusha na Maovu
Kama tutazungumzia Ayubu, basi lazima tuanze na namna ambavyo alitathminiwa kwa mujibu wa matamshi kutoka kwa kinywa cha Mungu mwenyewe: “hakuna hata mmoja aliye kama yeye duniani, mtu mkamilifu na mnyofu, mwenye kumcha Mungu, na kuuepuka uovu.”
Alhamisi, 30 Novemba 2017
Ngurumo Saba Zatoa Sauti— Zikitabiri Kuwa Injili ya Ufalme Itaenea Kote Ulimwenguni
Ngurumo Saba Zatoa Sauti— Zikitabiri Kuwa Injili ya Ufalme Itaenea Kote Ulimwenguni
Mwenyezi Mungu alisema, Mimi Naeneza kazi Yangu katika nchi za Mataifa. Utukufu Wangu unamulika kotekote ulimwenguni; mapenzi Yangu yamo katika mtawanyiko wa wanadamu, wote wakiongozwa kwa mkono Wangu na kufanya kazi ambayo Nimewapa. Kuanzia wakati huu kuendelea, Nimeingia katika enzi mpya, kuwaleta watu wote katika ulimwengu mwingine. Niliporudi katika “nchi Yangu,” Nilianza sehemu nyingine tena ya kazi katika mpango Wangu wa asili, ili mwanadamu aje kunijua zaidi.
Jumatatu, 30 Oktoba 2017
Kutanafusi kwa Mwenye Uweza
Kutanafusi kwa Mwenye Uweza
Mwenyezi Mungu alisema, Kunayo siri kubwa moyoni mwako. Huifahamu kamwe kwa sababu umekuwa ukiishi katika ulimwengu usio na mwanga unaoangaza. Moyo wako na roho yako vimechukuliwa mateka na yule mwovu. Macho yako yamefunikwa na giza; huwezi kuliona jua angani, wala nyota ikimetameta wakati wa usiku. Masikio yako yamezibwa na maneno ya udanganyifu na husikii sauti ya Yehova ingurumayo kama radi, wala sauti ya maji yatiririkayo kutoka katika kiti cha enzi. Umepoteza kila kitu ambacho kilipaswa kuwa chako na kila kitu ambacho mwenye Uweza alikupa. Umeingia katika bahari ya uchungu isiyokuwa na mwisho, pasipo uwezo wa kukuokoa, hukuna matumaini ya kuishi, umeachwa ukipambana na kuzunguka zunguka tu.… Tokea wakati huo, huwezi kuepuka kuteswa na yule mwovu, uko mbali na baraka za mwenye Uweza, mbali na kukimu kwa mwenye Uweza, na unaenenda katika njia ambayo huwezi kurejea nyuma tena.
Jisajili kwenye:
Machapisho (Atom)








