Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo kazi-ya-Mungu-ya-siku-za-mwisho. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo kazi-ya-Mungu-ya-siku-za-mwisho. Onyesha machapisho yote

Jumapili, 18 Machi 2018

Umeme wa Mashariki | Kazi na Kuingia (8)

Umeme wa Mashariki, Kanisa la Mwenyezi Mungu, wokovu,

Umeme wa Mashariki | Kazi na Kuingia (8)


Mwenyezi Mungu alisema, Nimezungumza mara nyingi sana kwamba kazi ya Mungu ya siku za mwisho ni kwa ajili ya kubadilisha roho ya kila mtu, kubadilisha nafsi ya kila mtu, ili kwamba moyo wake, ambao umeteseka sana na kiwewe, uwe umebadilishwa, hivyo kuokoa nafsi yake, ambayo imeumizwa kwa kina zaidi na Shetani; ni kwa sababu ya kuamsha roho za watu, kuyeyusha mioyo yao baridi, na kuwaruhusu kurudisha nguvu za ujana. Haya ndiyo mapenzi makubwa ya Mungu. Weka pembeni mazungumzo ya ni namna gani maisha na uzoefu wa mwanadamu ni ya kiburi au ya kina; mioyo ya watu itakapokuwa imeamshwa, wanapokuwa wameamshwa kutoka kwa ndoto zao na kujua kikamilifu madhara yaliyoletwa na joka kuu jekundu, kazi ya huduma ya Mungu itakuwa imekamilika. Siku ambayo kazi ya Mungu itakuwa imekamilika ni wakati ambapo mwanadamu ataanza rasmi njia ya imani sahihi kwa Mungu.

Jumatatu, 12 Machi 2018

Swahili Gospel Movie "Vunja Pingu Na Ukimbie" | Bwana ni Mchungaji Wangu


Swahili Gospel Movie “Vunja Pingu Na Ukimbie” | Bwana ni Mchungaji Wangu


Utambulisho


Lee Chungmin alikuwa mzee wa kanisa fulani huko Seoul, Korea ya Kusini. Kwa zaidi ya miaka ishirini, alimtumikia Bwana kwa shauku kubwa, akamakinika kikamilifu juu ya kusoma Biblia. Akifuatia mfano wa viongozi wake wa kidini, alidhani kuwa kumwamini Bwana kulimaanisha kuiamini Biblia, na kwamba kuwa na imani katika Biblia kulikuwa sawa kabisa na kuwa na imani katika Bwana. Aliamini kwamba almuradi angeshika Biblia, angenyakuliwa kuingia katika ufalme wa mbinguni. Dhana hizi zilimbana kama jozi ya pingu, zikimzuia kufuata nyayo za Mungu na kumwamini Mungu. Matokeo yake, Lee Chungmin kamwe hakufikiria kuchunguza kazi ya Mwenyezi Mungu ya siku za mwisho …