Je, ni desturi ngapi za kidini unazozizingatia? Ni mara ngapi wewe umeasi dhidi ya neno la Mungu na kwenda kwa njia yako mwenyewe? Ni mara ngapi wewe umetia katika vitendo neno la Mungu kwa sababu wewe kwa kweli unajali mizigo Aliyobeba na unatafuta kutimiza mapenzi Yake? Lielewe neno la Mungu na uliweke katika vitendo. Kuwa mwenye maadili katika vitendo na matendo yako; huku si kutii sheria au kufanya hivyo shingo upande kwa ajili ya kujionyesha. Badala yake, haya ni kutenda ukweli na kuishi kulingana na neno la Mungu. Kutenda kama huku pekee ndiko hutosheleza Mungu. Desturi yoyote inayompendeza Mungu si kanuni bali ni kutenda ukweli.
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo kutenda-ukweli. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo kutenda-ukweli. Onyesha machapisho yote
Jumatano, 31 Julai 2019
Jumatano, 12 Desemba 2018
Kuhusu Maisha ya Kawaida ya Kiroho
Kuhusu Maisha ya Kawaida ya Kiroho
Muumini lazima awe na maisha ya kawaida ya kiroho huu ni msingi wa kupitia maneno ya Mungu na kuingia katika hali halisi. Sasa hivi, je, maombi yote, kule kuja karibu na Mungu, kuimba, kusifu, kutafakari, na kule kujaribu kuelewa maneno ya Mungu ambayo mnatenda yanafikia viwango vya maisha ya kawaida ya kiroho? Hakuna kati yenu aliye wazi sana juu ya hili. Maisha ya kawaida ya kiroho hayakomi tukwa ombi, wimbo, maisha ya kanisa, kula na kunywa maneno ya Mungu, na matendo mengine kama haya, bali yana maana ya kuishi maisha ya kiroho yaliyo mapya na ya kusisimua.
Jumanne, 28 Agosti 2018
Umeme wa Mashariki Ushuhuda wa Kuipitia Hukumu | Mabadiliko ya Kweli Humaanisha Nini?
π»Umeme wa Mashariki Ushuhuda wa Kuipitia Hukumu | Mabadiliko ya Kweli Humaanisha Nini?π»
ππ~~~*******~~~π»π»π»~~~******~~~ππ
Jinru Mji wa Nanyang, Mkoa wa Henan
Wakati ndugu wa kiume au wa kike alipoonyesha dosari zangu au hakusikiza kauli yangu ama sikuhisi kushawishika au nilibishana nao. Nilijutia vitendo vyangu baadaye, lakini nilipokabiliwa na mambo haya, sikuweza kujizuia mwenyewe kuifichua tabia yangu potovu. Nilisumbuliwa na hili kwa kina, na nikafikiri: Kwa nini maneno ya wengine yanaweza kuniaibisha hadi kukasirika?
Jumapili, 26 Agosti 2018
Kujijua kwa Hakika kwa Kuuelewa Ukweli Tu
Kujijua kwa Hakika kwa Kuuelewa Ukweli Tu
Wenwen Mji wa Changchun, Mkoa wa Jilin
Kwa maoni yangu, daima nililidhani kwamba mradi matendo ya nje yalionekana ya kufaa ambapo watu hawangeweza kuona upotovu wowote, basi lilichukuliwa kuwa mabadiliko. Kwa hiyo, nilizingatia kwa namna ya kipekee matendo ya nje katika kila kitu nilichokifanya. Nilijali tu kuhusu kama matendo yangu yalikuwa sahihi au la, na mradi tabia zangu za nje na matendo yalikuwa ya maana, nilikuwa sawa. Nilipokabiliwa na upogolewaji, nilijali tu kama kulikuwa na kitu kibaya na matendo yangu. Ningeridhishwa tu kama ningekanushwa katika matendo yangu.
Jumamosi, 7 Julai 2018
Vigezo vya Mtu Mwema Kwa Dhati
Vigezo vya Mtu Mwema Kwa Dhati
Moran Mji wa Linyi, Mkoa wa Shandong
Tangu nilipokuwa mtoto, siku zote nilishikiza umuhimu mkubwa kwa jinsi watu wengine walivyoniona na ukadiriaji wao kwangu. Ili niweze kupata sifa kutoka kwa wengine kwa kila kitu nilichokifanya, sikubishana na yeyote asilani wakati wowote kitu chochote kilichoibuka, ili kuepuka kuharibu picha nzuri watu wengine walikuwa nayo kwangu. Baada ya kuikubali kazi ya Mungu katika siku za mwisho, niliendelea kwa njia hii, nikizingatia kwa kila njia iwezekanayo picha nzuri ambayo ndugu zangu wa kiume na wa kike walikuwa nayo kwangu. Hapo awali, wakati nilipokuwa ninasimamia kazi, kiongozi wangu mara nyingi angesema kwamba utendaji wangu ulikuwa kama "bwana ndiyo," wala sio utendaji wa mtu ambaye huweka ukweli katika vitendo.
Jumanne, 3 Julai 2018
Kumwamini Mungu Lazima Kulenge Uhalisi, Si Tamaduni za Kidini
Kumwamini Mungu Lazima Kulenge Uhalisi, Si Tamaduni za Kidini
Mwenyezi Mungu alisema, Je, ni desturi ngapi za kidini unazozizingatia? Ni mara ngapi wewe umeasi dhidi ya neno la Mungu na kwenda kwa njia yako mwenyewe? Ni mara ngapi wewe umetia katika vitendo neno la Mungu kwa sababu wewe kwa kweli unajali mizigo Aliyobeba na unatafuta kutimiza mapenzi Yake? Lielewe neno la Mungu na uliweke katika vitendo. Kuwa mwenye maadili katika vitendo na matendo yako; huku si kutii sheria au kufanya hivyo shingo upande kwa ajili ya kujionyesha. Badala yake, haya ni kutenda ukweli na kuishi kulingana na neno la Mungu. Kutenda kama huku pekee ndiko hutosheleza Mungu. Desturi yoyote inayompendeza Mungu si kanuni bali ni kutenda ukweli.
Jumatano, 20 Juni 2018
Uzoefu wa Kutenda Ukweli
Uzoefu wa Kutenda Ukweli
Hengxin Jiji la Zhuzhou, Mkoa wa Hunan
Sio muda mrefu mno uliopita, nilisikia "Ushirika na Kuhubiri Kuhusu Kuingia kwa Maisha," jambo ambalo lilinielekeza kuelewa kwamba ni wale tu wanaotenda ukweli wanaoweza kupata ukweli na hatimaye kuwa wale ambao wanaomiliki ukweli na ubinadamu hivyo kupata kibali cha Mungu. Kuanzia hapo kwendelea, kwa makusudi nilifanya jitihada za kuunyima mwili wangu na kutenda ukweli katika maisha yangu ya kila siku. Wakati fulani baadaye, nilitambua kwa furaha kwamba ningeweza kutenda ukweli kiasi. Kwa mfano, siku za nyuma niliogopa kuonyesha upande wangu mwovu kwa wengine. Sasa kwa makusudi nilikuwa wazi na ndugu wa kiume na wa kike, nikichangua tabia yangu potovu.
Jumamosi, 2 Juni 2018
Kupata Ahueni kwa Njia ya Kumwamini Mungu
Kupata Ahueni kwa Njia ya Kumwamini Mungu
Zhuanbian Mji wa Shanghai
Ingawa nilikuwa nikimfuata Mungu kwa miaka mingi, nilikuwa karibu sijafanya maendeleo yoyote na kuingia kwangu katika maisha, na hii ilinifanya nihisi kuwa na wasiwasi sana. Hasa wakati niliposikia rekodi ya mahubiri juu ya kuingia kwa maisha, na kusikia mtu aliyetumiwa na Roho Mtakatifu akizungumza na ndugu wa kiume na wa kike waliokuwepo na kusikiliza mahubiri, nilihisi nikiwa nimejawa na wasiwasi nikimsikia akisema jambo kama hili, "Nyinyi sasa mnamwamini Mungu na mmeonja uzuri wa ukimbizaji wa ukweli.
Jumatano, 23 Mei 2018
Umeme wa Mashariki | Uso halisi wa Mtu Anayedaiwa Kuwa Mtu Mzuri
Umeme wa Mashariki | Uso halisi wa Mtu Anayedaiwa Kuwa Mtu Mzuri
Kemu Jiji la Zhumadian, Mkoa wa Henan
Katika mawazo yangu mwenyewe, daima nimejifikiria kuwa na ubinadamu mzuri. Nimefikiria hivi kwa sababu, majirani zangu mara nyingi walinisifu mbele ya wazazi wangu kwa kuwa mwenye busara na wa kuijali familia yetu; wakisema kuwa mimi nilikuwa kipenzi cha wazazi wangu. Baada ya kuolewa, wakwe zangu walinishukuru mbele ya majirani kwa kuwa wema na mtoto wao. Katika kitengo changu, kiongozi wangu alinisifu kwa kuwa mwaminifu na mwenye ustadi. Na tangu nikubali hatua hii ya kazi ya Mungu, nimekuwa mtii kwa chochote kanisa huniomba kufanya. Huwa sipingani kamwe na kiongozi hata nikikemewa na kiongozi huyu kwa kutofanya kazi nzuri, na mara nyingi mimi huwasaidia ndugu wa kiume na wa kike walio na mahitaji.
Jumatano, 11 Aprili 2018
Umeme wa Mashariki | Kuhusu Maisha ya Petro
![]() |
| Kuhusu Maisha ya Petro |
Umeme wa Mashariki | Kuhusu Maisha ya Petro
Mwenyezi Mungu alisema, Petro ni mfano ambao Mungu aliutambulisha kwa wanadamu, na yeye ni mtu mashuhuri anayejulikana vizuri. Kwa nini mtu mnyonge kama huyo aliwekwa mahala kama mfano na Mungu na amesifiwa na vizazi vya baadaye? Bila shaka, ni wazi kwamba hili halitenganishwi na maonyesho yake na azimio lake la upendo kwa Mungu. Kuhusu wapi ambapo moyo wa Petro wa upendo kwa Mungu ulionyeshwa na kile ambacho uzoefu wake wa maishani ulivyokuwa kwa kweli, lazima turudi kwa Enzi ya Neema kutazama tena desturi za wakati huo, ili kumwona Petro wa enzi hiyo.
Jisajili kwenye:
Machapisho (Atom)








