Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Mungu-Mwenyewe. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Mungu-Mwenyewe. Onyesha machapisho yote

Jumapili, 6 Januari 2019

3. Utofautishaji Kati ya Kristo wa Kweli na Makristo wa Uongo

Kanisa la Mwenyezi Mungu,Umeme wa Mashariki,Mwenyezi Mungu

Sura ya 6 Aina Mbalimbali za Utofautishaji Ambazo Unafaa Kumiliki katika Kusadiki Kwako kwa Mungu

3. Utofautishaji Kati ya Kristo wa Kweli na Makristo wa Uongo

Maneno Husika ya Mungu:
Mungu aliyepata mwili Anaitwa Kristo, na hivyo Kristo ambaye Anaweza kuwapa binadamu ukweli anaitwa Mungu. Hakuna kitu kikuu kuliko hiki, kwa kuwa Anayo hali ya Mungu, na ana tabia za Mungu, na hekima katika kazi Yake, ambayo haiwezi kupatikana kwa binadamu. Wale wanaojiita Kristo, walakini hawawezi kufanya kazi ya Mungu, ni matapeli. Kristo wa kweli sio tu udhihirisho wa Mungu duniani, bali pia, mwili hasa ulioigwa na Mungu kufanya na kutimiza kazi Yake kati ya wanadamu.

Alhamisi, 3 Januari 2019

5. Kupata Mwili Mara Mbili Kunakamilisha Umuhimu wa Kupata Mwili

Kanisa la Mwenyezi Mungu,Umeme wa Mashariki,Mwenyezi Mungu

Sura ya 5 Ukweli Kuhusu Mungu Kupata Mwili

5. Kupata Mwili Mara Mbili Kunakamilisha Umuhimu wa Kupata Mwili

Maneno Husika ya Mungu:
Kupata mwili mara ya kwanza kulikuwa kumkomboa mwanadamu kutoka katika dhambi kupitia mwili wa Yesu, hivyo, Aliokoa mwanadamu kutoka kwa msalaba, lakini tabia potovu ya kishetani ilibaki ndani ya mwanadamu. Kupata mwili mara ya pili si kwa ajili ya kuhudumu tena kama sadaka ya dhambi ila ni kuwaokoa kamilifu wale waliokombolewa kutoka kwa dhambi. Hii inafanyika ili wale waliosamehewa wakombolewe kutoka kwa dhambi zao, na kufanywa safi kabisa, na kupata mabadiliko ya tabia, hivyo kujikwamua kutoka kwa ushawishi wa Shetani wa giza na kurudi mbele za kiti cha enzi cha Mungu.

Jumanne, 1 Januari 2019

3. Tofauti Kati ya Kazi ya Mungu Mwenye Mwili na Kazi ya Roho

Sura ya 5 Ukweli Kuhusu Mungu Kupata Mwili

3. Tofauti Kati ya Kazi ya Mungu Mwenye Mwili na Kazi ya Roho

Maneno Husika ya Mungu:
Wokovu wa Mungu kwa mwanadamu haufanywi moja kwa moja kupitia njia ya Roho ama kama Roho, kwani Roho Wake hawezi kuguzwa ama kuonekana na mwanadamu, na hawezi kukaribiwa na mwanadamu. Kama Angejaribu kumwokoa mwanadamu moja kwa moja kwa njia ya Roho, mwanadamu hangeweza kupokea wokovu Wake. Na kama sio Mungu kuvalia umbo la nje la mwanadamu aliyeumbwa, mwanadamu hawangeweza kupokea wokovu huu. Kwani mwanadamu hawezi kumkaribia kwa njia yoyote ile, zaidi kama jinsi hakuna anayeweza kukaribia wingu la Yehova.

Jumamosi, 22 Desemba 2018

3. Umuhimu wa Kazi ya Mungu ya Hukumu na Kuadibu

Sura ya 4 Ukweli wa Kazi ya Mungu ya Siku za Mwisho

3. Umuhimu wa Kazi ya Mungu ya Hukumu na Kuadibu

Maneno Husika ya Mungu:
Kazi ya siku za mwisho ni kutenganisha vitu vyote kulingana na jinsi yavyo, kuhitimisha mpango wa usimamizi wa Mungu, kwa maana muda u karibu na siku ya Mungu imewadia. Mungu huwaleta wote ambao wameingia katika ufalme Wake, yaani, wale wote ambao wamekuwa waaminifu Kwake mpaka mwisho, katika enzi ya Mungu Mwenyewe. Hata hivyo, kabla ya kuja kwa enzi ya Mungu Mwenyewe, kazi Atakayofanya Mungu si kutazama matendo ya mwanadamu wala kuchunguza maisha ya wanadamu, ila ni kuhukumu uasi wake, kwa maana Mungu atawatakasa wale wote wanaokuja mbele ya kiti Chake cha enzi.

Ijumaa, 7 Desemba 2018

Matamshi ya Mungu kwa Ulimwengu Mzimam | Utangulizi

"Matamshi ya Mungu kwa Ulimwengu Mzima" ni kundi la pili la matamshi yanayoonyeshwa na Kristo. Ndani yake, Kristo Anatumia utambulisho wa Mungu Mwenyewe. Yanajumlisha kipindi cha kuanzia Februari 20, 1992 hadi Juni 1, 1992, na yana jumla ya matamshi arobaini na saba. Namna, maudhui na mtazamo wa maneno ya Mungu katika matamshi haya hayafanani kabisa na "Maneno ya Roho kwa Makanisa." "Maneno ya Roho kwa makanisa" inafichua na kuongoza tabia ya watu ya nje na maisha yao rahisi ya roho. Hatimaye, inaisha kwa "majaribu ya watendaji huduma." Hata hivyo, "Matamshi ya Mungu kwa Ulimwengu Mzima," inaanza na hitimisho la utambulisho wa watu kama watendaji huduma na mwanzo wa maisha yao kama watu wa Mungu. 

Alhamisi, 22 Novemba 2018

nyimbo za kusifu na kuabudu | 76. Ni Mungu tu Ana Njia ya Uzima

Kanisa la Mwenyezi Mungu,Mwenyezi Mungu,Umeme wa Mashariki

nyimbo za kusifu na kuabudu | 76. Ni Mungu tu Ana Njia ya Uzima

I
Njia ya uzima si kitu ambacho mtu yeyote anaweza kuwa nacho;
si kitu ambacho mtu yeyote anaweza kuipata kwa urahisi.
Kwani uzima unatoka tu kwa Mungu,
ni Mungu Mwenyewe pekee Aliye na kiini cha uzima,
ni Mungu pekee aliye na njia ya uzima.
Hivyo ni Mungu pekee ndiye chanzo cha uzima,
na kisima cha maji ya uzima kinachotiririka milele.

Jumanne, 20 Novemba 2018

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Kazi ya Mungu na Kazi ya Mwanadamu

Kanisa la Mwenyezi Mungu,Mwenyezi Mungu,Umeme wa Mashariki
Ni kiasi gani cha kazi ya mwanadamu ni kazi ya Roho Mtakatifu na uzoefu wa mwanadamu ni kiasi gani? Hata sasa, tunaweza kusema kuwa watu bado hawayaelewi maswali haya, ambayo yote ni kwa sababu watu hawaelewi kanuni za utendaji kazi wa Roho Mtakatifu. Kazi ya mwanadamu Ninayoizungumzia, kimsingi, ni kwa kurejelea kazi za wale ambao wana kazi ya Roho Mtakatifu au wale ambao wanatumiwa na Roho Mtakatifu. Sizungumzii kazi ambayo inatokana na matakwa ya mwanadamu bali kazi ya mitume, watendaji kazi au kaka na dada wa kawaida waliopo katika mawanda ya kazi ya Roho Mtakatifu.

Jumanne, 13 Novemba 2018

Tamko la Tisini na Tisa

Kanisa la Mwenyezi Mungu,Mwenyezi Mungu,Umeme wa Mashariki
Kwa sababu mwendo wa kazi Yangu unaongeza kasi, hakuna anayeweza kuenda mwendo sawa na nyayo Zangu, na hakuna anayeweza kupenya akili Yangu, lakini hii ndiyo njia tu ambayo lazima isafiriwe. Hii ni “wafu” yaani wakati Ninapoongea kuhusu kufufuliwa kutoka kwa wafu (inarejelea kukosa uwezo wa kufahamu mapenzi Yangu, kukosa uwezo wa kuelewa kile Ninachomaanisha kutoka kwa maneno Yangu. Haya ni maelezo mengine ya “wafu”, na hayamaanishi kutelekezwa na Roho Wangu). Wakati nyinyi na Mimi tumebadilika kutoka kwa awamu hii hadi kwa mwili, basi maana ya awali ya kufufuliwa kutoka wafu itatimizwa (yaani, hii ni maana ya awali ya ufufuko kutoka kwa wafu).

Alhamisi, 8 Novemba 2018

Tamko la Kumi na Tano

Mwenyezi Mungu alisema, Kuonekana kwa Mungu tayari kumetokea katika makanisa yote. Roho ndiyo anayeongea, Yeye ni moto mkali, Yeye hubeba uadhama na Anahukumu; Yeye ni Mwana wa Adamu, liyevaa vazi lililofika kwa miguu, na kufungwa mshipi kwenye matiti na ukanda wa dhahabu. Kichwa Chake na nywele Zake ni nyeupe kama sufu nyeupe, na macho Yake ni kama mwale wa moto; na miguu Yake iko kama shaba iliyosuguliwa sana, kana kwamba imesafishwa katika tanuru; na sauti Yake kama sauti ya maji mengi.

Jumatatu, 5 Novemba 2018

Tamko la Mia Moja na Ishirini

Sayuni! Salamu! Sayuni! Ita kwa sauti! Nimerudi kwa ushindi, Nimerudi nikiwa mshindi! Watu wote! Harakisheni mpange foleni kwa utaratibu! Vitu vyote! Mtakuja kusimama kabisa, kwa sababu nafsi Yangu inaukabili ulimwengu mzima na nafsi Yangu inaonekana katika Mashariki ya dunia! Nani anayethubutu kutopiga magoti katika ibada? Nani anayethubutu kutosema kumhusu Mungu wa kweli? Nani anayethubutu kutoangalia juu kwa kumcha? Nani anayethubutu kutotoa sifa? Nani anayethubutu kutangaza kwa shangwe? Watu wangu wataisikia sauti Yangu, Wanangu watasalia ndani ya ufalme Wangu! Milima, mito, na vitu vyote vitashangilia bila kukoma, na kurukaruka bila kupumzika. 

Ijumaa, 2 Novemba 2018

Tamko la Themanini na Saba

Kanisa la Mwenyezi Mungu,Mwenyezi Mungu,Umeme wa Mashariki

Matamshi ya Mwenyezi MunguTamko la Themanini na Saba

Lazima uharakishe hatua na ufanye kile Nataka kufanya. Hii ni kusudi Langu lenye hamu kwenu. Inawezekana kuwa kwa wakati huu bado hamjaelewa maana ya maneno Yangu? Inawezekana kuwa bado hamjui kusudi Langu? Nimezungumza wazi zaidi na zaidi, na kusema mengi zaidi, lakini, je, ninyi hamjajitahidi kujaribu kuelewa maana ya maneno Yangu? Shetani, usifikiri kwamba unaweza kuharibu mpango Wangu! Wale wanaomtumikia Shetani, yaani, uzao wa Shetani (hii inahusu wale ambao wanamilikiwa na Shetani.

Jumatatu, 29 Oktoba 2018

Maneno ya Roho Mtakatifu | "Kazi ya Mungu na Kazi ya Mwanadamu" (Sehemu ya Kwanza)


Maneno ya Roho Mtakatifu | "Kazi ya Mungu na Kazi ya Mwanadamu" (Sehemu ya Kwanza)

Mwenyezi Mungu anasema, "Kile ambacho mwanadamu hukidhihirisha ni kile anachokiona, kupitia uzoefu na kukitafakari. Hata kama ni mafundisho au mitazamo, haya yote hufikiwa na fikra za mwanadamu. Bila kujali ukubwa wa kazi ya mwanadamu, haiwezi kuzidi mawanda ya uzoefu wa mwanadamu, kile ambacho mwanadamu huona, au kile ambacho mwanadamu anaweza kukitafakari au kuingia akilini mwake. Kile ambacho Mungu anadhihirisha ndivyo hivyo Mungu Mwenyewe alivyo, na hii ni nje ya uwezo wa mwanadamu, yaani, nje ya uwezo wa kufikiri kwa mwanadamu. Anadhihirisha kazi Yake ya kuwaongoza wanadamu wote, na hii haihusiani na undani wa uzoefu wa mwanadamu, badala yake inahusu usimamizi Wake. Mwanadamu anadhihirisha uzoefu wake wakati Mungu akidhihirisha hali Yake—hali hii ni tabia Yake ya asili na uko nje ya uwezo wa mwanadamu."
Sikiliza zaidi: Filamu za Injili

Jumamosi, 27 Oktoba 2018

Neno la Mungu | "Je, Utatu Mtakatifu Upo?"



Mwenyezi Mungu anasema, "Hii dhana ya Baba, Mwana, na Roho Mtakatifu ni upuuzi mtupu! Hili linamweka Mungu katika vitengo na kumgawanya kuwa nafsi tatu, kila moja ikiwa na hadhi na Roho; basi Atawezaje kuwa Roho mmoja na Mungu mmoja? Hebu niambie, je, mbingu na dunia na vyote vilivyomo viliumbwa na Baba, Mwana, au na Roho Mtakatifu? Wengine husema Waliviumba kwa pamoja. Basi ni nani alimkomboa mwanadamu? Alikuwa Roho Mtakatifu, Mwana, au Baba? Wengine husema ni Mwana aliyewakomboa wanadamu. Basi Mwana ni nani katika kiini? Siye kupata mwili kwa Roho wa Mungu? Mungu aliyepata mwili anamwita Mungu aliye Mbinguni Baba katika mtazamo wa mwanadamu aliyeumbwa.

Jumatano, 24 Oktoba 2018

Umeme wa Mashariki | Tamko la Sabini na Moja

Kanisa la Mwenyezi Mungu,Mwenyezi Mungu,Umeme wa Mashariki

Umeme wa Mashariki | Tamko la Sabini na Moja

Mimi wote Nimejiweka dhahiri kwenu, lakini kwa nini mnashindwa kutafakari maneno Yangu kwa mioyo na nafsi zenu zote? Kwa nini mnachukua maneno Yangu kama takataka? Je,yote Ninayosema ni makosefu? Je, maneno Yangu yamekupiga katika sehemu ya uzima? Daima kuchelewesha, daima kusita, kwa nini mnafanya mambo hivi? Je, Mimi sijaongea wazi? Nimesema mara nyingi sana kwamba maneno Yangu lazima yatafakariwe kwa makini, na lazima yazingatiwe kwa makini.

Jumanne, 23 Oktoba 2018

Tamko la Themanini na nane

 Tamko la Themanini na nane

Watu hawawezi tu kuwaza kiasi ambacho mwendo Wangu umezidisha kasi: Ni ajabu ambayo imetokea isiyoeleweka kwa mwanadamu. Tangu uumbaji wa dunia, mwendo Wangu umeendelea na kazi Yangu haijawahi kusimama. Ulimwengu wote hubadilika siku kwa siku na watu pia wanabadilika mara kwa mara. Hizi zote ni kazi Zangu, mipango Yangu yote na hata zaidi, usimamizi Wangu—hakuna mtu anayejua au kuelewa hivi vitu. Wakati tu Mimi Mwenyewe Ninapowaambia, wakati tu Ninapowasiliana nanyi uso kwa uso kuihusu ndipo unajua kidogo; vinginevyo, hakuna kabisa anayejua mpango makini wa mpango Wangu wa usimamizi.

Jumamosi, 13 Oktoba 2018

Unajua Nini Kuhusu Imani?

Smiley face

Ndani ya binadamu, kunalo neno lisilokuwa la uhakika, ilhali binadamu hajui imani inajumuisha nini, na vilevile hajui ni kwa nini anayo imani. Binadamu huelewa kidogo sana, na binadamumwenyewe amepungukiwa sana; yeye anakuwa tu na imani ndani Yangu bila kujali na bila kujua. Ingawa hajui imani ni nini wala ni kwa nini anayo imani ndani Yangu, anaendelea kufanya hivyo kwa shauku mno.

210. Mungu Mwenye Mwili Anapendeza Sana

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, Nyimbo
I
Baada ya Mungu kupata mwili, akiishi maisha kati ya wanadamu,
Aliona upotovu wa mwanadamu, hali ya maisha yake.
Mungu katika mwili alihisi sana kutojiweza kwa mwanadamu,
jinsi gani wanavyodharaulika; Alihisi huzuni yake.
Mungu alipata huruma zaidi kwa hali ya binadamu,
na hangaiko zaidi kwa wafuasi Wake kutoka kwa silika Yake ya mwili.

Jumatano, 10 Oktoba 2018

Nyimbo za Mungu | Kiini cha Kristo Ni Mungu

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, Nyimbo za Mungu

Nyimbo za Mungu | Kiini cha Kristo Ni Mungu

I
Mungu anayekuwa mwili anaitwa Kristo,
hivyo Kristo anayeweza kuwapa watu ukweli anaitwa Mungu.
Si kupita kiasi kusema hivyo.
Kwani Ana kiini cha Mungu.
Ana tabia ya Mungu na hekima katika kazi Yake,
ambayo haifikiwi na mwanadamu.
Wale wanaojiita Kristo wenyewe ilhali hawawezi kufanya kazi Mungu ni wadanganyifu.

Jumapili, 3 Desemba 2017

Umeme wa Mashariki | Mazungumzo Mafupi Kuhusu “Ufalme wa Milenia Umefika”

Umeme wa Mashariki,  Kanisa la Mwenyezi Mungu, ufalme,

Umeme wa MasharikiMazungumzo Mafupi Kuhusu "Ufalme wa Milenia Umefika"

Mwenyezi Mungu alisema, Mnayaonaje maono ya Ufalme wa Milenia? Baadhi ya watu hutafakari sana kuuhusu na kusema kuwa Ufalme wa Milenia utadumu duniani kwa miaka elfu moja, hivyo basi ikiwa waumini wazee katika kanisa hawajaoa, je, wanapaswa kuoa? Familia yangu haina pesa, je napaswa nianze kutafuta pesa? … Ufalme wa Milenia ni nini? Je, mnajua? Watu ni nusu vipofu na wanapitia mateso mengi. Kwa hakika, Ufalme wa Milenia bado haujafika rasmi. Katika hatua ya kuwafanya wanadamu wakamilike, Ufalme wa Milenia ni mfano mdogo tu; katika kipindi cha Ufalme wa Milenia uliozungumziwa na Mungu, mwanadamu atakuwa amefanywa mkamilifu.

Jumatano, 15 Novemba 2017

Kupata Mwili Mara Mbili Kunakamilisha Umuhimu wa Kupata Mwili

Umeme wa Mashariki,  Mwenyezi Mungu,  Kanisa la Mwenyezi Mungu,
Kupata Mwili Mara Mbili Kunakamilisha Umuhimu wa Kupata Mwili

Kupata Mwili Mara Mbili Kunakamilisha Umuhimu wa Kupata Mwili



Mwenyezi Mungu alisema, Kila hatua ya kazi iliyofanywa na Mungu ina umuhimu wake mkubwa. Yesu alipokuja zamani, Alikuwa mwanaume, lakini Mungu anapokuja wakati huu Yeye ni mwanamke. Kutokana na hili, unaweza kuona kwamba Mungu aliwaumba mwanaume na mwanamke kwa ajili ya kazi Yake na Kwake hakuna tofauti ya jinsia. Roho Wake anapowasili, Anaweza kuchukua mwili wowote kwa matakwa Yake na mwili huo unaweza kumwakilisha Yeye.