Wimbo wa Kuabudu 2019 | "Mungu Anashuka na Hukumu" | Christ of the Last Days Has Appeared
Anapokuja chini katika taifa la joka kuu jekundu,
Mungu anageuka kuutazama ulimwengu na unaanza kutingika.
Je, kuna mahali popote ambapo hapatapata hukumu Yake?
Ama kuishi katika janga Analotoa?
Kila mahali Aendapo anamwaga mbegu ya janga,
lakini kupitia kwayo Anatoa wokovu na kuonyesha upendo Wake.
Maneno Husika ya Mungu:
Mabadiliko katika tabia hasa huhusu mabadiliko katika asili ya watu. Mambo ya asili ya mtu hayawezi kuonekana kutoka kwa mienendo ya nje; yanahusisha moja kwa moja thamani na umuhimu wa kuwepo kwake. Yaani, yanahusisha moja kwa moja mitazamo ya mtu kuhusu maisha na maadili yake, mambo yaliyo ndani kabisa ya nafsi yake, na kiini chake. Mtu ambaye hawezi kukubali ukweli hatakuwa na mabadiliko katika hali hizi. Ni kwa kupitia kazi ya Mungu pekee, kuingia kikamilifu katika ukweli, kubadili maadili na mitazamo yake kuhusu kuwepo na maisha, kulinganisha msoni yake na ya Mungu, na kuwa na uwezo wa kutii na kujitoa kabisa kwa Mungu ndio tabia zake zinaweza kusemekana zimebadilika.









