Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Ujenzi-wa-ufalme. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Ujenzi-wa-ufalme. Onyesha machapisho yote

Jumatano, 11 Aprili 2018

Umeme wa Mashariki | Ufafanuzi wa Tamko la Kumi

Umeme wa MasharikiUfafanuzi wa Tamko la Kumi

Mwenyezi Mungu alisema, Katika wakati wa ujenzi wa kanisa, Mungu alitaja ujenzi wa kanisa kwa nadra. Hata Alipotaja, Alifanya hivyo katika lugha ya wakati wa ujenzi wa kanisa. Mara tu Enzi ya Ufalme ilipokuja, Mungu alifuta mbinu na wasiwasi nyingine za wakati wa ujenzi wa kanisa mara mmoja na Hakuwahi tena kusema hata neno moja kuuhusu. Hii hasa ni maana ya msingi ya “Mungu Mwenyewe” ambaye daima ni mpya na kamwe si mzee.

Jumapili, 8 Aprili 2018

Umeme wa Mashariki | Tamko la Kwanza

Umeme wa Mashariki | Tamko la Kwanza

Mwenyezi Mungu alisema, Je, wale wanaoshuhudia maneno Yangu huyakubali kwa kweli? Je, mnanijua kwa kweli? Mmejifunza utiifu kweli? Ninyi hutumia rasilimali kwa ajili Yangu kwa uaminifu? Mmekuwa na ushuhuda thabiti, usiokubali kushindwa Kwangu mlipokabiliwa na joka kuu jekundu? Je, moyo wenu wa ibada hulifedhehesha kweli joka kuu jekundu? Ni kupitia tu kwa jaribio la maneno Yangu ndipo Naweza kutimiza lengo Langu la kulitakasa kanisa na kuwachagua wale wanaonipenda Mimi kweli. Ni jinsi gani tena ambayo mtu yeyote angenielewa Mimi? Ni nani anaweza kuelewa uadhama Wangu, ghadhabu Yangu, na hekima Yangu kupitia kwa maneno Yangu? Nitakamilisha Nilichoanza, lakini bado ni Mimi nipimaye mioyo ya wanadamu.

Jumapili, 1 Aprili 2018

Umeme wa Mashariki | Tamko la Nane

Mwenyezi Mungu alisema, Ufunuo Wangu unapofika kilele chake, na wakati hukumu Yangu inapomalizika, utakuwa wakati ambao watu Wangu wote wanafichuliwa na kufanywa wakamilifu. Nyayo zangu hukanyaga kila pembe ya ulimwengu katika hali ya kutafuta kwa kudumu wale wenye kupendeza nafsi Yangu na wanafaa kwa matumizi Yangu. Nani anaweza kusimama na kushirikiana na Mimi? Upendo wa mwanadamu Kwangu ni mdogo mno na imani yake Kwangu ni ndogo ajabu.