Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo neema. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo neema. Onyesha machapisho yote

Jumamosi, 20 Julai 2019

Katika Imani Yako kwa Mungu Unapaswa Kumtii Mungu

Kanisa la Mwenyezi Mungu,Umeme wa Mashariki,Maisha ya kanisa

Kwa nini unamwamini Mungu? Watu wengi wanafadhaishwa na swali hili. Siku zote wana mitazamo tofauti kuhusu Mungu wa vitendo na Mungu wa mbinguni, jambo linaloonyesha kwamba wanamwamini Mungu sio ili wamtii, bali kupata manufaa fulani, au kuepuka mateso ya janga. Wakati huo tu ndipo wanakuwa watiifu kwa kiasi fulani, lakini utii wao ni wa masharti, ni kwa ajili ya matarajio yao wenyewe, na kushinikiziwa. Hivyo: kwa nini unamwamini Mungu? Ikiwa ni kwa ajili ya matarajio yako tu, na majaliwa yako, basi ni bora zaidi usingeamini. Imani kama hii ni kujidanganya, kujihakikishia, na kujishukuru.

Alhamisi, 10 Januari 2019

7. Tofauti Kati Ya Matendo Mazuri ya Nje na Mabadiliko Katika Tabia

Sura ya 6 Aina Mbalimbali za Utofautishaji Ambazo Unafaa Kumiliki katika Kusadiki Kwako kwa Mungu

7. Tofauti Kati Ya Matendo Mazuri ya Nje na Mabadiliko Katika Tabia

Maneno Husika ya Mungu:
Mabadiliko katika tabia hasa huhusu mabadiliko katika asili ya watu. Mambo ya asili ya mtu hayawezi kuonekana kutoka kwa mienendo ya nje; yanahusisha moja kwa moja thamani na umuhimu wa kuwepo kwake. Yaani, yanahusisha moja kwa moja mitazamo ya mtu kuhusu maisha na maadili yake, mambo yaliyo ndani kabisa ya nafsi yake, na kiini chake. Mtu ambaye hawezi kukubali ukweli hatakuwa na mabadiliko katika hali hizi. Ni kwa kupitia kazi ya Mungu pekee, kuingia kikamilifu katika ukweli, kubadili maadili na mitazamo yake kuhusu kuwepo na maisha, kulinganisha msoni yake na ya Mungu, na kuwa na uwezo wa kutii na kujitoa kabisa kwa Mungu ndio tabia zake zinaweza kusemekana zimebadilika.

Ijumaa, 4 Januari 2019

1. Unafaa Kutofautisha Vipi Kati ya Kazi ya Mungu na ya Mwanadamu?

Kanisa la Mwenyezi Mungu,Umeme wa Mashariki,Mwenyezi Mungu

Sura ya 6 Aina Mbalimbali za Utofautishaji Ambazo Unafaa Kumiliki katika Kusadiki Kwako kwa Mungu

1. Unafaa Kutofautisha Vipi Kati ya Kazi ya Mungu na ya Mwanadamu?

Maneno Husika ya Mungu:
Katika Enzi ya Neema, Yesu pia Alinena mengi na kufanya kazi nyingi. Alikuwaje tofauti na Isaya? Alikuwaje tofauti na Danieli? Je, Alikuwa nabii? Ni kwa nini inasemekana kwamba Yeye ni Kristo? Kuna tofauti gani baina yao? Wote walikuwa wanadamu walionena maneno, na maneno yao yalionekana sawa kwa wanadamu. Wote walinena na kufanya kazi. Manabii wa Agano la Kale walitoa unabii, na vivyo hivyo, pia na Yesu.

Jumamosi, 29 Desemba 2018

5. Unahitaji Kusadiki Vipi Mungu Ili Kuweza Kuokolewa na Kufanywa Kuwa Mtimilifu?

Kanisa la Mwenyezi Mungu,Umeme wa Mashariki,Mwenyezi Mungu

Sura ya 4 Ukweli wa Kazi ya Mungu ya Siku za Mwisho

5. Unahitaji Kusadiki Vipi Mungu Ili Kuweza Kuokolewa na Kufanywa Kuwa Mtimilifu?

Maneno Husika ya Mungu:
Kufanya muhtasari wa kuishika njia ya Petro katika kumwamini Mungu, ni kuishika njia ya kufuatilia ukweli, ambayo pia ni njia ya kujijua na kubadilisha tabia ya mtu. Ni kwa kuishika tu njia ya Petro ndio mtu atakuwa anashika njia ya kukamilishwa na Mungu. Mtu lazima aelewe hasa jinsi ya kuishika njia ya Petro na jinsi ya kuiweka katika vitendo. Kwanza, mtu lazima aweke kando madhumuni yake mwenyewe, shughuli zisizofaa, na hata familia yake na vitu vyote vya mwili wake.

Jumamosi, 15 Desemba 2018

Tabia Yako Ni Duni Sana!

Kanisa la Mwenyezi Mungu,Umeme wa Mashariki,Mwenyezi Mungu

Tabia Yako Ni Duni Sana!

Mwenyezi Mungu alisema, Ninyi nyote mmeketi katika viti vya kifahari, mkiwafundisha wale wa vizazi vijana ambao ni wa aina yenu, ukiwafanya waketi nawe. Je, mngekosaje kujua kwamba wale "watoto" wenu walikuwa tayari hawana pumzi, na kwamba hawakuwa na kazi Yangu zamani? Utukufu Wangu huangaza kutoka nchi ya Mashariki hadi nchi ya Magharibi, lakini wakati utukufu Wangu huenea mpaka mwisho wa dunia na wakati unapoanza kuinuka na kuangaza, Nitaondoa utukufu wa Mashariki na kuuletea Magharibi ili kwamba hawa watu wa giza katika Mashariki ambao wameniacha Mimi watakuwa bila mwanga unaong'aa kuanzia hapo kwendelea.

Jumatatu, 3 Desemba 2018

Umuhimu wa Kuukoa Uzao wa Moabu

Katika miaka hii miwili hadi mitatu ya kazi, kile kilichopaswa kutimizwa katika kazi ya hukumu iliyofanyika juu yenu kimetimizwa kimsingi. Watu wengi wamesahau matarajio na kudura yao ya baadaye. Hata hivyo, inapotajwa kuwa ninyi ni uzao wa Moabu, wengi wenu huchukizwa sana—nyuso zenu hubadilika, vinywa vyenu hupinda, na macho yenu hukodolea. Hamuwezi kabisa kuamini kwamba ninyi ni uzao wa Moabu. Moabu ilifukuzwa hadi nchi hii baada ya kulaaniwa. Ukoo wa wana wa Moabu umerithishwa mpaka leo, na ninyi nyote ni uzao wake. Hakuna kitu ambacho Ninaweza kufanya—nani aliyekusababisha uzaliwe katika nyumba ya Moabu? Ninakuhurumia na Siko radhi uwe hivi, lakini ukweli hauwezi kubadilishwa na watu.

Jumapili, 25 Novemba 2018

Maneno ya Kristo Alipokuwa Akitembea Makanisani (I) | Amri za Enzi Mpya

Kanisa la Mwenyezi Mungu,Mwenyezi Mungu,Umeme wa Mashariki

Maneno ya Kristo Alipokuwa Akitembea Makanisani (I) | Amri za Enzi Mpya

Mmeambiwa kuwa mjiandae kwa maneno ya Mungu, ya kuwa pasipo kujali kilichoandaliwa juu yenu, yote yamepangwa kwa mkono wa Mungu, na kwamba hakuna haja ya kuomba kwa bidii au kusali kwenu—haina maana. Ilhali kulingana na hali ya sasa, shida za kiutendaji mnazokumbana nazo hazitafakariki kwenu. Kama mnasubiri mipango ya Mungu tu, basi hatua zenu zitakaa zaidi, na kwa wale wasiojua kupitia kutakuwa na kulaza damu kwingi. Kwa hivyo, ikiwa umeshindwa kabisa kuyalewa mambo haya, basi umechanganyikiwa na kuwa mpumbavu katika uzoefu wako.

Alhamisi, 15 Novemba 2018

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Utangulizi

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Utangulizi

Mnamo Februari 11, mwaka wa 1991, Mungu alitoa tamko Lake la kwanza katika kanisa ambalo lilikuwa na athari isiyo ya kawaida kwa kila mmoja wa watu walioishi katika mkondo wa Roho Mtakatifu wakati huo. Tamko hili lilitaja yafuatayo: “Makazi ya Mungu yameonekana” na “Mkuu wa ulimwengu, Kristo wa siku za mwisho—Yeye ni Jua linalong’aa.” Kwa maneno haya ya maana sana, watu hawa wote waliletwa katika ulimwengu mpya. Wale wote waliosoma tamko hili walihisi maelezo ya kazi mpya, kazi kuu ambayo Mungu alikuwa karibu kuanzisha.

Jumapili, 21 Oktoba 2018

Dondoo za Filamu za Injili "Sauti Nzuri Ajabu" (4) - Je, Kusamehewa kwa Dhambi Zetu Ndiko Kweli Tiketi kuelekea Ufalme wa Mbinguni?


Watu wengi katika dini wanafikiria kuwa wamezikiri dhambi zao na kuzitubu baada ya kumsadiki Bwana, hivyo wamekombolewa, na wameokolewa kwa neema. Wakati Bwana atakapokuja, atawainua moja kwa moja hadi kwenye ufalme wa mbinguni, na haiwezekani Yeye kufanya kazi ya utakaso na wokovu. Je, mtazamo huu unalingana na uhalisi wa kazi ya Mungu? Inasemekana kwenye Biblia: "Utakatifu, bila huu hakuna mwanadamu atakayemwona Bwana" (Waebrania 12:14).

Jumanne, 9 Oktoba 2018

211. Mungu Katika Mwili Hufanya Kazi Kimya ili Kuwaokoa Wanadamu

I
Mungu alipata mwili, akabaki kujificha miongoni mwa wanadamu
ili kufanya kazi mpya, kutuokoa kutoka katika upotovu.
Anahifadhi maelezo.
Kwa mipango Aliyoifanya, Yeye hufanya kazi Yake hatua kwa hatua.
Maneno Yake yanaongezeka kila siku,
yakifariji, kukumbusha, kushutumu, na kuonya.

Jumapili, 23 Septemba 2018

Hukumu Ni Mwanga(II)

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, neema

Hukumu Ni Mwanga (II)

Zhao Xia Mkoa wa Shandong
Baada ya kupitia adabu na hukumu ya Mungu wakati huu, nilipata ujuzi fulani juu ya mwelekeo wangu wa kuzingatia heshima na hadhi, na nilikuwa radhi kuachana na mwili wangu na kumwamini Mungu na kutekeleza wajibu wangu kulingana na mahitaji Yake. Hata hivyo, uchafu wangu uliotokana na sumu za Shetani zilikuwa zimezama sana. Kina cha nafsi yangu bado kilikuwa kinatawaliwa na ushawishi wa Shetani.

Ijumaa, 14 Septemba 2018

5. Kwa Nini Yasemekana Kwamba Kuzijua Awamu Tatu za Kazi ya Mungu Ndiyo Njia ya Kujua Mungu?

Sura ya 3 Ukweli Kuhusu Awamu Tatu za Kazi ya Mungu

5. Kwa Nini Yasemekana Kwamba Kuzijua Awamu Tatu za Kazi ya Mungu Ndiyo Njia ya Kujua Mungu?

(Fungu Lililochaguliwa la Neno la Mungu)
Kujua Hatua Tatu za Kazi ya Mungu Ndiyo Njia ya Kumjua Mungu
Kazi ya kumsimamia mwanadamu imegawanywa katika hatua tatu, na ina maana kuwa kazi ya kumwokoa mwanadamu imegawanywa katika hatua tatu. Hatua hizi tatu hazihusishi kazi ya kuuumba ulimwengu, ila ni hatua tatu za kazi ya Enzi ya Sheria, Enzi ya Neema, na Enzi ya Ufalme. Kazi ya kuiumba dunia ilikuwa kazi ya kusababisha uwepo wa wanadamu wote. Haikuwa kazi ya kumwokoa mwanadamu, na haina uhusiano na kazi ya kumwokoa mwanadamu, kwa kuwa dunia ilipoumbwa mwanadamu hakuwa amepotoshwa na Shetani, na hivyo hakukuwa na haja ya kutekeleza kazi ya kumwokoa mwanadamu.

Jumanne, 31 Julai 2018

Umeme wa Mashariki | Tamko la Arubaini na Saba

Umeme wa Mashariki | Tamko la Arubaini na Saba

Ili kuwafanya wanadamu wawe wakomavu katika maisha na kuwafanya wanadamu na Mimi tuweze kutimiza matokeo katika udhanifu wetu wa pamoja, Nimewaendeka wanadamu kila mara, Nikiwakubalia kupata chakula na riziki kutoka kwa neno Langu na kupokea utele Wangu kutoka kwake. Sijawahi kuwapa wanadamu sababu ya kuaibika, lakini mwanadamu hafikirii hisia Zangu kamwe. Hii ni kwa sababu wanadamu hawana hisia na "hudharau" vitu vyote isipokuwa Mimi. Kutokana na dosari za wanadamu, Nawasikitikia sana na hivyo Nimefanya kila Niwezalo, ili waweze kufurahia utele wa dunia hadi kiasi cha kuiridhisha mioyo yao kwa wakati wao duniani. Simtendei mwanadamu bila haki na kwa kuzingatia watu walionifuata kwa miaka mingi, Nimekuwa na moyo wa huruma kwao. Ni kama kwamba Siwezi kujizuia kuweka mikono Yangu juu yao ili kufanya kazi Yangu.

Jumapili, 10 Juni 2018

Umeme wa Mashariki | Ufafanuzi wa Tamko la Kumi na Sita

Umeme wa Mashariki, Kanisa la Mwenyezi Mungu, neno la Mungu,

Umeme wa MasharikiUfafanuzi wa Tamko la Kumi na Sita

Mwenyezi Mungu alisema, Kwa watu, Mungu ni mkuu mno, mwenye utele mno, wa ajabu mno, Asiyeeleweka mno; machoni pao, maneno ya Mungu hupaa juu, na huonekana kama kazi bora sana ya ulimwengu. Lakini kwa vile watu wana kasoro nyingi sana, na akili zao ni za kawaida sana, na, zaidi ya hayo, kwa kuwa uwezo wao wa kukubali ni haba mno, bila kujali vile Mungu hunena maneno Yake kwa dhahiri, wanabaki palepale bila kutikisika, kana kwamba wana ugonjwa wa akili. Wanapokuwa na njaa, hawaelewi kwamba lazima wale, wanapokuwa na kiu, hawaelewi kwamba lazima wanywe maji;

Jumapili, 15 Aprili 2018

Mungu Kuja Duniani na Kuwa Sadaka ya Dhambi

Mungu Kuja Duniani na Kuwa Sadaka ya Dhambi


Kuja kwa Bwana Yesu hakumalizi tu enzi nzee iliyofungwa na sheria, na kuwaleta wanadamu kwa enzi mpya, lakini pia kunaboresha uhusiano kati ya mwanadamu na Mungu, na kunaashiria mwanzo mpya, hatua mpya ya kuanzia, kwa kazi ya Mungu ya usimamizi miongoni mwa wanadamu.
Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, Yesu,



Umeme wa Mashariki, Kanisa la Mwenyezi Mungu lilianzishwa kwa sababu ya kuonekana na kazi ya Mwenyezi Mungu, ujio wa pili wa Bwana Yesu, Kristo wa siku za mwisho. Linashirikisha wale wote ambao wanaikubali kazi ya Mwenyezi Mungu katika siku za mwisho na ambao wameshindwa na kuokolewa kwa maneno Yake. Liliasisiwa kikamilifu na Mwenyezi Mungu mwenyewe na linaongozwa naye kama Mchungaji. Kwa hakika halikuanzishwa na mtu. Kristo ni ukweli, njia, na uzima. Kondoo wa Mungu husikia sauti ya Mungu. Mradi unasoma maneno ya Mwenyezi Mungu, utaona kuwa Mungu ameonekana.

Jumapili, 1 Aprili 2018

Umeme wa Mashariki | Tamko la Saba

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, ushuhuda,
Tamko la Saba


Umeme wa Mashariki | Tamko la Saba

Mwenyezi Mungu alisema, Matawi yote ya magharibi yanapaswa kuisikiliza sauti Yangu:
Je, mmekuwa waaminifu Kwangu hapo awali? Je, mmekuwa mkiyasikia maneno Yangu mazuri ya ushauri? Je, mnayo matumaini ambayo ni halisi na yasiyo na mashaka? Utiifu wa mwanadamu, mapenzi yake, imani yake—hamna kipatikanacho ila kutoka Kwangu, hamna hata kimoja ila kilichotawazawa na Mimi.

Jumanne, 13 Machi 2018

Umeme wa Mashariki | Tamko la Thelathini na Tano

Umeme wa Mashariki, Kanisa la Mwenyezi Mungu, neema,

Umeme wa Mashariki | Tamko la Thelathini na Tano


Mwenyezi Mungu alisema, Nimeanza kutenda kazi Yangu kati ya wanadamu, kuwakubalia kuishi mkondo mmoja Nami. Nitakamilisha kazi Yangu nikiwa kati yao, maana wao ni vyombo Ninavyosimamia katika mpango Wangu wote wa usimamizi—na ni mapenzi Langu ili waweze kuwa watawala wa vitu vyote. Hivyo basi Naendelea kutembea kati ya wanadamu.

Jumanne, 6 Februari 2018

Swahili Gospel Song "Sala ya Watu wa Mungu" | Ishini Katika Upendo wa Mungu


Swahili Gospel Song "Sala ya Watu wa Mungu" | Ishini Katika Upendo wa Mungu


Utambulisho

Watu wa Mungu wanainuliwa mbele ya kiti Chake cha Enzi,
maombi mengi mioyoni mwao.
Mungu huwabariki wote wanaorejea Kwake;
wote wanaishi katika mwanga.
Omba Roho Mtakatifu alipe nuru neno la Mungu
ili kwamba tujue kikamilifu mapenzi ya Mungu.
Tunaomba watu wote walitunze sana neno la Mungu
na waje kutafuta kumjua Mungu.
Tunaomba Mungu atupe zaidi ya neema Yake,
ili tabia zetu ziweze kubadilika.
Tunaomba Mungu atufanye wakamilifu
ili tuwe moyo na mawazo moja pamoja na Yeye.
Tunaomba Mungu atufundishe nidhamu
ili tuweze kutimiza wajibu wetu Kwake.
Tunaomba Roho Mtakatifu kila siku atuongoze
kuhubiri na kumshuhudia Mungu.

Ijumaa, 19 Januari 2018

Swahili Gospel Song | "Njia Yote Pamoja na Wewe" Mungu ni Upendo


Swahili Gospel Song | "Njia Yote Pamoja na Wewe" Mungu ni Upendo

Utambulisho

Nilikuwa kama mashua, ikielea baharini.


Ulinichagua, na mahali pazuri Uliniongoza.


Sasa katika familia Yako, nikipewa joto na upendo Wako,


nina amani kabisa.


Unanibariki, Unatoa maneno Yako ya hukumu.


Bado sijui jinsi ninavyokosa kuithamini neema Yako.

Alhamisi, 16 Novemba 2017

Je, Wewe Ni Muumini wa Kweli wa Mungu?


Umeme wa Mashariki, Mwenyezi Mungu, Kanisa la Mwenyezi Mungu,

Je, Wewe Ni Muumini wa Kweli wa Mungu?


Mwenyezi Mungu alisema, Huenda ikawa safari yako ya imani katika Mungu imekuwa ndefu zaidi ya mwaka mmoja au miwili, na labda kwa maisha yako umestahimili ugumu mwingi miaka hii yote; au labda haujapitia ugumu na badala yake umepokea neema nyingi. Kuna uwezekano pia kuwa hujapitia ugumu wala kupokea neema, na badala yake umeishi maisha ya kawaida tu. Hiyo haijalishi, kwani wewe bado u mfuasi wa Mungu, kwa hivyo tushirikiane  kuhusu mada ya kumfuata Mungu.