Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Mwogope-Mungu. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Mwogope-Mungu. Onyesha machapisho yote

Jumatano, 24 Januari 2018

Kazi ya Mungu, Tabia ya Mungu, na Mungu Mwenyewe II | Kuhusu Ayubu

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, Biblia,
Matoleo ya kuteketezwa mapema asubuhi

Kuhusu Ayubu

Mwenyezi Mungu alisema, Baada ya kusikia namna Ayubu alivyopitia majaribio, kunao uwezekano kwamba wengi wenu watataka kujua maelezo zaidi kuhusu Ayubu mwenyewe, hasa kuhusiana na siri iliyomfanya akapata sifa za Mungu. Hivyo basi leo, hebu tuzungumzie kuhusu Ayubu!

Katika Maisha ya Kila Siku ya Ayubu Tunaona Utimilifu, Unyofu, Kumcha Mungu, na Kujiepusha na Maovu

Kama tutazungumzia Ayubu, basi lazima tuanze na namna ambavyo alitathminiwa kwa mujibu wa matamshi kutoka kwa kinywa cha Mungu mwenyewe: “hakuna hata mmoja aliye kama yeye duniani, mtu mkamilifu na mnyofu, mwenye kumcha Mungu, na kuuepuka uovu.”

Jumanne, 23 Januari 2018

Kazi ya Mungu, Tabia ya Mungu, na Mungu Mwenyewe II | 3. Shetani Amjaribu Ayubu Mara Nyingine Tena (Majipu Mabaya Yaupiga Mwili wa Ayubu)

3. Shetani Amjaribu Ayubu Mara Nyingine Tena (Majipu Mabaya Yaupiga Mwili wa Ayubu)

a. Maneno Yaliyotamkwa na Mungu
(Ayubu 2:3) BWANA akamwuliza Shetani, je, umemwangalia mtumishi wangu Ayubu, kwa kuwa hakuna hata mmoja aliye kama yeye duniani, mtu mkamilifu na mnyofu, mwenye kumcha Mungu, na kuuepuka uovu; naye hata sasa anashikamana na utimilifu wake, ujapokuwa ulinichochea dhidi yake, ili nimwangamize pasipo sababu.
(Ayubu 2:6) BWANA akamwambia Shetani, Tazama, yeye yumo mkononi mwako; lakini uutunze uhai wake.
b. Maneno Yaliyotamkwa na Shetani

Jumapili, 21 Januari 2018

Kazi ya Mungu, Tabia ya Mungu, na Mungu Mwenyewe II | C. Ayubu

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, Biblia,

Ukadiriaji wa Ayubu na Mungu na kwenye Biblia


C. Ayubu

1. Ukadiriaji wa Ayubu na Mungu na kwenye Biblia

    (Ayubu 1:1) Palikuwa na mtu katika nchi ya Uzi, jina lake aliitwa Ayubu; mtu huyo alikuwa mkamilifu na mnyoofu, na mmoja aliyemcha Mungu, na kuepukana na uovu .

    (Ayubu 1:5) Na ilikuwa hivyo, hizo siku za karamu zao zilipokuwa zimetimia, Ayubu aliwatuma na kuwatakasa, kisha akaamka asubuhi na mapema, na kutoa sadaka za kuteketezwa kulingana na hesabu yao wote ilivyokuwa; kwani Ayubu alisema, Inaweza kuwa kwamba wanangu wamefanya dhambi, na kumkufuru Mungu mioyoni mwao. Hivyo ndivyo Ayubu alivyofanya siku zote.