Jumanne, 10 Aprili 2018

Umeme wa Mashariki | Ufafanuzi wa Tamko la Kumi na Moja

Umeme wa MasharikiUfafanuzi wa Tamko la Kumi na Moja

Mwenyezi Mungu alisema, Kwa macho ya mwanadamu, inaonekana hakuna badiliko katika matamshi ya Mungu wakati wa kipindi hiki, ambalo ni kwa sababu watu hawawezi kuelewa sheria ambazo kwazo Mungu hunena, na hawafahamu muktadha wa maneno Yake. Baada ya kusoma maneno ya Mungu, watu hawaamini kwamba kuna mafumbo yoyote mapya katika maneno haya; hivyo, hawawezi kuishi maisha yaliyo mapya kiajabu, na badala yake huishi maisha yaliyokwama na yasiyokuwa na uhai. Lakini katika matamshi ya Mungu, tunaona kwamba kuna kiwango cha kina cha maana, kile kisichofahamika na pia kisichofikika na mwanadamu.

Jumatatu, 9 Aprili 2018

Umeme wa Mashariki | Tamko la Thelathini na Saba

Umeme wa MasharikiTamko la Thelathini na Saba

Mwenyezi Mungu alisema, Kotekote katika enzi, kazi yote Niliyoifanya—kila hatua ya kazi hiyo—imekuwa na mbinu Zangu zinazofaa za kazi. Ni kwa sababu ya hili ndio watu Wangu wapendwa wamekuwa watakatifu zaidi na zaidi, na wa kufaa zaidi na zaidi kwa matumizi Yangu. Kwa sababu hiyo hiyo, hata hivyo, jambo la kusikitisha ni kwamba kadri mbinu Zangu za kazi zinavyoongezeka, idadi ya watu inapungua, ambalo husababisha watu kuzama katika kutafakari. Bila shaka, Kazi Yangu leo sio tofauti na watu wengi wamejikuta tena katika kutafakari, kwa hiyo kwa sababu ya mabadiliko ya mbinu Zangu, kuna sehemu ya watu ambao watajiondoa. Inaweza kuelezwa kwa njia hii: Hili lilikuwa limeamuliwa na Mimi kabla, lakini halikufanywa na Mimi.

Umeme wa Mashariki | Tamko la Thelathini na Nne

Umeme wa MasharikiTamko la Thelathini na Nne

Mwenyezi Mungu alisema, Wakati mmoja Nilimwalika mwanadamu kama mgeni nyumbani Kwangu, lakini alikimbia huku na huko kwa sababu ya miito Yangu–kama kwamba, badala ya kumwalika kama mgeni, Nilikuwa nimemleta kwenye eneo la kuuawa. Kwa hiyo, nyumba yangu inaachwa tupu, kwa maana mwanadamu ameepukana Nami daima, na daima amejilinda dhidi Yangu. Hili limeniacha bila njia yoyote ya kutekeleza sehemu ya kazi Yangu, ambalo ni kusema, ni kama kwamba Nimeirudisha karamu Niliyomtayarishia, kwa maana mwanadamu hayuko radhi kuifurahia karamu hii, na kwa hiyo Sitamlazimisha kufanya hivyo. Lakini mwanadamu ghafula hujikuta akizongwa na njaa, kwa hiyo anakuja kubisha mlangoni Mwangu akiomba msaada Wangu—na Nikimwona amepata mashaka kama hayo, Ningewezaje kukosa kumsaidia?Hivyo, kwa mara nyingine Namwandalia mwanadamu karamu, ili aweze kuifurahia, na wakati huo tu ndio anahisi jinsi Ninavyopendeka, na hivyo anakuja kunitegemea.

Jumapili, 8 Aprili 2018

Umeme wa Mashariki | Tamko la Tatu

Umeme wa Mashariki | Tamko la Tatu

Mwenyezi Mungu alisema, Kwa kuwa mnaitwa watu Wangu, mambo hayapo kama yalivyokuwa; mnapaswa kusikiliza na kutii matamshi ya Roho Wangu, fuateni kwa karibu kazi Yangu, na msitenganishe Roho Wangu na mwili Wangu, maana kwa asili Sisi ni wamoja, na Hatujatengana. Yeyote ambaye hugawanya Roho na mwanadamu, akimthamini mwanadamu au Roho, atapata hasara, na ataweza tu watakunywa kutoka kwenye kikombe chao kichungu—ni hayo tu.

Umeme wa Mashariki | Tamko la Kwanza

Umeme wa Mashariki | Tamko la Kwanza

Mwenyezi Mungu alisema, Je, wale wanaoshuhudia maneno Yangu huyakubali kwa kweli? Je, mnanijua kwa kweli? Mmejifunza utiifu kweli? Ninyi hutumia rasilimali kwa ajili Yangu kwa uaminifu? Mmekuwa na ushuhuda thabiti, usiokubali kushindwa Kwangu mlipokabiliwa na joka kuu jekundu? Je, moyo wenu wa ibada hulifedhehesha kweli joka kuu jekundu? Ni kupitia tu kwa jaribio la maneno Yangu ndipo Naweza kutimiza lengo Langu la kulitakasa kanisa na kuwachagua wale wanaonipenda Mimi kweli. Ni jinsi gani tena ambayo mtu yeyote angenielewa Mimi? Ni nani anaweza kuelewa uadhama Wangu, ghadhabu Yangu, na hekima Yangu kupitia kwa maneno Yangu? Nitakamilisha Nilichoanza, lakini bado ni Mimi nipimaye mioyo ya wanadamu.

Jumamosi, 7 Aprili 2018

Umeme wa Mashariki | Tamko la Pili

Umeme wa MasharikiTamko la Pili

Mwenyezi Mungu alisema, Kufuata kuanza kazi kwa mtazamo mpya, kutakuwa na hatua mpya katika kazi Yangu. Kama ilivyo katika ufalme, Nitafanya mambo moja kwa moja kupitia kwa uungu, Nikiongoza kila hatua ya njia, sahihi hadi kwa maelezo madogo, na bila kutiwa najisi na nia za binadamu hata kidogo. Yafuatayo yanaeleza kwa muhtasari namna ya utekelezaji halisi: Kwa vile ni kupitia katika ugumu na usafishaji ndiyo wamepata jina la “watu”, na kama walivyo watu wa ufalme Wangu, lazima Niwafanye watii kwa mahitaji kali, ambayo ni ya juu kushinda mbinu za kazi Yangu kwa vizazi vilivyopita. Huu sio tu uhalisi wa maneno, bali pia la muhimu zaidi ni uhalisi wa kutenda, na hili lazima kwanza litimizwe. Katika kila neno na matendo, ni lazima watosheleze viwango vinachohitajika kwa watu wa ufalme, na mkosaji yeyote ataondolewa mara moja, ili kuzuia aibu kulijia jina Langu.

Umeme wa Mashariki | Tamko la Kumi

Umeme wa MasharikiTamko la Kumi

Mwenyezi Mungu alisema, Enzi ya Ufalme ni, hata hivyo, tofauti na nyakati za kale. Haihusu kile anachofanya mwanadamu. Badala yake, Mimi binafsi Natekeleza kazi Yangu baada ya kushuka duniani—kazi ambayo wanadamu hawawezi kuelewa wala kufanikisha. Tangu kuumbwa kwa ulimwengu mpaka leo, miaka hii yote daima imehusu kujenga kanisa, lakini hakuna mtu anayesikia kamwea kuhusu kujenga ufalme. Japokuwa Nazungumza kuhusu haya kwa kinywa Changu mwenyewe, yupo yeyote anayejua asili yake? Wakati mmoja Nilishuka kwenye ulimwengu wa binadamu Nikapitia na Nikaangalia kwa makini mateso yao lakini bila ya kutimiza lengo la kupata mwili Kwangu. Wakati ujenzi wa ufalme unapoendelea, Mimi Niliyepata mwili huanza rasmi kutekeleza huduma; yaani, Mfalme wa ufalme rasmi Anachukua uwezo wa mamlaka Yake makuu.