Jumanne, 7 Agosti 2018

Mwenyezi Mungu Ndiye Yesu Aliyerudi

Sura ya 1 Lazima Ujue Kwamba Mwenyezi Mungu Ndiye Mungu Mmoja wa Kweli Ambaye Aliumba Mbingu na Dunia na Kila kitu Ndani Yao

2. Mwenyezi Mungu Ndiye Yesu Aliyerudi.

Maneno Husika ya Mungu:
Mungu Amekuwa mwili katika nchi ya China, ambayo wenyeji wa Hong Kong na Taiwan wanaiita bara. Mungu Alipokuja kutoka juu na kuja duniani, hakuna mtu mbinguni wala duniani aliyejua, maana hii ndiyo maana ya kweli ya Mungu kurudi kwa namna ya siri. Amekuwa katika mwili Akifanya kazi na kuishi kwa muda mrefu, bado hakuna mtu yeyote aliyejua. Hata leo hii, hakuna mtu anayetambua. Pengine hiki kitabakia kuwa kitendawili cha milele. Mungu kuja katika mwili wakati huu sio kitu ambacho mtu yeyote anaweza kujua. Haijalishi ni kwa kiwango kikubwa kiasi gani Roho Mtakatifu Anafanya kazi, siku zote Mungu yupo katika hali ya utulivu, kamwe Hajiachilii mbali. Mtu anaweza kusema kwamba inaonekana kama hatua hii ya kazi Yake inafanyika mbinguni. Ingawa ipo wazi kabisa kwa kila mtu, hakuna anayeitambua.

Jumatatu, 6 Agosti 2018

Umeme wa Mashariki | Yule Anayeshikilia Ukuu // Juu ya Kila Kitu


✨Some feelings about God destroying this world by flood in the documentary the One Who Holds Sovereignty Over...
Annie Lee 發佈於 2018年7月18日星期三

Some feelings about God destroying this world by flood in the documentary the One Who Holds Sovereignty Over Everything
Due to God’s sovereignty, various birds and beasts could enter the ark orderly according to God’s instruct. There were big elephants, dainty rabbits, fierce tigers, meek sheep and various insects and so on. They could live in harmony in the ark and no longer slaughtered and fought with each other even they were natural enemies before. At that moment, they could conduct properly and didn’t cross the line. What a big miracle it was! Just as it goes in the hymn, “His deed is everywhere, His power is everywhere, His wisdom is everywhere, and His authority is everywhere.” Let’s see God’s wonderful deeds and realize His sovereignty!

Jumapili, 5 Agosti 2018

Mapenzi ya Mungu ni Kuwaokoa Watu kwa Kiwango Kikubwa Sana Kinachowezekana

Umeme wa Mashariki, Kanisa la Mwenyezi Mungu, Mapenzi ya Mungu,

Sura ya 12. Mapenzi ya Mungu ni Kuwaokoa Watu kwa Kiwango Kikubwa Sana Kinachowezekana

1. Usijishughulishe na Ikiwa Umejaaliwa na Mungu, bali Ujishughulishe na Ufuatiliaji Wako
Mwenyezi Mungu alisema, Watu wengi hawaelewi mapenzi ya Mungu; wanafikiri kuwa kila mtu ambaye ameamuliwa na Mungu ataokolewa bila kuepuka na wanafikiri kuwa kila mtu asiyeamuliwa na Mungu hataokolewa hata wakiyafanya mambo vyema zaidi. Wanafikiri kwamba Mungu hataamua matokeo ya watu kulingana na utendaji na tabia yao. Iwapo unafikiri hivi, basi unamwelewa Mungu visivyo kabisa. Iwapo Mungu angefanya hili kweli, basi Mungu angekuwa mwenye haki? Mungu huamua matokeo ya watu kulingana na kanuni: Mwishowe matokeo ya watu yataamuliwa kulingana na utendaji wao wa kibinafsi na tabia.

Jumamosi, 4 Agosti 2018

Wimbo wa Injili 2018 | "Matendo Ya Mungu Yanajaza Ulimwengu Mzima Tupu" Sifa kwa matendo ya Mungu ya ajabu



💞@@@@🎼@@@@😇@@@@🎶@@@@🎤

🎻~~~~🎵~~~~💞~~~~💞~~~~💓~~~~💕
Kanisa la Mwenyezi Mungu | Nyimbo wa Injili 2018 | "Matendo Ya Mungu Yanajaza Ulimwengu Mzima Tupu" Sifa kwa matendo ya Mungu ya ajabu 🎬😇👍

I
Mungu anatazama chini juu ya vitu vyote kutoka juu,
na Anatawala vitu vyote kutoka juu.
Wakati huo huo, Mungu ametuma wokovu Wake juu ya dunia.
Mungu anaangalia kutoka mahali Pake pa siri kila wakati,
kila hatua ya mwanadamu, kila kitu anachosema na kufanya.

Ijumaa, 3 Agosti 2018

Ufafanuzi wa Tamko la Kumi na Tisa

Kanisa la Mwenyezi Mungu | Ufafanuzi wa Tamko la Kumi na Tisa

Mwenyezi Mungu alisema, Inaonekana kwamba katika mawazo ya watu, Mungu ni wa fahari sana naye Haeleweki. Ni kana kwamba Mungu haishi miongoni mwa wanadamu, kana kwamba anawadharau watu kwa sababu Yeye ni wa fahari sana. Mungu, hata hivyo, Huziseta fikira za wanadamu na kuzifuta zote, Akizika fikira zao zote ndani ya "makaburi" ambamo zinageuka kuwa majivu. Mtazamo wa Mungu kwa fikira za wanadamu ni sawa na mtazamo Wake kwa wafu, Akiwafafanua apendavyo. Ni kana kwamba hakuna athari kutokana na fikira. Kwa hiyo tangu uumbaji wa ulimwnegu mpaka sasa, Mungu amekuwa Akifanya kazi hii na Hajaacha kamwe. Kwa sababu ya mwili, wanadamu hupotoshwa na Shetani, na kwa sababu ya matendo ya Shetani duniani, wanadamu huunda kila aina ya fikira wakati wa uzoefu wao. Huu unaitwa "muundo asilia.

Alhamisi, 2 Agosti 2018

Ni Muhimu Sana Kutii Kazi ya Roho Mtakatifu!

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, Roho Mtakatifu,

Ni Muhimu Sana Kutii Kazi ya Roho Mtakatifu!

Xiaowei    Mji wa Shanghai
Wakati fulani kitambo, hata kama daima nilipata msukumo kiasi na fadhila wakati dada mmoja aliyeshiriki nami alishiriki nuru aliyokuwa amepata wakati alipokula na kunywa neno la Mungu, pia kila wakati nilikuwa na hisia ya muda mrefu kuwa alikuwa anajionyesha. Ningejiuliza, “Nikimjibu sasa hivi, sitakuwa nikimtia moyo? Kwa namna hiyo, sitaonekana basi kuwa duni kumliko yeye?” Matokeo yake yakawa, nilikataa kutaja maoni yangu mwenyewe katika ushirika au kutoa maoni kuhusu mawazo yoyote aliyoshirikisha. Wakati mmoja, dada yangu, alipopata utambuzi fulani kutoka kwa kula na kunywa fungu fulani la neno la Mungu, alihisi kuwa kulikuwa na kasoro fulani na hali yetu na kuniuliza kama ningekuwa radhi kuwasiliana naye kuhusu fungu hilo la neno la Mungu.

Jumatano, 1 Agosti 2018

Umeme wa Mashariki | Tamko la Arubaini na Sita

Umeme wa Mashariki, Kanisa la Mwenyezi Mungu, Mwenyezi Mungu,

Umeme wa Mashariki | Tamko la Arubaini na Sita

Sijui jinsi watu wanavyoendelea katika kuyafanya maneno Yangu kuwa msingi wa kuweko kwao. Nimehisi wasiwasi kila mara kwa ajili ya majaliwa ya mwanadamu, lakini watu hawaonekani kuwa na fahamu yoyote kuhusu hili—na kutokana na hilo, hawajawahi kuyatilia maanani mambo Yangu, na hawajawahi kukuza kuabudu kokote kwa ajili ya mtazamo Wangu kuhusiana na mwanadamu. Ni kana kwamba walitupa hisia zamani ili kuuridhisha moyo Wangu. Nikikumbwa na hali kama hizo, Nakimya mara nyingine. Kwa nini maneno Yangu hayastahili kufikiriwa na watu, kuhusu kuingia zaidi?