Jumanne, 6 Novemba 2018

Umeme wa Mashariki | Tamko la Thelathini na Mbili

Kanisa la Mwenyezi Mungu,Mwenyezi Mungu,Umeme wa Mashariki

Umeme wa MasharikiTamko la Thelathini na Mbili

Mwanga ni nini? Katika siku za nyuma kwa kweli mliuona mbadiliko wa kazi ya Roho Mtakatifu kama mwanga. Kuna mwanga wa kweli wakati wote, unaojumuisha ninyi kupata kile Mungu alicho kupitia kwa kunikaribia na kushirikiana na Mimi; kuwa na utambuzi katika maneno ya Mungu na kufahamu mapenzi ya Mungu katika maneno Yake—yaani, mnapokula na kunywa, mnahisi Roho wa maneno ya Mungu na kupokea maneno ya Mungu ndani yenu; kuelewa kile Alicho huku mkipitia na kupokea mwangaza wa Mungu huku mkizungumza na Yeye; na pia kupewa nuru na kuwa na utambuzi mpya katika maneno ya Mungu wakati wote huku mkifikiria na kutafakari. Ukielewa neno la Mungu na uhisi mwanga mpya, basi hutakuwa na nguvu katika huduma yako? Ninyi hujitia wasiwasi sana katika huduma yenu!

Swahili Christian Video "Macho Kila Mahali" (Mazungumzo Chekeshi) | The Means the CCP Uses to Capture Christians



Mchezo wa kuchekesha Macho Kila Mahali unaeleza jinsi Chama cha Kikomunisti cha China kinavyojaribu kuondoa dini kwa kutumia uchunguzi mkubwa kote nchini, pamoja na kuwageuza watu katika kila tabaka na kazi ya maisha kuwa macho ili kuchunguza, kusimamia, na kupeleleza Wakristo. Kupitia igizo chekeshi dhahiri, jozi hii ya mchezo wa kuigiza inatuonyesha sote mbinu zinazostahili kudharauliwa na makusudi ya kuchukiwa sana ambayo kwayo CCP kinakamata Wakristo, na wakati huohuo inatuonyesha sisi jinsi Wakristo wanavyomtegemea Mungu kukwepa jozi moja ya macho baada ya nyingine, wanavyoeneza injili, na kumshuhudia Mungu.

Soma Zaidi: Chanzo cha Mafanikio ya Umeme wa Mashariki


Jumatatu, 5 Novemba 2018

Tamko la Mia Moja na Kumi na Tatu

Kanisa la Mwenyezi Mungu,Mwenyezi Mungu,Umeme wa Mashariki
Mwenyezi Mungu alisema, Kila kitendo Ninachokifanya kina hekima Yangu ndani yake, lakini mwanadamu hawezi kukielewa kamwe; mwanadamu anaweza tu kuona matendo Yangu na maneno Yangu, lakini hawezi kuuona utukufu Wangu, au kuonekana kwa nafsi Yangu, kwa sababu mwanadamu hasa anakosa uwezo huu. Chini ya hali ya kutombadilisha mwanadamu, wazaliwa Wangu wa kwanza nami tutarejea Sayuni na kubadili sura, ili mwanadamu aweze kuiona hekima Yangu na kudura Yangu. Hekima Yangu na kudura Yangu ambayo mwanadamu anaiona sasa ni sehemu moja ndogo tu ya utukufu Wangu, na haistahili kutajwa kamwe.

Tamko la Mia Moja na Ishirini

Sayuni! Salamu! Sayuni! Ita kwa sauti! Nimerudi kwa ushindi, Nimerudi nikiwa mshindi! Watu wote! Harakisheni mpange foleni kwa utaratibu! Vitu vyote! Mtakuja kusimama kabisa, kwa sababu nafsi Yangu inaukabili ulimwengu mzima na nafsi Yangu inaonekana katika Mashariki ya dunia! Nani anayethubutu kutopiga magoti katika ibada? Nani anayethubutu kutosema kumhusu Mungu wa kweli? Nani anayethubutu kutoangalia juu kwa kumcha? Nani anayethubutu kutotoa sifa? Nani anayethubutu kutangaza kwa shangwe? Watu wangu wataisikia sauti Yangu, Wanangu watasalia ndani ya ufalme Wangu! Milima, mito, na vitu vyote vitashangilia bila kukoma, na kurukaruka bila kupumzika. 

Jumapili, 4 Novemba 2018

Matamshi ya Mungu | "Kiini Cha Kristo Ni Utiifu kwa Mapenzi ya Baba wa Mbinguni"


Mwenyezi Mungu anasema, "Mungu mwenye mwili Anaitwa Kristo, na Kristo ni mwili uliovishwa na Roho wa Mungu. Mwili huu ni tofauti na wa mwanadamu yeyote aliye wa nyama. Tofauti hii ni kwa sababu Kristo sio wa mwili na damu bali ni mwili wa Roho. Anao ubinadamu wa kawaida na uungu kamili. Uungu Wake haujamilikiwa na mwanadamu yeyote. Ubinadamu Wake wa kawaida unaendeleza shughuli Zake zote za kawaida katika mwili, wakati uungu Wake unafanya kazi ya Mungu Mwenyewe. Basi iwe ubinadamu Wake au uungu, yote hujiwasilisha kwa mapenzi ya Baba wa mbinguni. Kiini cha Kristo ni Roho, yaani, uungu. Kwa hivyo, chemichemi Yake ni ile ya Mungu Mwenyewe; Dutu hii haitapinga kazi Yake Mwenyewe, na Yeye hangeweza kufanya kitu chochote kinachoharibu kazi Yake Mwenyewe, wala milele Yeye kutamka maneno yoyote ambayo yanakwenda kinyume na mapenzi Yake Mwenyewe."

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Tamko la Ishirini na Tatu

Matamshi ya Mwenyezi MunguTamko la Ishirini na Tatu

Kwa ndugu wote ambao wameisikia sauti Yangu: Mmeisikia sauti ya hukumu Yangu kali na mmevumilia mateso yaliyokithiri. Hata hivyo, mnapaswa kujua kwamba katika sauti Yangu kali kumejificha nia Zangu! Ninawafundisha nidhamu ili muweze kuokolewa. Mnapaswa kujua kwamba kwa wana Wangu wapendwa, Nitawafundisha nidhamu na kuwapogoa na kuwafanya muwe wakamilifu hivi karibuni. Moyo Wangu una hamu sana, lakini ninyi hamuelewi moyo Wangu na hamtendi kulingana na neno Langu. Maneno Yangu leo yanawajia ninyi na kuwafanya kutambua kweli kwamba Mungu ni Mungu mwenye upendo na nyote mmepitia upendo wa dhati wa Mungu.

Jumamosi, 3 Novemba 2018

Swahili Gospel Movie Segment "Mungu Anashikilia Ukuu Juu Ya Majaliwa ya Kila Nchi na Watu Wote"

Swahili Gospel Movie Segment "Mungu Anashikilia Ukuu Juu Ya Majaliwa ya Kila Nchi na Watu Wote"

Milki ya kale ya Kirumi na Milki ya zamani ya Uingereza zilikuwa na mafanikio na nguvu kwa haraka sana na kisha kufifia kuelekea kudhoofika na uharibifu. Sasa, Marekani limekuwa taifa kubwa lisilobishaniwa la ulimwengu na pia lina jukumu lisilofidika la kudumisha na kuimarisha hali ya ulimwengu. Ni mafumbo ya aina gani hasa yaliyofichika kuhusiana na kuinuka na kuanguka kwa mataifa? Ni nani aliye na mamlaka juu ya majaliwa ya kila nchi na watu wote? Sehemu hii ya ajabu kutoka kwa filamu ya Kikristo, "Yule Anayeshikilia Ukuu Juu ya Kila Kitu", itakufichulia majibu haya.
Sikiliza zaidi: Utongoaji wa Neno la Mungu, nyimbo za dini video