Ijumaa, 10 Novemba 2017

Mwenyezi Mungu Amekuwa Ameketi Kwenye Kiti Kitukufu cha Enzi




Mwenyezi Mungu Amekuwa Ameketi Kwenye Kiti Kitukufu cha Enzi

Mfalme mwenye ushindi amekuwa ameketi kwenye kiti kitukufu cha enzi.

Amekamilisha ukombozi, akiongoza watu Wake wote kuonekana katika utukufu.

Vitu vyote vimo mkononi Mwake. Kwa busara takatifu na nguvu,

Amejenga na kuimarisha Sayuni, kujenga na kuimarisha Sayuni.

Kwa uadhama, Yeye huhukumu ulimwengu huu muovu,

na huhukumu mataifa yote na watu wote, nchi na bahari na viumbe hai ndani yazo,

pamoja na wale ambao wamelewa kwa divai ya uzinifu.

Kwao Mungu atatimiza hukumu Yake.

Mungu atapata hasira nao, kuonyesha uadhama Wake,

na kuwahukumu mara moja, bila taahira yoyote.

Moto wa hasira Yake utazichoma dhambi zao za mauti,

kuzichoma dhambi zao za mauti. Majanga yatawajia wakati wowote,

na wataona vigumu kutoroka na kutafuta usalama; wakilia na kusaga meno yao, huleta maangamizi kwao wenyewe.

Wataona vigumu kutoroka na kutafuta usalama; wakilia na kusaga meno yao, huleta maangamizi kwao wenyewe.

Washindi, wana wapendwa wa Mungu, watabaki Sayuni.

Hawatawahi kutoka hapo, hawatawahi kutoka hapo.

Mungu aliye wa kweli pekee ameonekana (Mungu ameonekana)!

Mwisho wa dunia (mwisho wa dunia) umefichuliwa mbele yetu.

Hukumu katika siku za mwisho imeanza.

Watu wote husikia sauti ya Mungu na kuzingatia matendo Yake.

Sauti ya kusifu haitawahi kukoma kamwe, haitawahi kukoma kamwe.

Watu wote husikia sauti ya Mungu na kuzingatia matendo Yake.

Sauti ya kusifu haitawahi kukoma, haitawahi kukoma.

Sauti ya kusifu haitawahi kukoma, haitawahi kukoma.

kutoka kwa Neno Laonekana katika Mwili
Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki,  Kanisa,
Mwenyezi Mungu Amekuwa Ameketi Kwenye Kiti Kitukufu cha Enzi

   Umeme wa Mashariki, Kanisa la Mwenyezi Mungu lilianzishwa kwa sababu ya kuonekana na kazi ya Mwenyezi Mungu, ujio wa pili wa Bwana Yesu, Kristo wa siku za mwisho. Linashirikisha wale wote ambao wanaikubali kazi ya Mwenyezi Mungu katika siku za mwisho na ambao wameshindwa na kuokolewa kwa maneno Yake. Liliasisiwa kikamilifu na Mwenyezi Mungu mwenyewe na linaongozwa naye kama Mchungaji. Kwa hakika halikuanzishwa na mtu. Kristo ni ukweli, njia, na uzima. Kondoo wa Mungu husikia sauti ya Mungu. Mradi unasoma maneno ya Mwenyezi Mungu, utaona kuwa Mungu ameonekana.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni