Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Amini-kwa-Mungu. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Amini-kwa-Mungu. Onyesha machapisho yote

Jumatatu, 19 Februari 2018

11. Kupitia Utunzaji wa Uangalifu wa Mungu wa Wokovu wa Mwanadamu katika Maafa

11. Kupitia Utunzaji wa Uangalifu wa Mungu wa Wokovu wa Mwanadamu katika Maafa

Muling , Beijing
Agosti 16, Mwaka wa 2012
Mnamo Julai 21, mwaka wa 2012, Beijing ilipata mvua kubwa zaidi katika miaka sitini. Katika mvua hiyo kubwa niliona matendo ya Mungu na kuona jinsi Yeye huwaokoa mwanadamu.
Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, ukombozi,
Kupitia Utunzaji wa Uangalifu wa Mungu wa Wokovu wa Mwanadamu katika Maafa




Siku hiyo adhuhuri, dada zangu watatu na mimi tulikuwa tumekutana. Nje mvua ilikuwa ikiendelea kunyesha. Saa kumi u nusu jioni mume wangu, ambaye hakuwa muumini, alirudi akitwambia kwamba kulikuwa na maji mengi kwa mzunguko kiasi kwamba watu hawakuweza kupitia. Hata hivyo, saa kumi na moja jioni aliondoka kwa haraka sana kwenda kwa zamu yake ya usiku kazini. Wakati huo sikuhisi kitu chochote kisicho cha kawaida, na nilienda kupika chakula cha jioni kama kawaida. Saa moja usiku, mpangaji wetu kwa ghafla alibisha mlango akiniita, na nilipotoka kuangalia, kile nilichoona kilinipa mshtuko mkubwa: