![]() |
| Umeme wa Mashariki | Baada ya Kupoteza Hadhi Yangu … |
Umeme wa Mashariki | Baada ya Kupoteza Hadhi Yangu …
Huimin Mji wa Jiaozuo, Mkoa wa Henan
Kila wakati nilipoona au kusikia kuhusu mtu aliyekuwa amebadilishwa naye kujisikia mwenye huzuni, dhaifu au mnunaji, na kutotaka kufuata tena, basi niliwaangalia kwa dharau. Nilidhani haikuwa kitu zaidi ya watu tofauti waliokuwa na majukumu tofauti ndani ya kanisa, kwamba hakukuwa na tofauti kati ya juu au chini, kwamba sote tulikuwa uumbaji wa Mungu na hakukuwa na sababu ya kuhuzunikia. Kwa hiyo kama nilikuwa nikiwatunza waumini wapya au kuongoza wilaya, sikuwahi kufikiri kuwa nilizingatia sana hadhi yangu, kwamba nilikuwa mtu wa aina hiyo. Singeweza kamwe kufikiri hata katika miaka milioni moja kwamba ningeonyesha tabia ya aibu kama hiyo wakati mimi mwenyewe nilipobadilishwa ...
