Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Inashindwa-kuanguka. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Inashindwa-kuanguka. Onyesha machapisho yote

Jumatano, 31 Januari 2018

Sababu ya Kweli ya Kazi Isiyofaa | Ushuhuda wa Kuipitia Hukumu ya Kristo

Umeme wa Mashariki | Sababu ya Kweli ya Kazi Isiyofaa 

Xinyi Mji wa Xi’an, Mkoa wa Shaanxi

Katika ziara zangu za karibuni kwa makanisa, mara nyingi niliwasikia viongozi na wafanyakazi wakisema kwamba watu wengine, baada ya kuhudhuria ushirika na mimi, waligeuka hasi, wanyonge na walikosa motisha ya kuendelea kutafuta. Wengine walisema ilikuwa vigumu sana kumwamini Mungu na walimwelewa Mungu visivyo. Wengine walisema kwamba hali zao zilikuwa nzuri kabla ya wao kukutana na mimi, lakini punde tu waliponiona, walihisi shinikizo kubwa mno na wasio na raha. ...Niliposikia haya yote, nilihuzunika, na nilihisi kukosewa vibaya—kila wakati nilipokuja kushiriki na wao ningeishi kwa baadhi ya siku, na, ili kutatua shida zao, nilipitia na kudondoa kama mifano vifungu vingi vya neno la Mungu, nikizungumza hadi nilipokauka mdomo, na wakati huo wote nikifikiri kwamba juhudi zangu zilikuwa zimetoa matokeo mazuri. Sikuwahi kufikiri kwamba mambo yangegeuka kuwa hivi. Mbona hili lilifanyika. Niliweka swali hili katika mawazo yangu nilipomwomba Mungu, “Ee Mungu, hakika mimi ni mwenye makosa kwa ajili ya yote ambayo yamefanyika, lakini sijui nilikosea wapi. Naomba mwongozo Wako, ili niweze kutambua zaidi makosa yangu. Niko tayari kusubiri kupokea nuru Yako.”

Jumamosi, 30 Desemba 2017

Umeme wa Mashariki | Roho Ya Majivuno Kabla ya Kuanguka | kutoka kwa Ushuhuda wa Kuipitia Hukumu ya Kristo

Umeme wa Mashariki, Kanisa la Mwenyezi Mungu, ukweli,
Umeme wa Mashariki | Roho Ya Majivuno Kabla ya Kuanguka

Umeme wa Mashariki |  Roho Ya Majivuno Kabla ya Kuanguka

Baixue Mji wa Shenyang
Kwa sababu ya mahitaji ya kazi, nilihamishiwa hadi sehemu nyingine ya kazi. Wakati huo, nilikuwa na shukurani sana kwa Mungu. Nilihisi kwamba nilikuwa ninapungukiwa sana, lakini kwa njia ya ukuzwaji mtakatifu na Mungu, nilipewa nafasi ya kutimiza wajibu wangu katika eneo la kazi la ajabu hivyo. Niliweka nadhiri kwa Mungu moyoni mwangu: Ningefanya lote ninaloweza kumlipa Mungu. Hata hivyo, baada ya kufika, nilitambua utata mwingi katika kazi iliyokuwa ikifanyika.