Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Katika-Mwangaza-Wake. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Katika-Mwangaza-Wake. Onyesha machapisho yote

Jumatano, 13 Desemba 2017

Wanaompenda Mungu Wataishi Milele Katika Mwangaza Wake

Umeme wa Mashariki,  Kanisa la Mwenyezi Mungu,  Kanisa,
Umeme wa Mashariki | Wanaompenda Mungu Wataishi Milele Katika Mwangaza Wake

Wanaompenda Mungu Wataishi Milele Katika Mwangaza Wake

Mwenyezi Mungu alisema,Kiini cha imani ya watu wengi katika Mungu ni imani za kidini: Hawana uwezo wa kumpenda Mungu, na wanaweza kumfuata Mungu tu kama roboti, bila kuweza kumtamani Mungu, ama kumwabudu. Wanamfuata tu kimyakimya. Watu wengi wanamwamini Mungu, lakini wapo wachache sana ambao humpenda Mungu; wanamheshimu tu Mungu kwa sababu wanaogopa majanga, au hata wanamstahi Mungu kwa sababu ni Mwenye nguvu na aliye juu—lakini katika kumheshimu na kuvutiwa kwao hakuna upendo au kutamani kwa kweli. Katika matukio wanayoyapitia wanataka chembe za ukweli, au hata miujiza fulani isiyokuwa na maana.