Swahili Gospel Video "Kanisa la Nafsi Tatu ni Mwavuli Wangu"
Utambulisho
Wakati mmoja, serikali ya Kikomunisti ya Uchina iliwakamata Wakristo wengi wa Kanisa la Mwenyezi Mungu kutoka mahali fulani usiku wa manane. Jambo hili lilisababisha ghasia kubwa mahali hapo. Lilichochea majadiliano miongoni mwa washirika wa Kanisa la Nafsi Tatu. Watu wengine waliamini kwamba Umeme wa Mashariki umepitia ukandamizaji na mateso ya kikatili ya serikali ya kikomunisti ya Uchina. Ni hatari sana kuamini katika Umeme wa Mashariki, na ni salama sana kuamini katika Kanisa la Nafsi Tatu. Hawatapitia taabu na wataweza kuingia katika ufalme wa mbinguni. Watu wengine waliamini kwamba Umeme wa Mashariki ndiyo njia ya kweli hasa, lakini mateso na kukamatwa ambayo wanapitia ni makali mno.