Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Mzizi-wa-kushindwa. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Mzizi-wa-kushindwa. Onyesha machapisho yote

Alhamisi, 1 Februari 2018

Kwa Nini Nimetembea Njia ya Mafarisayo | Ushuhuda wa Kuipitia Hukumu ya Kristo

Umeme wa Mashariki, Kanisa la Mwenyezi Mungu, Biblia,
Kwa Nini Nimetembea Njia ya Mafarisayo

Kwa Nini Nimetembea Njia ya Mafarisayo

Suxing Mkoa wa Shanxi
Mimi ni mtu mwenye kiburi na majivuno, na cheo kimekuwa udhaifu wangu. Kwa miaka mingi, nimefungwa na sifa na cheo na sijaweza kujiweka huru kutoka kwazo. Mara kwa mara nimepandishwa cheo na kubadilishwa na mtu mwingine; nimekuwa na vizuizi vingi katika cheo changu na nimekumbwa na matuta mengi njiani. Baada ya miaka mingi ya kushughulikiwa na kusafishwa, nilihisi kwamba sikuwa nachukulia cheo changu kwa uzito. Sikutaka kuwa kama nilivyokuwa katika nyakati zilizopita nikifikiri kwamba mradi nilikuwa kiongozi ningeweza kukamilishwa na Mungu na kwamba iwapo sikuwa kiongozi, basi sikuwa na matumaini. Nilielewa kwamba pasipo kujali jukumu ambalo nilikuwa natimiza, nilihitaji tu kutafuta ukweli na ningefanywa kamili na Mungu; kufuatilia sifa na cheo ni njia ya yule anayempinga Kristo.