Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Nuhu-safina. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Nuhu-safina. Onyesha machapisho yote

Jumatatu, 25 Juni 2018

Maangamizo ya Mungu ya Dunia kwa Mafuriko

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, wokovu,

Maangamizo ya Mungu ya Dunia kwa Mafuriko

“Mwisho wa kila mwenye mwili umekuja mbele zangu; kwa sababu dunia imejawa na dhuluma kupitia kwao; na, tazama, nitawaharibu pamoja na dunia” (Mwanzo 6:13).

Mungu ananuia kuangamiza ulimwengu kwa gharika, anamwagiza Nuhu kuijenga safina.

(Mwa 6:9-14) Hivi ndivyo vizazi vya Nuhu: Nuhu alikuwa mtu wa haki na mkamilifu katika vizazi vyake, na Nuhu alitembea pamoja na Mungu. Nuhu akazaa wana watatu wa kiume, Shemu, na Hamu, na Yafethi. Dunia pia ilikuwa potovu mbele za Mungu, dunia ilijaa dhuluma.