Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Nyakati-mpya. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Nyakati-mpya. Onyesha machapisho yote

Jumapili, 7 Januari 2018

Je, Wajua? Mungu Amefanya Jambo Kubwa Miongoni Mwa Wanadamu

Kanisa la Mwenyezi Mungu,  Umeme wa Mashariki, Mwenyezi Mungu,
Neno Laonekana katika Mwili

Je, Wajua? Mungu Amefanya Jambo Kubwa Miongoni Mwa Wanadamu

Mwenyezi Mungu alisema,Enzi ya zama ishaenda, na enzi mpya imefika. Mwaka baada ya mwaka na siku baada ya siku, Mungu amefanya kazi nyingi. Alikuja duniani, kisha Akaondoka. Mzunguko kama huu umeendelea kwa vizazi vingi. Siku ya leo, Mungu anaendelea kama mbeleni kufanya kazi Anayopaswa kufanya, kazi ambayo bado Hajaikamilisha, kwani hadi leo, bado Hajaingia mapumzikoni. Kutoka wakati wa uumbaji hadi leo, Mungu amefanya kazi nyingi, lakini ulijua kwamba kazi anayoifanya Mungu leo ni nyingi kuliko awali na kipimo ni kikubwa zaidi? Hii ndiyo maana Nasema Mungu amefanya jambo kubwa miongoni mwa wanadamu. Kazi zote za Mungu ni muhimu sana, iwe kwa mwanadamu ama Mungu, kwani kila kitu cha kazi Yake kina uhusiano na mwanadamu.