Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Wakati-wa-Maafa. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Wakati-wa-Maafa. Onyesha machapisho yote

Jumamosi, 28 Julai 2018

Mungu Aliilinda Familia Yetu Wakati wa Maafa

Umeme wa Mashariki, Kanisa la Mwenyezi Mungu, ushuhuda,

Mungu Aliilinda Familia Yetu Wakati wa Maafa

Wang Lan, Beijing
Agosti 6, Mwaka wa 2012
Mnamo Julai 21, mwaka wa 2012, mafuriko makubwa zaidi tangu miaka sitini yalipitia kijijini mwetu kwa nguvu mno. Maafa yalianguka kutoka mbinguni, maji ya mafuriko yalichanganya matope na mawe na kuharibu kijiji chote. Nyumba nyingi ziliharibiwa na maji na maporomoko ya matope.
Baada ya saa kumi na moja alasiri hiyo, mvua ilikuwa ikinyesha kwa nguvu sana. Kulikuwa na maji ya mafuriko na mawe makubwa yaliyoanguka kutoka juu ya nyumba yetu, na maji ya mafuriko yalikuwa makubwa mbele na nyuma ya nyumba yetu.