Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo utamaduni-wa-kale-na-historia. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo utamaduni-wa-kale-na-historia. Onyesha machapisho yote

Jumapili, 18 Machi 2018

Umeme wa Mashariki | Kazi na Kuingia (7)

Umeme wa Mashariki, kumjua Mungu, Kanisa la Mwenyezi Mungu,

Umeme wa Mashariki | Kazi na Kuingia (7)


Mwenyezi Mungu alisema, Imemchukua mwanadamu mpaka siku hii kutambua kwamba kile mtu anachokosa si tu kuruzukiwa maisha ya kiroho na uzoefu wa kumjua Mungu, lakini, muhimu zaidi, mabadiliko katika tabia yake. Kutokana na ujinga kamili wa mwanadamu wa historia na utamaduni wa kale wa wanadamu, hana ujuzi wa kazi ya Mungu hata kidogo. Mwanadamu hutumaini kuwa ndani kabisa ya moyo, mwanadamu anaweza kumpenda Mungu sana, lakini kwa sababu ya upotovu mkubwa mno wa mwili wa mwanadamu, pamoja na kutojali na upumbavu, mwanadamu ameshushwa kuwa asiye na ufahamu wa Mungu hata kidogo. Mungu Anakuja miongoni mwa wanadamu siku ya leo kwa kusudi la kubadilisha mawazo na roho zao, na taswira ya Mungu katika mioyo yao ambayo wamekuwa nayo kwa maelfu ya miaka.