Jumamosi, 11 Novemba 2017

Umeme wa Mashariki | Kuhusu Biblia (1)

Umeme wa Mashariki, Mwenyezi Mungu,  Kanisa la Mwenyezi Mungu,
Umeme wa Mashariki | Kuhusu Biblia (1)

Umeme wa Mashariki | Kuhusu Biblia (1)


    Mwenyezi Mungu alisema: Biblia inapaswa kuangaliwaje kuhusiana na imani kwa Mungu? Hili ni swali muhimu sana. Kwa nini tunawasiliana swali hili? Kwa sababu wakati ujao utaeneza injili na kupanua kazi ya Enzi ya Ufalme, na haitoshi tu kuweza kuzungumza juu ya kazi ya Mungu leo. Ili kupanua kazi Yake, ni muhimu zaidi kwamba unakuwa na uwezo wa kubadilisha dhana za watu za dini ya kale na njia za kale za imani, na kuwaacha wakiwa wameshawishika kabisa—na kufikia katika hoja hiyo Biblia inahusishwa. Kwa miaka mingi, imani ya watu ya kitamaduni (hiyo ya Ukristo, moja ya dini kuu tatu za dunia) imekuwa ni kusoma Biblia; kujitenga na Biblia sio imani kwa Bwana, kujitenga na Biblia ni madhehebu maovu, na uzushi, na hata pale watu wanaposoma vitabu vingine, msingi wa vitabu hivi ni lazima uwe ni ufafanuzi wa Biblia.

Ijumaa, 10 Novemba 2017

Mwenyezi Mungu Amekuwa Ameketi Kwenye Kiti Kitukufu cha Enzi




Mwenyezi Mungu Amekuwa Ameketi Kwenye Kiti Kitukufu cha Enzi

Mfalme mwenye ushindi amekuwa ameketi kwenye kiti kitukufu cha enzi.

Amekamilisha ukombozi, akiongoza watu Wake wote kuonekana katika utukufu.

Vitu vyote vimo mkononi Mwake. Kwa busara takatifu na nguvu,

Amejenga na kuimarisha Sayuni, kujenga na kuimarisha Sayuni.

Kwa uadhama, Yeye huhukumu ulimwengu huu muovu,

na huhukumu mataifa yote na watu wote, nchi na bahari na viumbe hai ndani yazo,

pamoja na wale ambao wamelewa kwa divai ya uzinifu.

Kwao Mungu atatimiza hukumu Yake.

Umeme wa Mashariki | Mungu Amekuja Mungu Ametawala | " Kwaya ya Injili ya Kichina Onyesho la 18"



Kwaya za Injili :

1. Mungu ndiye Mwanzo na tena Mwisho

2. Mwenyezi Mungu Amekuwa Ameketi Kwenye Kiti Kitukufu cha Enzi

1. Mungu ndiye Mwanzo na tena Mwisho

 

 Umeme wa Mashariki, Kanisa la Mwenyezi Mungu,  Kanisa,
Mungu Amekuja Mungu Ametawala
Mungu ndiye Mwanzo, Mungu ndiye Mwanzo, Mungu ndiye Mwanzo, na tena Mwisho, na tena Mwisho, na tena Mwisho. Mungu ndiye Mpanzi, Mungu ndiye Mpanzi, Mungu ndiye Mpanzi, na Mvunaji (Mvunaji). Mungu ndiye Mwanzo na Mwisho; Mungu ndiye Mpanzi na Mvunaji. Mungu ndiye Mwanzo na Mwisho; Mungu ndiye Mpanzi na Mvunaji. Mungu ndiye Mwanzo na Mwisho; Mungu ndiye Mpanzi na Mvunaji. Mungu Anakuwa mwili hasa kwa ajili ya kuikaribisha enzi mpya, na, kwa hakika, Anapoikaribisha enzi mpya, Atakuwa Ameikamilisha enzi ya kale wakati uo huo. Mungu ndiye Mwanzo (Mungu ndiye Mwanzo) na Mwisho (na Mwisho); ni Yeye Mwenyewe Anayetekeleza kazi Yake na hivyo lazima iwe Yeye Mwenyewe Anayemaliza enzi ya kale. Huo ndio ushahidi kuwa Yeye humshinda Shetani (humshinda Shetani) na huishinda dunia, ushahidi kuwa           Yeye huishinda dunia.Ha! Ha! Ha! Ha! Kila wakati Yeye Mwenyewe Anapofanya kazi miongoni mwa mwanadamu, ni mwanzo wa mapigano mapya. Bila mwanzo wa kazi mpya, kwa kawaida hakungekuwa na kikomo kwa enzi ya kale. Na bila kikomo kwa enzi ya kale ni thibitisho kuwa vita na Shetani, vita na Shetani havijafika mwisho. (Ha!)
     Ni kama tu Mungu Mwenyewe Anakuja miongoni mwa mwanadamu na kutenda kazi mpya ndipo mwanadamu atakapoweza kujitoa kutoka katika miliki ya Shetani, miliki ya Shetani, na kupata maisha mapya, maisha mapya na mwanzo mpya. Vinginevyo, mwanadamu ataishi milele katika enzi ya kale na milele kuishi katika ushawishi wa kale wa Shetani, katika ushawishi wa kale wa Shetani. Ha! Ha! Ha! Ha! Katika kila enzi inayoongozwa na Mungu, sehemu ya mwanadamu huwekwa huru, na hivyo, mwanadamu huendelea na kazi ya Mungu kuelekea enzi mpya. Ushindi wa Mungu ni ushindi kwa wale wote ambao humfuata Yeye. Ushindi wa Mungu in ushindi, ushindi kwa wale wote wanaomfuata Yeye.

Alhamisi, 9 Novemba 2017

Umeme wa Mashariki | Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee X | Mungu ni Chanzo cha Uhai kwa Vitu Vyote (IV)

Umeme wa Mashariki,  Kanisa la Mwenyezi Mungu,  Mwenyezi Mungu,
Mungu ni Chanzo cha Uhai kwa Vitu Vyote (IV)

Umeme wa Mashariki | Mungu Mwenyewe, Yule waKipekeeX | 

Mungu ni Chanzo cha Uhai kwa Vitu Vyote (IV)

    Mwenyezi Mungu alisema: Leo, tunafanya ushirika juu ya mada maalum. Kwa kila mmoja wenu, kuna vitu viwili vikuu tu ambavyo mnapaswa kujua, kuvipitia na kuvielewa—na vitu hivi viwili ni vipi? Cha kwanza ni kuingia binafsi kwa watu katika maisha, na cha pili kinahusu kumjua Mungu. Leo Nawapa uchaguzi: Chagua kimoja. Mngependa kusikia kuhusu mada inayouhusu uzoefu wa maisha ya kibinafsi ya watu, au mngependa kusikia inayohusu kumjua Mungu Mwenyewe? Na kwa nini Ninawapa uchaguzi huu? Kwa sababu leo Ninafikiria kufanya ushirika nanyi juu ya mambo mapya kuhusu kumjua Mungu. Lakini, hata hivyo, kwanza nitawaacha mchague kimoja kati ya vitu viwili ambavyo Nimezungumzia hivi punde.

Jumatano, 8 Novemba 2017

Umeme wa Mashariki | Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee IX | Mungu ni Chanzo cha Uhai kwa Vitu Vyote (III)

Umeme wa Mashariki,  Mwenyezi Mungu, Kanisa la Mwenyezi Mungu,
Umeme wa Mashariki | Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee IX | Mungu ni Chanzo cha Uhai kwa Vitu Vyote (III)

Umeme wa MasharikiMungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee IX

Mungu ni Chanzo cha Uhai kwa Vitu Vyote (III)


Mwenyezi Mungu alisema, Kwa kipindi hiki chote, tumezungumza juu ya mambo mengi yanayohusiana na kumjua Mungu na hivi karibuni tulizungumza kuhusu kitu fulani muhimu sana juu ya mada hii: Mungu ni Chanzo cha Uhai kwa Vitu Vyote. Wakati uliopita tulizungumza juu ya vipengele vichache vya mazingira kwa ajili ya kuendelea kuishi ambayo Mungu aliyatengeneza kwa ajili ya binadamu, vilevile Mungu kuandaa kila aina ya riziki ya lazima kwa ajili ya watu katika maisha yao. Kwa kweli, kile ambacho Mungu anafanya si tu kuandaa mazingira kwa ajili ya kuendelea kuishi kwa watu wala si tu kuandaa riziki yao ya kila siku, bali ni kuandaa vipengele mbalimbali vya kazi kubwa ya ajabu na ya lazima kwa ajili ya kuendelea kuishi kwa watu na kwa ajili ya maisha ya binadamu. Haya yote ni matendo ya Mungu.

Jumanne, 7 Novemba 2017

Umeme wa Mashariki | Mungu ni Chanzo cha Uhai kwa Vitu Vyote (II)

Umeme wa Mashariki | Mungu ni Chanzo cha Uhai kwa Vitu Vyote (II)

Mwenyezi Mungu alisema, Tuendelee na mada ya mawasiliano ya wakati uliopita. Je, mnaweza kukumbuka ni mada gani tuliwasiliana wakati uliopita? (Mungu ni chanzo cha uhai kwa vitu vyote.) Je, “Mungu ni chanzo cha uhai kwa vitu vyote” ni mada mnayohisi ikiwa mbali sana nanyi? Mtu fulani anaweza kuniambia wazo kuu la mada hii tuliyowasiliana wakati uliopita? (Kupitia kwa uumbaji wa Mungu wa vitu vyote, ninaona kwamba Mungu hulea vitu vyote na hulea wanadamu. Katika siku zilizopita, kila mara nilifikiria kwamba Mungu anapompa mwanadamu, Anawapa tu watu Wake waliochaguliwa neno Lake, lakini kamwe sikuona, kupitia kwa sheria za vitu vyote, kwamba Mungu anawalea wanadamu. Ni kupitia tu kwa mawasiliano ya Mungu ya kipengele hiki cha ukweli ndipo ninaona sasa kwamba uhai wa vitu vyote unapewa na Mungu, kwamba Mungu anatengeneza sheria hizi, na kwamba Anavilea vitu vyote.

Umeme wa Mashariki | (I) Mhutasari juu ya Mamlaka ya Mungu, Tabia ya Haki ya Mungu, na Utakatifu wa Mungu


Umeme wa Mashariki | (I) Mhutasari juu ya Mamlaka ya Mungu, Tabia ya Haki ya Mungu, na Utakatifu wa Mungu

Mwenyezi Mungu alisema, Mnapomaliza maombi yenu, je, mioyo yenu inahisi utulivu katika uwepo wa Mungu? (Ndiyo.) Ikiwa moyo wa mtu unaweza kutulizwa, ataweza kusikia na kuelewa neno la Mungu na ataweza kusikia na kuuelewa ukweli. Ikiwa moyo wako hauwezi kutulizwa, ikiwa moyo wako siku zote unayoyoma, au siku zote unafikiria juu ya mambo mengine, utaathiri kuja kwako pamoja kusikia neno la Mungu. Sasa, ni kitu gani cha msingi tunachokijadili wakati huu? Hebu sote turudi nyuma kidogo katika hoja kuu. Kuhusiana na kumjua Mungu Mwenyewe, yule wa kipekee, sehemu ya kwanza tuliyoijadili ni ipi? (Mamlaka ya Mungu.) Ya pili ilikuwa ni ipi? (Tabia ya haki ya Mungu.) Na ya tatu? (Utakatifu wa Mungu.) Tumejadili mara ngapi kuhusu mamlaka ya Mungu? Je, imekuwa na matokeo? (Mara mbili.) Vipi kuhusu tabia ya haki ya Mungu? (Mara moja.)