Jumatatu, 4 Desemba 2017

Umeme wa Mashariki | Njia ya Huduma ya Kidini lazima Ipigwe Marufuku

Kanisa la Mwenyezi Mungu,Umeme wa Mashariki,Kanisa

Umeme wa Mashariki | Sitisha Huduma ya Kidini

Umeme wa Mashariki | Njia ya Huduma ya Kidini lazima Ipigwe Marufuku

Mwenyezi Mungu alisema, Tangu mwanzo wa kazi Yake katika ulimwengu mzima, Mungu ameamulia kabla watu wengi kumhudumia Yeye, wakiwemo watu kutoka kila nyanja ya maisha. Kusudio Lake ni kutimiza mapenzi Yake Mwenyewe na kuhakikisha kwamba kazi Yake hapa ulimwenguni imetimia. Hili ndilo kusudio la Mungu katika kuwachagua watu wa kumhudumia Yeye. Kila mtu anayehudumia Mungu lazima aelewe mapenzi haya ya Mungu.

Jumapili, 3 Desemba 2017

Umeme wa Mashariki | Mazungumzo Mafupi Kuhusu “Ufalme wa Milenia Umefika”

Umeme wa Mashariki,  Kanisa la Mwenyezi Mungu, ufalme,

Umeme wa MasharikiMazungumzo Mafupi Kuhusu "Ufalme wa Milenia Umefika"

Mwenyezi Mungu alisema, Mnayaonaje maono ya Ufalme wa Milenia? Baadhi ya watu hutafakari sana kuuhusu na kusema kuwa Ufalme wa Milenia utadumu duniani kwa miaka elfu moja, hivyo basi ikiwa waumini wazee katika kanisa hawajaoa, je, wanapaswa kuoa? Familia yangu haina pesa, je napaswa nianze kutafuta pesa? … Ufalme wa Milenia ni nini? Je, mnajua? Watu ni nusu vipofu na wanapitia mateso mengi. Kwa hakika, Ufalme wa Milenia bado haujafika rasmi. Katika hatua ya kuwafanya wanadamu wakamilike, Ufalme wa Milenia ni mfano mdogo tu; katika kipindi cha Ufalme wa Milenia uliozungumziwa na Mungu, mwanadamu atakuwa amefanywa mkamilifu.

Mungu Anaongoza Majaliwa ya Wanadamu Wote

Mungu Anaongoza Majaliwa ya Wanadamu Wote


    Mwenyezi Mungu alisema,Kama washiriki wa jamii ya binadamu na Wakristo wamchao Mungu, ni jukumu na wajibu wetu wote kutoa akili na mwili wetu kwa kutimiza agizo la Mungu, kwani uhai wetu wote ulitoka kwa Mungu, na upo kwa sababu ya ukuu wa Mungu. Kama akili zetu na miili yetu si kwa ajili ya agizo la Mungu na si kwa sababu ya haki ya mwanadamu, basi nafsi zetu hazina thamani kwa wale waliokufa kishahidi kwa ajili ya agizo kwa Mungu, na thamani ndogo zaidi kwa Mungu, aliyetupa kila kitu.

Jumamosi, 2 Desemba 2017

Kuonekana kwa Mungu Kumeleta Enzi Mpya

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki,


Kuonekana kwa Mungu Kumeleta Enzi Mpya


    Mpango wa Mungu wa miaka elfu sita ya usimamizi unaisha, na lango la ufalme limefunguliwa kwa wale ambao wanatafuta kuonekana kwa Mungu. Ndugu wapendwa, mnasubiri nini? Mnatafuta nini? Mnasubiri kuonekana kwa Mungu? Mnazitafuta nyayo za Mungu? Kuonekana kwa Mungu kunatamaniwa sana! Ni vigumu, kiasi gani kupata nyayo za Mungu! Katika enzi kama hii, katika dunia kama hii, lazima tufanye nini ili tushuhudie kuonekana kwa Mungu? Sharti tufanye nini ili tufuate nyayo za Mungu? Wale wote wanaosubiri kuonekana kwa Mungu wanakumbana na maswali kama haya.

Umeme wa Mashariki | Dibaji

Umeme wa Mashariki, Kanisa la Mwenyezi Mungu, Mwenyezi Mungu,
 Umeme wa Mashariki | Dibaji

Umeme wa Mashariki | Dibaji

Mwenyezi Mungu alisema,Ingawa watu wengi wanaamini katika Mungu, ni wachache wanaoelewa ni nini maana ya imani katika Mungu, na ni nini wanachopaswa kufanya ili waupendeze moyo wa Mungu. Hii ni kwa sababu, hata ingawa watu wengi wanalifahamu neno “Mungu” na mafungu ya maneno kama “kazi ya Mungu”, hawamjui Mungu, na kwa kiwango cha chini zaidi hawaijui kazi ya Mungu. Si ajabu, basi, wale wote wasiomjua Mungu wamejawa na imani iliyovurugika. Watu hawachukulii imani kwa Mungu kwa makini kwa kuwa kuamini katika Mungu ni jambo geni, jambo lisolo la kawaida sana kwao.

Ijumaa, 1 Desemba 2017

Umeme wa Mashariki | Maisha Mapya Katika Ufalme - "Papa hapa, Hivi Sasa, Tuungane Pamoja" (Video Rasmi ya Muziki)



Umeme wa Mashariki | Maisha Mapya Katika Ufalme - "Papa hapa, Hivi Sasa, Tuungane Pamoja"

Papa hapa, Hivi Sasa, Tuungane Pamoja
Kwa kupendana, sisi ni familia. Ah … ah …
Papa hapa, hivi sasa, tunaungana; kusanyiko la watu wampendao Mungu.
Bila upendeleo, tukishikizwa kwa karibu, furaha na utamu vikijaza nyoyo zetu.
Jana tuliacha majuto na hatia; leo tunaelewana, tunaishi katika upendo wa Mungu.

Umeme wa Mashariki | Mbingu Mpya na Nchi Mpya | Tamthilia ya Jukwaa "Kwaya ya Injili ya Kichina 13"

   
 1. WANADAMU WAMEUPATA TENA UTAKATIFU WAO WALIOKUWA NAO AWALI

La … la … la … la …

    Wakati huu wa shangwe, wakati huu wa nderemo (du ba du ba), haki ya Mungu na utakatifu wa Mungu vimeenda ugenini kote ulimwenguni (ba ba ba …), na binadamu wote wanavisifu bila kikomo. (Du … ba … ba la ba ba) Miji ya mbingu inacheka kwa furaha (du ba du ba), na falme za nchi zinacheza kwa shangwe (Ba ba ba …) Ni nani wakati huu ambaye haonyeshi furaha? Na ni nani wakati huu ambaye halii? (Du … ba … ba la ba ba) Nchi ni miliki ya mbingu, na mbingu imeungana na nchi. Mwanadamu ni ugwe unaounganisha mbingu na nchi, na kwa sababu ya utakatifu wake, kwa sababu ya mwanadamu kufanywa upya, mbingu haijafichwa tena kwa nchi, na nchi haiko kimya tena kwa mbingu.