Ijumaa, 16 Machi 2018

Umeme wa Mashariki | Maono ya Kazi ya Mungu (3)

Umeme wa Mashariki, Kanisa la Mwenyezi Mungu, Jina la Mungu,
Maono ya Kazi ya Mungu (3)

Umeme wa MasharikiMaono ya Kazi ya Mungu (3)

Mwenyezi Mungu alisema, Mara ya kwanza Mungu alipopata mwili ilikuwa kupitia kutungwa mimba kwa Roho Mtakatifu, na ilihusiana na kazi Aliyokusudia kufanya. Jina la Yesu liliashiria mwanzo wa Enzi ya Neema. Wakati Yesu Alianza kufanya huduma Yake, Roho Mtakatifu Alianza kutoa ushuhuda kwa jina la Yesu, na jina la Yehova halikuzungumziwa tena, na badala yake Roho Mtakatifu Alianza kazi mpya hasa kwa jina la Yesu.

Umeme wa Mashariki | Kazi na Kuingia (10)

Umeme wa Mashariki, Kanisa la Mwenyezi Mungu, kumjua Mungu,
Kazi na Kuingia (10)

Kazi na Kuingia (10)


Mwenyezi Mungu alisema, Kwa wanadamu kuendelea mbele kiasi hiki ni hali isiyo na kigezo. Kazi ya Mungu na kuingia kwa mwanadamu vinaendelea bega kwa bega, na hivyo kazi ya Mungu, pia, ni tukio kubwa lisilo na kifani. Kuingia kwa mwanadamu hadi sasa ni ajabu ambayo kamwe haijawahi kufikiriwa na mwanadamu. Kazi ya Mungu imefikia upeo wake—na, kufuatia, "kuingia" kwa mwanadamu[1] pia kumefikia kilele chake. Mungu amejishusha kwa kadiri Anavyoweza, na kamwe Hajawahi kuwalalamikia wanadamu au vitu vyote katika ulimwengu.

Alhamisi, 15 Machi 2018

Maono ya Kazi ya Mungu (2)

Umeme wa Mashariki, Kanisa la Mwenyezi Mungu, wokovu,
Maono ya Kazi ya Mungu (2)

Maono ya Kazi ya Mungu (2)

Mwenyezi Mungu alisema, Enzi ya Neema ilihubiri injili ya toba, na alimradi mwanadamu aliamini, basi angeokolewa. Leo, badala ya wokovu kuna majadiliano tu ya ushindi na ukamilifu. Haisemwi katu kwamba mtu mmoja akiamini, familia yake yote itabarikiwa, au kwamba wokovu ni ya mara moja na kwa wote. Leo, hakuna mtu anayezungumza maneno haya, na vitu kama vile vimepitwa na wakati. Wakati huo kazi ya Yesu ilikuwa ni ukombozi wa wanadamu wote. Dhambi za wote ambao walimwamini zilisamehewa; ilimradi wewe ulimwamini, Angeweza kukukomboa wewe; kama wewe ulimwamini Yeye, wewe hukuwa tena mwenye dhambi, wewe ulikuwa umeondolewa dhambi zako. 

Maono ya Kazi ya Mungu (1)

Umeme wa Mashariki, Kanisa la Mwenyezi Mungu, ukweli,
Maono ya Kazi ya Mungu (1)

Maono ya Kazi ya Mungu (1)

Mwenyezi Mungu alisema, Yohana alimfanyia Yesu kazi kwa miaka saba, na tayari alikuwa ameandaa njia Yesu alipofika. Kabla ya haya, injili ya ufalme wa mbinguni iliyohubiriwa na Yohana ilisikika kotekote katika nchi, hivyo ilienea kutoka upande mmoja hadi upande mwingine wa Uyahudi, na kila mtu alimwita nabii. Wakati huo, Mfalme Herode alitamani kumuua Yohana, lakini hakuthubutu, kwani watu walimheshimu sana Yohana, na Herode aliogopa kwamba kama angemuua Yohana wangemuasi. Kazi iliyofanywa na Yohana ilikita mizizi miongoni mwa watu wa kawaida, na aliwafanya Wayahudi kuwa waumini. Kwa miaka saba alimwandalia Yesu njia, mpaka wakati ambapo Yesu alianza kutekeleza huduma Yake.

Jumatano, 14 Machi 2018

Umeme wa Mashariki | Tamko la Thelathini na Tatu

Mwenyezi Mungu alisema, Katika nyumba Yangu, kulikuwapo wakati mmoja wale waliolisifu jina Langu takatifu, ambao walifanya kazi bila kuchoka ili utukufu Wangu duniani ungejaza anga. Kwa sababu ya hili, Nilifurahi sana, moyo Wangu ulijawa na furaha—lakini nani angeweza kufanya kazi badala Yangu, akiacha usingizi usiku na mchana? Azimio la mwanadamu mbele Yangu hunipa raha, lakini uasi wake huchochea hasira Yangu, na hivyo, kwa sababu mwanadamu hawezi kamwe kuzingatia wajibu wake, huzuni Yangu kwa ajili yake inakua kubwa zaidi. Kwa nini watu daima hawawezi kujitolea Kwangu? Kwa nini daima wao hujaribu kubishana na Mimi? Mimi ni msimamizi mkuu wa kituo cha biashara? Kwa nini Mimi hutimiza kwa moyo kamili kile ambacho watu hudai kutoka Kwangu, lakini Nitakacho kutoka kwa mwanadamu hakitimii?" Inawezekana kuwa mimi Sina maarifa katika njia za biashara, lakini mwanadamu anayo? Kwa nini watu daima hunidanganya kwa mazungumzo ya ushawishi na ya kusifu mno?Kwa nini watu kila mara huja wakibeba "zawadi," wakiomba njia ya kurudi ndani? Je, hili ndilo Nililomfundisha mwanadamu kufanya?

Umeme wa Mashariki | Tamko la Thelathini na Mbili

    Mwenyezi Mungu alisema, Watu wanapokusanyika pamoja na Mimi, moyo Wangu unajawa na furaha. Mara moja, Ninatoa baraka zilizo mkononi Mwangu miongoni mwa binadamu, ili watu waweze kukusanyika kwa mkutano na Mimi, na kutokuwa maadui wanaoniasi lakini marafiki wanaotangamana na Mimi. Hivyo, Mimi pia ni wa dhati kwa mwanadamu. Katika kazi Yangu, mwanadamu anaonekana kama mwanachama wa shirika la ngazi ya juu, hivyo Ninamzingatia zaidi, kwa maana daima amekuwa kusudi la kazi Yangu. Nimeweka imara mahali Pangu katika mioyo ya watu, ili mioyo yao iweze kuniheshimu—ilhali wanabaki wasiojua kabisa kwa nini Ninafanya hili, na hawafanyi lolote ila kusubiri. Ingawa kuna mahali ambapo Nimeweka imara katika mioyo ya watu, hawahitaji kwamba Niishi hapo. Badala yake, wanamsubiri “Mtakatifu” katika mioyo yao kuwasili ghafla. Kwa sababu utambulisho Wangu ni duni sana, Sifikii mahitaji ya watu na hivyo Naondolewa na wao. Kwa sababu wanachotaka ni “Mimi” ambaye ni mwenye majivuno sana—ilhali Ninapokuja, Sikuonekana kwa njia hii kwa mwanadamu, kwa hivyo aliendelea kuangalia mbali, akimsubiri aliye moyoni mwake. Ninapokuja mbele ya watu, wananikataa mbele ya umma.

Jumanne, 13 Machi 2018

Umeme wa Mashariki | Tamko la Thelathini na Tano

Umeme wa Mashariki, Kanisa la Mwenyezi Mungu, neema,

Umeme wa Mashariki | Tamko la Thelathini na Tano


Mwenyezi Mungu alisema, Nimeanza kutenda kazi Yangu kati ya wanadamu, kuwakubalia kuishi mkondo mmoja Nami. Nitakamilisha kazi Yangu nikiwa kati yao, maana wao ni vyombo Ninavyosimamia katika mpango Wangu wote wa usimamizi—na ni mapenzi Langu ili waweze kuwa watawala wa vitu vyote. Hivyo basi Naendelea kutembea kati ya wanadamu.