Jumapili, 22 Julai 2018

Umeme wa Mashariki | Mabadiliko ya Mtu Aliyeanguka(1)

Umeme wa Mashariki, Umeme wa Mashariki, wokovu,

Mabadiliko ya Mtu Aliyeanguka(1)

Tong Xin    Mkoa wa Fujian
Nilizaliwa vijijini. Nilitoka kwa nasaba ya wakulima wanyenyekevu na zaidi ya hayo familia yetu ilikuwa na watu wachache, kwa hiyo mara nyingi tulikuwa tunadhulumiwa. Nilipokuwa na umri wa miaka 13, kulikuwa na mtoto aliyepigwa na mtu fulani kutoka nje ya kijiji chetu. Wanakijiji walimlaumu kwa uongo baba yangu kwa kuchochea hilo na wakasema walitaka kupekua nyumba yetu na kuchukua ngawira mali yetu, kuchukua nguruwe wetu na hata kumpiga baba yangu. Kulikuwa na wakati pia ambapo mwanakijiji mwingine alichukua wavu wetu wa uvuvi na kuuweka kama wake mwenyewe. Wakati baba yangu alipokwenda kuurudisha, mwanamjiji huyo kwa kweli alimgonga baba yangu, akitegemea nguvu na ushawishi wake mwenyewe. Baba yangu alilazimika kujidhalilisha tu kwa kuwa alijua kwamba hakuwa na fedha wala nguvu. Mama yangu akawaambia ndugu zangu wa kiume nami kwamba ni lazima tujipiganie wenyewe katika siku zijazo, na kamwe tusiishi maisha ya ukandamizwaji kama huu. Nikiwa mchanga na mwenye kuchukia udhalimu katika jamii, nilidhamiria kuwa siku zijazo ningejitokeza na kuwa bora kuliko wengine na kupata heshima yao, na kamwe nisikandamizwe. Kwa hiyo nilisoma kwa bidii sana, lakini sikuwa mwerevu kutosha na sikuweza kuingia katika vyuo vikuu vyovyote, kwa hiyo nilichagua kufuatilia ustawisho katika jeshi na kujiunga kwa urahisi kwa njia ya ahali.
Wakati kwanza nilijiunga, nilisombera kuchukua kazi zote ngumu na chafu na kuonyesha uamilifu wangu kuwavutia viongozi wangu na kupandishwa cheo katika siku zijazo. Hata hivyo, bila kujali nilijaribu kwa bidii kiasi gani, sikuweza hata kupata nafasi ya kiongozi wa kikosi. Pia nilitaniwa na kudhulumiwa daima na wanajeshi wenza kwa sababu ya nguo zangu chakavu na iktisadi, jambo ambalo lilizidisha tu hamu yangu ya kujitokeza. Baadaye, kwa kuegemea ushauri kutoka kwa mwanakijiji mwenzangu, nilijifunza kwamba tathmini na kupandishwa cheo katika jeshi havitegemei kazi ngumu, lakini badala yake ni utoaji zawadi. Ingawa niliona kitu cha aina hii kikiwa chukizo, ilinibidi nichukue njia ya pekee ya kupandishwa cheo. Kwa hiyo, nilidhamiria kuchukua akiba yangu yote ili kutoa zawadi kwa viongozi wangu na kufanya miunganisho, kama kila mtu mwingine yeyote karibu nami; baada ya hapo niliweza kujiandikisha katika chuo cha kijeshi. Lakini baada ya kuhitimu, nilipewa kazi kupika katika kantini kwa sababu sikuwa na fedha za kutosha za kutoa zawadi, na baadaye nikawa Afisa Mgavi, lakini kwa jina tu. Baada ya miaka kadhaa ya maisha ya kijeshi, nilielewa kuwa warasimu hawakuwaadhibu watoa zawadi na huwezi kufanikisha chochote bila ya kujipendekeza sana kwao. Ukitaka kuendelea, unapaswa kujaribu kila njia za kutengeneza pesa na kutoa zawadi, vinginevyo huwezi kufanikisha chochote bila kujali uwezo wako ni mkubwa kiasi gani. Ili kufanikisha hamu yangu ya kupata, nilianza kutengeneza pesa na kuchangisha fedha kila mahali: Nilitaja bei ya juu na kutia chumvi kiasi kwa makusudi wakati wa kununua chakula, nikipata pesa kidogo ya ziada ya haramu; kuona Afisa Wagavi wengine wakiuza mchele, niliuza kwa siri lori moja ya mchele kutoka kwa jeshi na kutengeneza yuan elfu kadhaa, na kadhalika. Ingawa nilikuwa nimemwamini Yesu tangu utotoni na nilifahamu wazi kwamba vitu hivi nilivyokuwa nikivifanya vilikuwa ni uhalifu, nilikuwa pia na wasiwasi daima kuhusu kupatikana na kuhukumiwa siku moja, nia ya kupandishwa cheo ilinielekeza kufanya mambo hayo kinyume cha dhamiri yangu. Mara nilipokuwa nimekwisha kuweka akiba pesa kiasi, nilianza kuwapendeza viongozi wangu na kuwapa zawadi zilizowaauni kwa upendeleo wao. Kila wakati kiongozi fulani alipokuja kuniona ningejishughulisha nikienda kunywa pombe naye, kuimba, kuwasiliana na makahaba …. Nilifanya kila kitu kilichowezekana ili kujipendekeza kwake. Nilijaribu kumpendeza kwa njia yoyote iliyowezekana. Wakati wowote viongozi walipohitaji msaada fulani, nilifurahi kuwapa huduma zangu. Yeyote aliyekuwa na uhusiano mzuri na viongozi hao, ningejaribu kuwa karibu naye ili kupata pendekezo zuri. Katika miaka hiyo, nilipanda haraka hadi kwa cheo cha kamanda wa batalioni kwa kukimbilia aina hii ya falsafa ya kidunia. Hatimaye nilijitokeza na niliweza kurudi nyumbani kwa utukufu! Baada ya hapo, kila wakati niliporudi nyumbani, wanakijiji wangenizunguka, wakinipendeza na kunisifu, jambo ambalo liliridhisha majisifu yangu sana. Malengo yangu na tamaa zangu zilikua wakati huo. Kama vile watu wangesema, "Maafisa wengine wana yatetea masilahi yao wenyewe tu, sio umma," "Tumia mamlaka ukiwa nayo, kwa sababu yakishaondoka, huwezi kuyatumia," na "Hakuna kitu kama afisa ambaye hahongeki." Kwa hiyo, nilianza kufurahia marupurupu ya kuwa afisa. Ningepata vitu vya bure popote nilipoenda, na kama mtu angetafuta msaada kutoka kwangu, ningewataka wanipe zawadi na singewasaidia kama zawadi zilikuwa duni. Nilianza kufuatilia chakula na mavazi ya kupendeza, na kuanza kujidai. Nikitegemea ukweli kwamba nilikuwa kama "mtoto wa bidii anayependwa na wote" nikijuana na viongozi muhimu kama kamanda na kamissa wa kisiasa, hata nikawa na kiburi sana hivi kwamba ningewadhulumu watu kwa kuringia uhusiano wangu na wenye nguvu, kuomba zawadi kutoka kwa wasaidizi wangu nikitumia majina ya viongozi hawa. Hivi ndivyo jinsi nilivyopotoka kutoka kuwa kijana sahili Mkristo wa mashambani hadi kuwa mtu mwenye shauku, mwenye udanganyifu wa shetani.
Nikiwa mpotovu na aliyeanguka, hata nilionyesha asili yangu ya kuogofya kwa wengine. Mara nyingi nilishuku bila sababu nzuri kwamba mke wangu mrembo ambaye alifanya kazi kwa kampuni ya kigeni alikuwa na uhusiano wa kando; hili lilisababisha mgogoro zaidi kati yetu na utengano uliokuwa ukizidi. Mnamo mwaka 2006, mambo yalimzidi sana mke wangu na akaanzisha mchakato wa talaka; hili lilikuwa kama fedheha kubwa kwangu, hivyo singelikubali. Usiku wa maname daima ningekuwa nikifikiri kuhusu maisha yangu. Nilifikiri mwenyewe: Nimekuwa nikidhamiria kujitokeza tangu utotoni na mke wangu na mimi sote tumefanikiwa katika kazi zetu. Hali katika nyumba yetu ni nzuri kwa kila njia na watu wengine wanatuonea wivu, hivyo kwa nini ninaishi katika maumivu kama hayo, na kwa nini imefika kiasi kwamba mke wangu anataka kunitaliki? Hata mwana wetu wa kiume anateseka pamoja nasi. Je, maisha yangu yako jinsi ninavyotaka yawe? Ninaishi hasa kwa sababu ya nini? Nilipokuwa tu nikihisi kupotea na kuchanganyikiwa, mke wangu aliukubali wokovu wa Mwenyezi Mungu katika siku za mwisho. Kwa njia ya mikutano ya mara kwa mara na ushirika na ndugu wa kike na wa kiume, akawa mwenye matumaini mema zaidi na zaidi, aliacha kubishana nami, na kamwe hakutaja talaka tena. Badala yake, alijishughulisha na kuihubiri injili na kutimiza wajibu wake. Baadaye, nikielekezwa na mke wangu na mama yangu, pia nilianza kumwamini Mwenyezi Mungu.
kutoka kwa Ushuhuda wa Kuipitia Hukumu ya Kristo
Kujua zaidi: Kuhusu Kanisa la Mwenyezi Mungu

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni