Ijumaa, 28 Septemba 2018

Matamshi na Ushuhuda wa Kristo Mwanzoni | Tamko la Themanini

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, Mwenyezi Mungu

Matamshi na Ushuhuda wa Kristo Mwanzoni | Tamko la Themanini

Kila kitu kinahitaji mawasiliano halisi na Mimi ili kupata nuru na kuangazwa; aidha, ni kwa njia hii tu ndio roho inaweza kuwa na amani. La sivyo, haitakuwa na amani. Sasa ugonjwa mbaya zaidi kati yenu ni kutenganisha ubinadamu Wangu wa kawaida kutoka kwa uungu Wangu kamili; aidha, wengi wenu huweka mkazo kwa ubinadamu Wangu wa kawaida, kama kwamba kamwe hawajui kuwa Mimi nina uungu kamili pia. Hii inanikufuru Mimi! Je, mnajua? Ugonjwa wenu ni mbaya sana kiasi kwamba msipoharakisha kuurekebisha mtauawa kwa mikono Yangu. Mbele zangu mnatenda kwa njia moja (kuonekana kama waungwana wa kweli, wanyenyekevu na wastahimilivu), lakini bila Mimi kufahamu nyinyi hutenda kwa njia tofauti kabisa (waungwana wasio wa kweli, wapotovu na wasio wa kujizuia, mkifanya chochote mnachotaka kufanya, kuunda mifarakano, kuanzisha falme za kujitegemea, kutaka kunisaliti), ninyi ni vipofu! Fungua macho yako ambayo yametiwa mchanga na Shetani! Tazama Mimi ni nani hasa! Huna aibu! Hujui kwamba matendo Yangu ni ya ajabu! Hujui kuhusu uweza Wangu! Je, ni nani ambaye atasemekana kwamba anamtumikia Kristo lakini hajaokolewa? Hujui ni kazi gani unafanya! Kwa kweli wewe huja mbele Zangu kwa kujifanya ukionyesha uzuri wako, mfidhuli sana! Mimi nitakutimua kutoka kwa nyumba Yangu, Situmii mtu wa aina hii kwa sababu sikumwamulia kabla au kumchagua.
Ninafanya kile ninachosema, wale wanaotenda uovu hawapaswi kuogopa. Simkosei mtu yeyote. Daima Mimi hutenda kulingana na mpango Wangu, nikitenda kulingana na haki Yangu. Kwa sababu wale wanaotenda uovu wamekuwa wazao wa Shetani tangu uumbaji, Sikuwachagua, hii ndiyo maana ya "chui hawabadili madoa yao." Katika mambo ambayo wanadamu hawawezi kuelewa, kila kitu kimefanywa wazi na hakuna kitu kilichofichwa Kwangu. Labda wewe unaweza kuficha kitu kutoka kwa macho ya idadi ndogo ya watu, ukipata uaminifu wa watu wachache sana, lakini na Mimi si rahisi sana. Mwishoni huwezi kutoroka hukumu Yangu. Mtazamo wa wanadamu ni mdogo, na hata wale ambao wanaweza kuelewa sehemu ndogo ya hali ya sasa wanahesabiwa kama kuwa na ujuzi fulani. Kwangu kila kitu kinaendelea vizuri, hakuna kitu kinachonizuia hata kidogo, kwa sababu yote yako chini ya udhibiti na utaratibu Wangu. Ni nani angeweza kuthubutu kutojisalimisha chini ya udhibiti Wangu! Nani angeweza kuthubutu kuvuruga usimamizi Wangu! Nani angeweza kuthubutu kuniasi au kunikufuru! Ni nani angeweza kuthubutu kuniambia kitu ambacho si kweli, badala yake aniambie uongo mtupu! Hakuna hata mmoja wao atakayetoroka mikono Yangu yenye ghadhabu. Hata kama wewe sasa umejisalimisha, na uko tayari kuadibiwa, na kuingia shimo lisilo na mwisho, Sitakuachilia kwa urahisi. Lazima nikutoe kutoka shimo lisilo na mwisho ili kwa mara nyingine tena uwe chini ya adhabu Yangu yenye hasira (kuchukia kwa kiwango cha juu sana), ukiona mahali unapotorokea. Kitu ambacho Ninachukia zaidi ni kutenganisha ubinadamu Wangu wa kawaida kutoka kwa uungu Wangu kamili.
Heri wale walio waaminifu Kwangu, yaani, heri wao ambao kweli wananitambua kama Mungu Mwenyewe ambaye huchunguza kwa karibu moyo wa mwanadamu, na hakika Nitazidisha baraka zao, nikiwawezesha kufurahia baraka nzuri katika ufalme Wangu milele. Hii pia ni njia yenye ufanisi zaidi ya kumwaibisha Shetani. Hata hivyo, usiwe na pupa au wasiwasi zaidi, kuna muda uliotengwa Nami kwa kila jambo. Ikiwa muda Wangu nilioamua kabla bado haujafika, hata kama ni sekunde kabla, Sitatenda. Mimi hutenda kwa usahihi na kulingana na mpangilio, si kutenda bila sababu. Kwa wanadamu Mimi sina wasiwasi, Niko thabiti kama Mlima Taishan, lakini hujui kwamba Mimi ni Mwenyezi Mungu Mwenyewe? Usiwe na pupa sana, yote yako mikononi Mwangu. Yote yameandaliwa kitambo, yote yanangoja tu kunitumikia. Dunia yote ya ulimwengu inaonekana kuwa na vurugu kutoka nje, lakini kulingana na mtazamo Wangu ni yenye utaratibu. Kile Nilichokuandalia wewe ni kwa ajili yako tu kufurahia, unatambua hili? Usijiingize katika usimamizi Wangu, Nitawaacha watu wote na mataifa yote kuona uweza Wangu kutoka kwa vitendo Vyangu, walibariki na kulisifu jina Langu takatifu kwa ajili ya matendo Yangu ya ajabu. Kwa sababu Nimesema kuwa hakuna chochote ninachofanya kisicho na msingi, lakini kila kitu kimejazwa na hekima Yangu na nguvu Zangu, kujazwa na haki Yangu na uadhama, na hata pia zaidi ghadhabu Yangu.
Wale ambao mara moja wanazinduka wanaposikia maneno Yangu hakika watapata baraka Zangu, hakika watapata ulinzi Wangu na utunzaji, na hawatapitia mateso ya kuadibiwa, lakini watafurahia furaha ya mbinguni. Je, unajua hili? Mateso ni ya milele, lakini furaha ni ya milele hata zaidi; yote yanapitiwa kuanzia sasa hivi. Iwapo unateseka au kufurahi, kunategemea kama una mwelekeo wa kutubu. Na kuhusu ikiwa wewe ni mmojawapo wa Niliowaamulia kabla na wateule wangu au la, wewe unapaswa kuwa na uhakika juu yake kulingana na kile ambacho nimesema. Unaweza kuwapumbaza watu, lakini huwezi kunipumbaza. Wale ambao nimewaamulia kabla na kuwateua watabarikiwa sana kuanzia sasa; wale ambao Sijawaamulia kabla na kuwateua nitawaadibu vikali kuanzia sasa. Huu utakuwa uthibitisho Wangu kwako. Wale ambao wamebarikiwa sasa bila shaka ni wapendwa Wangu; wale ambao wanaadibiwa, haina haja ya kusema kuwa hawajaamuliwa kabla na kuchaguliwa na Mimi. Unapaswa kuelewa hili! Yaani, kama unayopata sasa ni Mimi kukushughulikia, ikiwa ni maneno Yangu ya hukumu kali, basi wewe unachukiwa na unasinya moyoni Mwangu na wewe utakuwa yule atakayetupwa mbali na Mimi. Ikiwa unapokea faraja Yangu na unapokea utoaji Wangu wa uzima, basi wewe unamilikiwa na Mimi, wewe ni mmoja wa wapendwa Wangu. Wewe huwezi kuamua hii kulingana na sura Yangu ya nje. Usiwaze zaidi juu ya hili!
Maneno Yangu yanasema kwa hali halisi ya kila mtu. Je, ninyi mnaamini kwamba Ninaendeleza tu mada zisizo na mpangilio? Kwamba Ninasema chochote ninachohisi kusema? La hasha! Katika kila neno Langu pamefichwa hekima Yangu. Yachukueni tu maneno Yangu kuwa ukweli. Kwa muda mfupi sana, wageni ambao wanatafuta njia ya kweli wataingia ndani. Wakati huo ninyi mtapigwa na butwaa na kila kitu kitafanyika bila ugumu wowote. Je, hamjui kuwa Mimi ndiye Mwenyezi Mungu? Kwa kusikia maneno Yangu mnayaamini kabisa, sivyo? Mimi sikosei, sembuse kukosea kusema, mnajua hili? Kwa hiyo, nimesisitiza mara kwa mara kwamba Ninawaelekeza haraka ili muwaongoze na kuwachunga, mnajua hili? Kupitia kwenu Nitawafanya wawe wakamilifu. Hata muhimu zaidi, kupitia kwenu nitaonyesha ishara Zangu kubwa na maajabu, yaani, miongoni mwa wale wanaodharauliwa na wanadamu Nimechagua kikundi cha watu kunidhihirisha, kulitukuza jina Langu, kusimamia kila kitu kwa niaba Yangu, kutawala kama wafalme pamoja Nami. Kwa hiyo, kwamba ninawaelekeza sasa ni usimamizi mkubwa zaidi wa ulimwengu; hili ni jambo la kushangaza ambalo wanadamu hawawezi kutekeleza. Kwa kuwafanya kuwa wakamilifu Nitamtupa Shetani ndani ya ziwa la moto na kiberiti na shimo lisilo na mwisho, kumtupa kabisa joka kubwa jekundu hadi kifo chake, asifufuke tena kamwe. Kwa hiyo, wote ambao wanatupwa katika shimo lisilo na mwisho ni wazao wa joka kubwa jekundu. Ninawachukia kwa kiwango kikubwa sana. Haya Nimeyasababisha, kwani hamwezi kuona? Wote wasio na uaminifu, wote wanaotumia uhalifu na udanganyifu wamefichuliwa. Wenye kiburi, majivuno, wanaojidai, wajeuri ni wazao wa malaika mkuu na wao wafanana zaidi na Shetani—wote ni maadui Zangu wa jadi, wapinzani Wangu. Lazima Niwaadhibu mmoja mmoja ili kutuliza chuki ndani ya moyo Wangu. Nitafanya hili moja moja, nikilitatua moja moja.
Sasa, hata hivyo, ziwa la moto na kiberiti na shimo lisilo na mwisho ni nini? Katika mawazo ya wanadamu ziwa la moto na kiberiti ni jambo yakinifu, lakini wanadamu hawajui kuwa haya ni maelezo yenye makosa sana, lakini bado yana nafasi fulani katika akili za wanadamu. Ziwa la moto na kiberiti ni mkono Wangu ukigawa kuadibu kwa wanadamu. Yeyote anayetupwa katika ziwa la moto na kiberiti ameuawa kwa mkono Wangu. Nafsi, roho, na miili ya watu hawa yanateseka milele. Hii ndiyo maana ya kweli ya kile Nilichosema wakati niliposema kuwa yote yamo mikononi Mwangu. Na shimo lisilo na mwisho linamaanisha nini? Katika dhana za mwanadamu unafikiriwa kuwa lindi kuu ambalo halina mwisho na lenye kina kirefu sana. Shimo lisilo na mwisho la kweli ni ushawishi wa Shetani. Mtu akianguka mikononi mwa Shetani, mtu huyu yuko katika shimo lisilo na mwisho; hata akipata mabawa hawezi kuruka nje. Kwa hiyo, inaitwa shimo lisilo na mwisho. Watu hawa wote wataadibiwa milele, Nimepanga iwe hivyo.
kutoka kwa Neno Laonekana katika Mwili

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni