Jumanne, 25 Septemba 2018

ushuhuda wa Umeme wa Mashariki | Kuahidi Maisha Yangu kwa Moyo wa Ibada(II)

Umeme wa Mashariki, Kanisa la Mwenyezi Mungu, maombi

Kuahidi Maisha Yangu kwa Moyo wa Ibada(II)

Zhou Xuan Mkoa wa Shandong
Siku iliyofuata, askari waovu walikuja na kunihoji tena, kwa kweli walishangaa na kusema: "Ni nini kibaya na uso wako?" Nilipotazama katika kioo, sikuweza kujitambua; askari muovu alikuwa ameupiga uso wangu mijeledi kwa kamba siku iliyopita na ulikuwa umevimba sana na kuwa mweusi na bluu na kuwa kama panda. Nilipoona kuwa uso wangu ulikuwa umebadilika kabisa mpaka kutotambulika, nilihisi chuki kali kwa joka kubwa jekundu na nikafanya azimio langu kuwa shahidi. Sikuweza kabisa kuruhusu njama yake ishinde! Miguu yangu ilikuwa imepigwa vibaya sana kiasi kwamba sikuweza kutembea na wakati nilipokwenda msalani, niliweza kuona kwamba miguu yangu yote haikuwa na hali ya kawaida iliyobaki, kila kitu kilikuwa cheusi na bluu. Mmoja wa askari waovu akasema: "Hakuna haja ya wewe kuteswa hivi; ukiongea basi hutahitaji kuteseka; unajifanyia hivi mwenyewe! Lifikirie; kiri na tutakutuma nyumbani kwa mumeo na binti yako." Baada ya kumsikia akisema haya, nilimchukia kabisa. Baadaye, walibadilisha mbinu zao na wakaanza kushika zamu kwa kutoniruhusu nilale mchana kutwa na usiku kucha. Nilipoanza kulala, wangepiga yowe na kupiga kelele kubwa ili kuniamsha; walijaribu kuivunja dhamira yangu kwa kutoniruhusu kulala ili nizungumze kwa usahaulifu, katika hali ya akili isiyobainika. Nilimshukuru Mungu kwa kunilinda. Ingawa wale askari waovu waliniweka kwa muda wa siku nne mchana na usiku, haikujalisha jinsi walivyonihoji, nilimtegemea Mungu kwa ustahimilivu na imani, na sio tu kwamba sikuwa na usahaulifu, lakini nilikuwa macho mno. Askari waovu waliponihoji tena na tena, wakasononeka zaidi na zaidi na wakawa wenye kukata tamaa. Walianza kutekeleza masaili ya shingo upande; walitoa matusi na kulalamika, walikasirikia kwamba nilikuwa nimewasababisha kupoteza hamu yao ya kula, kutopata mapumziko mazuri, na kuteswa na mimi, walihisi kuwa walikuwa na bahati mbaya sana. Hatimaye, yote waliyofanya yalikuwa kuniuliza maswali ya kawaida na hawakuwa tena na utashi wa kunihoji. Katika duru hii ya vita Shetani aliishia kushindwa tena.
Askari waovu hawakuachia hapo, walijaribu kunitongoza. Askari mmoja muovu alikuja na kuweka vidole chini ya kidevu changu, akachukua mkono wangu na kusema jina langu. Kwa sauti ya "upendo" akasema: "Wewe ni mzuri sana; haina thamani kuteseka sana hapa. Matatizo yoyote uliyo nayo, naweza kukusaidia kuyatatua. Imani yako kwa Mungu haijakupatia kitu. Nina nyumba mbili, siku moja, nitakuleta huko ili uwe na burudani; sisi wawili tunaweza kutengeneza ubia. Ukikiri, basi utakuwa huru. Chochote unachotaka, naweza kukusaidia. Sitakutendea bila haki….” Niliposikia uongo wake mbaya, mchafu sana, nilijihisi kuchafuka moyo na kwa nguvu zote nilimkataa. Hakuwa na chaguo jingine bali kuondoka kwa aibu. Hili lilinifanya niwaelewe kabisa hawa watu waliolaaniwa na wasio na aibu wanaodaiwa kuwa "polisi wa watu." Wao huuza roho zao wenyewe ili kupata malengo yao wenyewe; wao hutumia mbinu zilizolaaniwa na za kishenzi bila aibu yoyote; hawana heshima yoyote au uadilifu; kwa kweli wao ni pepo wabaya na wachafu!
Hao askari waovu walikuwa na njama moja ya ujanja baada ya nyingine na waliitumia vibaya watu wa familia yangu kujaribu kunishurutisha, wakisema: "Unamwamini Mungu tu, hufikirii juu ya mume wako, binti, wazazi, na watu wengine wa familia; binti yako atakwenda shuleni siku fulani na kutafuta kazi. Unaamini katika dhehebu bovu na hili litaathiri moja kwa moja matarajio yake ya mustakabali. Je, utaruhusu hili lifanyike kwake? Wewe humfikirii; Je, una moyo mgumu wa kumruhusu ahusike katika hili?" Kufuatia hili, walimleta mume wangu, binti, na shangazi ndani ili kuwaacha wajaribu kunishawishi. Nilipomwona binti yangu ambaye sikuwa nimemwona kwa miaka kadhaa, machozi yangu yalitiririka bila kuzuilika. Wakati huu, niliomba kwa nguvu zangu zote kwa Mungu: "Ee Mungu, nakuomba Uulinde moyo wangu, kwa sababu mwili wangu ni dhaifu mno. Wakati huu, siwezi kukamatwa na hila za Shetani na siwezi kujaribiwa na Shetani kuanguka katika hisia zangu; Siwezi kumsaliti Mungu au kuwasaliti ndugu zangu wa kiume na wa kike; namwomba tu Mungu awe pamoja nami na kunipa imani na nguvu." Shangazi akaniambia: "Fanya haraka na uzungumze, kwa nini wewe ni mjinga hivi? Ina thamani yoyote kupitia hili kwa sababu ya imani yako kwa Mungu? Ni nani atakayekushughulikia iwapo chochote kitatokea? Mama yako na baba yako wanahangaika juu yako, wana wasiwasi kila siku kukuhusu, hawawezi kula au kulala vizuri. Hujakuwa na mawasiliano yoyote kwa miaka mingi. Ni lazima utufikirie na urudi na kuishi maisha na sisi. Usimwamini Mungu. Mungu yuko wapi? Angalia ni shida gani ulizopitia kwa sababu ya imani yako kwa Mungu; kwa nini unajisumbua?" Ingawa nilikuwa dhaifu, nililindwa na Mungu na nilitambua kuwa hili lilikuwa pambano la kiroho na niliweza kugundua hila za Shetani; maneno ya Mungu yalinikumbusha moyoni mwangu kwamba: “… lazima umridhishe Mungu licha ya kutotaka kuacha kitu chochote unachopenda, au kilio cha uchungu” (“Ni Lazima Wale Wanaofaa Kufanywa Wakamilifu Wapitie Usafishaji” katika Neno Laonekana katika Mwili). Wakati huo, nilimwambia: "Shangazi, usijaribu kunishawishi, nimesema kila kitu ninachopaswa kuwaambia. Sijui nini kingine ninachopaswa kuwaambia. Wanaweza kunitendea kwa hali yoyote wanayotaka, ni juu yao. Hupaswi kujali kunihusu. Unapaswa kurudi! "Wakati wale askari waovu walipoona mwelekeo wangu imara, hawakuwa na uchaguzi mwingine bali kuiruhusu familia yangu irudi. Wale askari waovu walikereza meno yao na kusema: "Kwa kweli wewe ni mkatili! Wewe una ubinafsi sana. Kwa hakika huna asili ya binadamu. Mungu wako yuko wapi? Kama Yeye ni mwenyezi sana, basi kwa nini Anaruhusu uteswe hapa? Kwa nini Mungu wako haji na kukuokoa? Kama kwa kweli kuna Mungu, basi kwa nini Yeye haji na kufungua pingu zako na kukuokoa? Mungu yuko wapi? Usidanganywe na uongo huu, usiwe mjinga. Hujachelewa mno kuamka na kuuona ukweli. Usipokiri, basi tutakupeleka gerezani kwa miaka mingi!" Uongo wa askari hawa waovu ulinifanya nifikirie maono ya Bwana Yesu akisulubishwa msalabani. Mungu mwenyewe alikuja na kuwa mwili ili kuwakomboa wanadamu wote; kila kitu Alichokifanya kilikuwa ni kwa manufaa ya mwanadamu; hata hivyo, alidhihakiwa, kukashifiwa, kushtakiwa, kukufuriwa, kutukanwa, na kuuawa na Mafarisayo na wale waliokuwa na mamlaka. Mungu alipitia fedheha mno ili kuwaokoa wanadamu, na hatimaye alitundikwa msalabani kwa ajili ya dhambi za wanadamu. Maumivu yote ambayo Mungu alipitia ni kwa ajili ya wanadamu na leo maumivu ninayoyapitia ni maumivu ninayohitaji kuyapitia. Kwa sababu nina sumu ya joka kubwa jekundu, Mungu anatumia mazingira haya kwa upande mmoja ili kunipima, na kwa upande mwingine ili kuniruhusu kuelewa kwa hakika asili mbaya ya joka kubwa jekundu na, kulidharau na kulisaliti joka kubwa jekundu, na kumfuata Mungu kikamilifu. Kama vile tu neno la Mungu linavyosema: “Mungu anakusudia kutumia sehemu ya kazi ya pepo wachafu ili kuikamilisha sehemu ya mwanadamu, ili watu hawa waweze kufahamu matendo ya mapepo, na kuwawezesha watu wote wawafahamu kwa kweli mababu zao. Ni wakati huo tu ndipo wanadamu wanaweza kujinasua, sio tu kuwatoroka watoto wa mapepo, lakini hata zaidi mababu zao. Hili ndilo kusudi la asili la Mungu kulishinda kabisa joka kubwa jekundu, kufanya hivyo ili wanadamu wote wajue umbo halisi la joka kubwa jekundu, Aambue kinyago chake kabisa, na kuona umbo lake halisi. Hili ndilo Mungu anataka kutimiza, nalo ni lengo Lake la mwisho duniani ambalo Amefanyia kazi nyingi sana; Ananuia kulifanikisha hili ndani ya watu wote. Hili linajulikana kama ushawishi wa vitu vyote kwa ajili ya kusudi la Mungu” (“Ufafanuzi wa Tamko la Arubaini na Moja” katika Neno Laonekana katika Mwili).
Hatimaye, wale askari waovu walinipeleka kwa kituo cha kizuizi na kunizuia kama mhalifu kwa mwezi mmoja. Katika mwezi huu, walinihoji mara moja zaidi. Kwa siku mbili mchana na usiku, hawakuniacha nilale na hawakunipa chakula cha kutosha. Wakati mwingine hawakunipa chakula chochote, lakini bado ilikuwa bure. Joka kubwa jekundu huwatesa na kuwaumiza watu jinsi hii bila kikomo! Wakati kuzuiliwa kwangu kulipofikia kikomo, walinihukumu miaka miwili ya marekebisho kupitia kwa kazi kwa "kuamini katika dhehebu bovu na kuvuruga utaratibu wa jamii" bila ushahidi wowote. Kabla ya kwenda kambi ya kazi, familia yangu ilinitumia yuan 2,000 kwa ajili ya gharama za maisha, lakini zote zilibadhiriwa nao. Pepo hawa walikuwa kweli Shetani na pepo wabaya ambao walikuwa na kiu ya damu na uhai wa binadamu. Ulikuwa ni uovu kabisa! Katika nchi ya joka kubwa jekundu, hakuna sheria; chochote linachopinga, linaweza kuchinja na kunyonya lipendavyo; linaweza kuanzisha mashtaka ya jinai linavyotaka ili kuwadhibiti watu na kuwanasa watu. Joka kubwa jekundu huwasingizia na kuwanasa watu, huwaua watu wasio na hatia, hufanya kitu duni kuwa muhimu, na bila haki huwapachika watu sifa. Wao ni dhehebu halisi na la kweli, wao ni kikundi cha wahalifu wenye utaratibu na majambazi ambao huleta majanga na maafa kwa wanadamu. Kwa miaka miwili katika kambi ya kazi, niliona askari waovu wa serikali ya Kichina kimsingi huwadhulumu vibaya na kuwaamrishaamrisha wafanya kazi kama watumwa. Waliwalazimisha watu kula skonzi zilizookwa kwa mvuke na mchuzi wa mboga kila siku; mchana na usiku, walitulazimisha tufanye kazi ya ziada. Nilichoka kwa namna isiyovumilika kila siku na sikupokea fidia yoyote. Nilipokosa kufanya kazi nzuri, ningepata ukosoaji mkali na adhabu (muda mrefu wa kazi, kunyimwa chakula, kulazimishwa kusimama kimya). Wakati huu, hao askari waovu bado hawangeniruhusu niende, walinihoji wakijaribu kunilazimisha kukiri mazingira ya kanisa. Nililichukia vikali, nikitegemea imani na nguvu kutoka kwa Mungu, nikasema kwa hasira: "Mmenipiga na kuniadhibu; mnataka nini kingine? Nimesema kila kitu ninachopaswa kusema; mnaweza kunihoji kwa miaka kumi, miaka ishirini, na bado sitajua chochote. Mnaweza kusahau kuhusu hilo!" Waliposikia hili, wakasema kwa ghadhabu: "Huwezi kuponyeka, unaweza kusubiri hapa tu!" Hatimaye, hao askari waovu waliondoka kwa aibu na kushindwa.
Baada ya kupitia mateso ya kinyama ya joka kubwa jekundu na matendo ya kikatili pamoja na kuishi bila haki gerezani kwa miaka miwili, niliona kwa dhahiri kwamba tabia ya joka kubwa jekundu ni uongo, uovu, kiburi, na ukali. Ni chini ya mifugo. Wao hufikia kiwango cha kuweka mabango yakisema "uhuru wa kidini," kisha wanakwenda huku na huko wakiwafuatilia na kuwatesa wateule wa Mungu kwa kila njia iwezekanayo. Wao kwa wayowayo huivuruga na kuivunja kazi ya Mungu. Wao ni wauaji ambao huua bila kupepesa jicho, wao ni majambazi ambao hupora kwa kisingizio cha "sadaka, haki, amani, na uadilifu." Mwishowe, barakoa zao zimeambuliwa kabisa kupitia hekima ya kazi ya Mungu, na nyuso zao mbaya za pepo zimefunuliwa katika mwanga ili tuweze kufungua uwanja wetu wa maono na kuamka kutoka kwa ndoto zetu. Kama vile tu neno la Mungu linavyosema: “Kwa maelfu ya miaka hii imekuwa ni nchi ya uchafu, ni chafu sana, shida zimejaa, mizimu wanazunguka kila kona, wakihadaa na kudanganya, wakitoa tuhuma zisizokuwa na msingi,[b] wakiwa katili na waovu, wakikandamiza mji huu ulio mahame na kuuacha ukiwa umetapakaa maiti; harufu ya uozo inaijaza nchi na kuenea hewani, na inalindwa isivyo kawaida[c]. Nani awezaye kuuona ulimwengu kupita anga? Shetani anaufunga mwili wote wa mwanadamu, anafumba macho yake yote, na kufunga kinywa chake kwa nguvu. Mfalme wa mashetani amefanya ghasia kwa maelfu kadhaa ya miaka, hadi leo hii, wakati bado anaangalia kwa karibu mji ulio mahame kana kwamba ulikuwa ‘kasiri la pepo’ lisilopenyeka; kundi hili la walinzi, wakati uo huo, wakiangalia kwa macho yanayong'aa, wakiogopa sana kwamba Mungu atawakamata bila wao kujua na kuwafutilia wote mbali, Akiwaacha wakiwa hawana sehemu ya ‘amani na furaha.’ Inawezekanaje watu wa mji wa mahame kama huu wawe wamewahi kumwona Mungu? Je, wamekwishawahi kufurahia uzuri na upendo wa Mungu? Wanathamini vipi masuala ya ulimwengu wa kibinadamu? Ni nani miongoni mwao anayeweza kuelewa matakwa ya kina ya Mungu? Haishangazi, basi, kwamba Mungu mwenye mwili abaki kuendelea kuwa Amefichwa: Katika jamii ya giza kama hii, ambapo mashetani hawana huruma na ni katili, inawezekanaje mfalme wa mashetani anayeua watu kwa kufumba na kufumbua, avumilie uwepo wa Mungu ambaye ni mwenye upendo, mpole, na mtakatifu? Anawezaje kushangilia na kufurahia ujio wa Mungu? Vikaragosi hawa! Wanalipa upole kwa chuki, wanamtweza Mungu kwa muda mrefu, wanamtukana Mungu, ni washenzi kupita kiasi, hawamjali Mungu hata kidogo, wanapora na kuteka nyara, wamepoteza dhamiri yote, na hawana hata chembe ya wema, na wanawajaribu watu wasiokuwa na hatia kuwa watu wasiokuwa na uwezo wa kuhisi. Wazazi wa kale? Viongozi Wapendwa? Wote wanampinga Mungu! Udukuzi wao umeacha wote walio chini ya mbingu katika hali ya giza na machafuko! Uhuru wa dini? Haki halali na matakwa ya wananchi? Zote hizo ni njama za kufunika dhambi!” (“Kazi na Kuingia (8)” katika Neno Laonekana katika Mwili).
Mwenyezi Mungu milele ni mwenye hekima, mwenye kudura na mshindi wa ajabu, na Shetani, joka kubwa jekundu, milele ni wa kusikitisha, mchafu na mshinde asiyeweza. Bila kujali jinsi alivyo mshenzi na mkosa nidhamu, na bila kujali jinsi hujitahidi na kuasi, daima atakuwa chombo cha Mungu kuwafundishia watu Wake wateule. Aidha, limehukumiwa kubagwa kuzimu na Mungu kama adhabu ya milele. Linajaribu kuvunja dhamira ya watu kupitia mateso yake ya kinyama ili watu waweze kujitenga na Mungu na kumtelekeza Mungu. Lakini limekosea! Mateso yake hutufanya tuone kwa usahihi kiini cha pepo na kutambua upendo na wokovu wa Mwenyezi Mungu. Ni jambo linalotuamsha kabisa kulisaliti kabisa na kuwa na imani na ujasiri kumfuata Mungu kwenye njia sahihi ya uzima. Huyu pepo mwenye hila na mzee hatambui kwamba kweli ni mjinga, mwenye akili dhaifu, na kipofu! Daima nitamtegemea Mungu mwenye busara na mwenyezi. Kuanzia sasa kwendelea, bila kujali ni hatari zipi kemkem na shida zilizo kwa njia iliyo mbele, sitawahi kamwe kupatana au kuishi pamoja na joka kubwa jekundu. Nitamfuata Mungu kwa uthabiti mpaka mwisho na kupitia uhalisi wa vitendo vyangu, nitatangaza hukumu kwa joka kubwa jekundu na kulilaani ili liangamie milele katika kuzimu ambako Mungu ameliandalia.
Tanbihi:
a. Maandishi asilia yanasoma "kutoweza kuwa."
b. "Wakitoa tuhuma zisizokuwa na msingi" inahusu mbinu ambazo shetani hutumia huwadhuru watu.
c. "Inalindwa isivyo kawaida" inaonyesha kuwa mbinu ambazo shetani hutumia huwatesa watu ni mbovu hasa, na kuwadhibiti watu sana kiasi kwamba hawana nafasi ya kusogea.
kutoka kwa Ushuhuda wa Kuipitia Hukumu ya Kristo
Tazama zaidi: ushuhuda wa Kanisa la Mwenyezi Mungu

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni