Jumanne, 25 Septemba 2018

ushuhuda wa Umeme wa Mashariki | Kuahidi Maisha Yangu kwa Moyo wa Ibada(I)

Umeme wa Mashariki, Kanisa la Mwenyezi Mungu, ushuhuda

ahidi Maisha Yangu kwa Moyo wa Ibada(I)

Zhou Xuan Mkoa wa Shandong
Mnamo Aprili 3, mwaka wa 2003, niliambatana na dada mmoja kumtembelea muumini mpya. Muumini huyu mpya alikuwa bado hajawekwa katika ukweli na aliishia kuturipoti. Kwa sababu hiyo, askari wanne waovu wenye nguo za raia walikuja na kwa ugomvi kutuingiza sisi wawili katika gari lao na kutupeleka kwa kituo cha polisi. Njiani, moyo wangu ulikuwa na wasiwasi mno, kwa sababu mwilini mwangu nilikuwa na peja ya mawasiliano, orodha isiyo kamili ya majina ya wanajumuiya wa kanisa letu, na daftari dogo. Niliogopa kwamba wale askari waovu wangeweza kugundua vitu hivi na niliogopa zaidi kwamba ndugu zangu wa kiume na wa kike wangeniita kupitia peja yangu ya mawasiliano, kwa hiyo mimi kwa mfululizo nilimwomba Mungu kwa haraka moyoni mwangu: "Mungu, ninapaswa kufanya nini? Ninakuomba Unipe suluhisho na usiruhusu vitu hivi viingie mikononi mwa askari hawa waovu." Baada ya hili, nilichukua vitu hivi kutoka kwa mkoba wangu na kwa kimya kuviweka kiunoni mwangu na kusema kwamba tumbo langu liliuma na nilihitaji kutumia msala.
Wale askari waovu wakaniapizia wakisema: "Wewe umejaa upuuzi!" Baada ya maombi yangu ya mara kwa mara, walimtaka askari mmoja wa kike anichunge nilipokwenda msalani. Nilipouondoa mshipi wangu, kifaa changu cha mawasiliano kilianguka na kwa urahisi nikakiokota na kukitupa katika bomba la maji taka. Kwa sababu niliogopa wakati huo kwamba huyo afisa wa kike angegundua mkoba kiunoni mwangu, sikuutupa katika bomba, lakini badala yake niliutia katika pipa la taka; nilidhani kwamba ningetumia msala tena usiku na kisha kuutupa ndani ya choo. Ilivyotukia, sikurudi kwa msala huo kamwe. Ilitukia kuwa wale askari waovu waliupata ule mkoba niliokuwa nimeutupa katika jaa la taka. Wale askari waovu wakatufungia yule dada na mimi katika chumba kimoja na kutulazimisha tuvue nguo zetu zote ili waweze kutupekua. Walipekua hata kwa nywele zetu kuona kama tulificha chochote. Baada ya kumaliza kutafuta, walitutia pingu na kutufungia katika kile chumba. Ilipofika usiku, wale askari waovu walitutenganisha ili tuhojiwe kwa makini; waliniuliza: "Unatoka wapi? Jina lako ni nani? Ulikuja hapa lini? Unafanya nini hapa? Unaishi wapi? Unaamini nini? Jina la mtu uliye naye ni nani?" Kwa sababu hawakuridhishwa na majibu yangu, wale askari waovu walisema hivi kwa hasira: "Sisi huonyesha upole kwa wale wanaokiri na ukali kwa wale wanaobisha. Usiposema ukweli, utajilaumu mwenyewe! Sema! Ni nani anayekusimamia? Unafanya nini? Sema na tutakutendea kwa upole." Wakati huo nilifikiria: Sijavunja sheria yoyote au kufanya uhalifu wowote, askari polisi hawawezi kunifanyia chochote. Kwa hiyo, bila kujali jinsi walivyojaribu kulazimisha kukiri kwangu, sikuwajibu, kwa sababu nilikuwa nimekata kauli: kabisa sitakuwa Yuda, sitawasaliti ndugu zangu wa kiume na wa kike na sitazisaliti nia za familia ya Mungu. Walipoona kwamba hawakuweza kupata chochote kutoka kwangu, waliingiwa na wasiwasi na kuanza kunigonga na kunipiga mateke kwa ukali wakisema: "Kwa kuwa husemi chochote, tutakuadhibu kwa kukunyosha mikono na miguu!" Kisha ghafla kulikuwa na mlipuko mwingine wa kupigwa ngumi na mateke kwa ukali sana. Baadaye, mmoja wao akaniamuru niketi chini, na akanitia pingu na kuipinda mikono yangu kwelekea nyuma yangu kwa kukaza alivyoweza. Kisha akaweka kiti nyuma yangu na kutumia kamba kuifunga mikono yangu nyuma ya kiti. Alitumia mikono yake na akawekea nguvu zake zote kwelekea chini, akiweka shinikizo juu ya mikono yangu. Mara moja, mikono yangu ikahisi kama ingevunjika; iliumia vibaya sana hivi kwamba nilitoa yowe kali. Walikwenda mbele na nyuma jinsi hii kwa mikono yangu wakiniumiza bila kukoma kwa muda wa saa kadhaa. Baadaye, sikuweza kuvumilia na nilitikisika kutoka utosini hadi kidoleni. Walipoona hayo, wakasema: "Usijifanye kana kwamba wewe ni wazimu, tumeona hili mara nyingi kabla. Je, unadhani unamshtua nani? Je, unadhani kuwa kufanya hivi kutakuondoa kwa tatizo hili?" Waliona kwamba bado nilikuwa nikitikisika na askari mmoja mwovu akasema: "Nenda naye msalani na kumtia kinyesi kiasi kinywani mwake, angalia kama atakila au la." Walitumia kijiti kuchotea kinyesi kiasi na kukifikicha ndani ya kinywa changu na kunifanya nikile; nilikuwa bado nikitoa pofu kwa kinywa na waliona kwamba bado nilikuwa nikitikisika, kwa hiyo waliniacha nishuke kutoka kwa kiti. Mwili wangu mzima uliumia bila kuvumilika kama kwamba nilikuwa na mito kutoka utosini hadi kidoleni na nilitoa yowe kwa maumivu nilipolala sakafuni nikiwa nimeduwaa. Baada ya muda mrefu, viganja vyangu na mikono viliaanza kusogea tena. Hawa mapepo waliogopa kwamba ningepigisha kichwa changu kwa ukuta na kujiua, kwa hiyo walinipa helmeti. Baadaye, waliniburuta na kunirudisha kwa kile chumba kidogo cha chuma. Nililia na kumwomba Mungu: "Ewe Mungu, mwili wangu ni dhaifu sana. Natamani kuwa Unilinde. Bila kujali jinsi Shetani anavyonitesa, ningependelea kufa kuliko kukusaliti Wewe kama Yuda. Sitawasaliti ndugu zangu wa kiume na wa kike au maslahi ya familia ya Mungu. Niko tayari kuwa shahidi Kwako ili kumuaibisha yule Shetani mzee."
Siku ya tatu, wale askari waovu walichukua ile daftari dogo na orodha ya majina ya wanajumuiya wa kanisa niliyokuwa nimeitupa katika jaa la taka na kunihoji. Nilipoona vitu hivi, nilihisi hasa kutokuwa na raha na kujaa kujilaumu na majuto. Nilichukia kwamba nilikuwa na hofu sana na mwoga na kwamba sikuwa na ujasiri wa kutosha wakati huo wa kutupa mkoba ndani ya bomba la maji taka, jambo lililosababisha matokeo haya ya hatari. Nilichukia hata zaidi kwamba sikusikiliza mipango ya familia ya Mungu na kuleta vitu hivi wakati wa kutimiza wajibu wangu, jambo ambalo limelisababishia kanisa hasara kubwa. Nilijua kwa kina kwamba nilistahili mateso niliyokuwa nikiyapitia siku hii na kwamba ilikuwa ni kuadibu kwa Mungu na hukumu vikinijia, na nilikuwa radhi kuvikubali. Nilikuwa radhi pia kumtegemea Mungu ili kumshinda Shetani. Wakati huu nilifikiri juu ya wimbo wa uzoefu: "Sijali kuhusu njia iliyo mbele; ni kutenda tu mapenzi ya Mungu kama wito wangu. Wala sijali juu ya mustakabali wangu. Kwa kuwa nimechagua kumpenda Mungu, nitakuwa mwaminifu mpaka mwisho. Bila kujali jinsi hatari na shida zilivyo kubwa, au jinsi njia iliyo mbele ilivyo na mashimoshimo na ya kuparuza, kwa kuwa ninalenga siku ambayo Mungu atapata utukufu, nitatelekeza kila kitu na kujitahidi kwenda mbele" ("Kutembea Kama Askari kwa Njia ya Kumpenda Mungu" katika Mfuateni Mwanakondoo na Kuimba Nyimbo Mpya). Niliuimba wimbo huu kimya kimya na moyo wangu ulikuwa na imani na nguvu tena. Wale askari waovu wakaniuliza: "Je, vitu hivi ni vyako? Sema ukweli nasi, hatutakutendea bila haki. Wewe ni mwathirika na umedanganywa. Dini yenu ni dhehebu bovu; Mungu mnayemwamini ni Mungu asiye dhahiri na yu mbali, ni ndoto za mchana. Chama cha Kikomunisti ni kizuri, na unapaswa kutegemea hicho chama na serikali. Ukiwa na shida yoyote, unaweza kuja kwetu na tutakusaidia kuitatua. Ukihitaji usaidizi kupata kazi, tunaweza kukusaidia pia. Kiri tu kila kitu juu ya kanisa lako; tuambie kile watu hawa walio kwa orodha yako wanachofanya. Wanaishi wapi? Ni nani mkuu wenu?" Nilitambua hila zao za uwongo na kusema: "Vitu hivi si vyangu, sijui." Walipoona kwamba singefichua chochote, basi ilifichuka ni watu wa aina gani kamili na walinipiga kikatili na kuniangusha chini na kuendelea kunipiga kwa ukali sana na kutumia nguvu zao zote kuniburuta huku na huko wakitumia pingu zangu. Jinsi walivyozidi kuniburuta, ndivyo pingu zilivyozidi kujikaza na kuukata mwili wangu. Niliumia vibaya sana kiasi cha kulia kwa sauti kubwa na wale askari waovu wakasema kwa ukali: "Tutakufanya uonge, tutakuminya kidogo kidogo kama dawa ya meno ili kukufanya uzungumze!" Hatimaye, walichukua mikono yangu miwili na kuifunga ikielekea nyuma kwa kiti na kunifanya nikalie sakafu. Walinigonga na kuwekea nguvu zao na kugandamiza kwelekea chini juu ya mikono yangu; nilihisi maumivu yasiyovumilika na uchungu uliochoma kana kwamba mikono yangu ingevunjika. Wale askari waovu walinitesa na kunikemea: "Sema wazi!" Bila kusita nikasema: "Sijui!" "Usiposema wazi tutakuua; usiposema wazi basi usitarajie kuishi; tutakufunga jela kwa miaka kumi, miaka ishirini, maisha yako yote; usitarajie kutoka jela kamwe!" Niliposikia hivi, wazo fulani likanijia akilini mwangu ghafla: ni lazima niamue kuwa tayari kwenda jela maisha. Baadaye nilifikiri juu ya wimbo wa uzoefu: "Toa sadaka ya kupendeza mno kwa Mungu, nijidunduizie ile chungu zaidi. Simama na kwa uthabiti ushuhudie kwa Mungu, usikubali kushindwa na Shetani. Aa! Huenda vichwa vikavunjika na damu kuvuja, lakini hadhi ya watu wa Mungu haiwezi kupotea. Imani ya Mungu hupumzika kwa moyo, ni lazima niamue kumdhalilisha Shetani mzee" ("Ninataka Kuona Siku Ambapo Mungu Atapata Utukufu" katika Mfuateni Mwanakondoo na Kuimba Nyimbo Mpya). Mungu alinipa nuru, akinifanya niwe imara na kuwa na ujasiri na akinipa imani na uamuzi kupitia kila kitu na kuwa shahidi kwa Mungu. Kwa sababu hiyo, hila za hao askari waovu hazikushinda; walinitesa mpaka wakachoka, kisha wakanirudisha kwa chumba cha chuma.
Siku chache baadaye, niliteswa na hao askari waovu mpaka nikawa sina nguvu. Nilikuwa katika mpagao wa usahaulifu kabisa na mikono yangu ilikuwa na ganzi. Katika kukabiliana na mateso haya katili na ya kinyama, niliogopa hasa kwamba hao askari waovu wangerudi na kunihoji. Mara tu nilivyofikiria hili, moyo wangu haukuweza kujizuia kutetemeka kwa hofu. Kwa kweli sikujua ni nini kingine wangetumia kunitesa, na sikujua ni lini masaili haya yangeisha. Niliweza tu kuendelea kuomba ndani ya moyo wangu kwa Mungu na kumwomba Mungu kuulinda moyo wangu na kunipa hiari na nguvu za kuvumilia mateso ili ningeweza kuwa shahidi kwa Mungu na kumfanya Shetani ashindwe kwa fedheha kamili.
Wakati wale askari waovu walipoona kuwa singekiri, waliungana na Brigedi ya Usalama wa Taifa na Shirika la Usalama wa Umma ili kunihoji. Kulikuwa na watu zaidi ya ishirini huko wakishika zamu kunihoji mchana na usiku wakijaribu kunilazimisha kukiri. Siku hiyo, askari wawili waovu kutoka kwa Brigedi ya Usalama wa Taifa ambao tayari walikuwa wamenihoji mara moja kabla walinijia na mwanzoni walizungumza kwa huruma wakisema: "Ukikiri ukweli, basi tutakuacha uende na tutahakikisha usalama wako. … Ni chama cha Kikomunisti tu kinachoweza kukuokoa, na Mungu hawezi kukuokoa ….” Wakati mmoja wao alipoona kwamba singetamka neno, aliingiwa na wasiwasi na kuanza kunipigia yowe kwa maneno machafu, akinilazimisha niketi sakafuni. Alinipiga teke kwa miguuni kwa nguvu alivyoweza akitumia viatu vya ngozi akisababisha maumivu yasiyoweza kustahimilika. Askari mwingine muovu akamwuliza: "Kunaendaje, anazungumza?" Alisema: "Yeye ni mkaidi sana, bila kujali unampiga kiasi gani na hatazungumza." Huyo mtu akasema kwa ukali: "Kama hazungumzi, basi mpige hadi afe!" Yule askari muovu akanitishia akisema: "Hutazungumza? Basi tutakuua!" Nikasema: "Nimesema kila kitu ambacho nilihitaji kusema, sijui!" Alikasirika sana kiasi kwamba alionekana kuwa wazimu kabisa, kisha akanguruma kama mnyama wa mwitu na kuanza kunichapa na kunipiga mateke. Hatimaye alipata uchovu kwa kunipiga na kupata kamba kiasi cha unene wa kidole na kuiviringishia mkononi mwake mara chache. Kwa ukatili aliupiga uso wangu mijeledi tena na tena akisema: "Je, wewe humwamini Mungu? Wewe unateseka, kwa nini Mungu wako haji na kukuokoa? Kwa nini Yeye haji na kukufungua pingu? Mungu wako yuko wapi?" Niliyakereza meno yangu na kuvumilia maumivu. Niliomba kwa utulivu moyoni mwangu kwa Mungu: "Ee Mungu, ninapitia shida hii kwa sababu ya uasi wangu; ni kile ninachostahili. Mungu, ulisulubiwa ili kutuokoa; hata kama wakinipiga hadi kufa leo, kamwe sitakuwa kama Yuda. Nataka Uwe pamoja nami na kuulinda moyo wangu. Niko tayari kutoa maisha yangu ili kuwa shahidi Kwako na kumfedhehesha Shetani mzee." Nilifikiria wimbo wa uzoefu: "Hakuna huruma katika kifo, na hakuna mshangao kwa hilo. Mapenzi ya Mungu huzidi yote. … Mungu aliniokoa na ameniwasilisha kwa Shetani, haya ndiyo mapenzi mazuri ya Mungu; moyo wangu utampenda Mungu wangu milele" ("Rudisha Upendo kwa Mungu" katika Mfuateni Mwanakondoo na Kuimba Nyimbo Mpya). Nilifunga macho yangu na kuvumilia mateso ya Shetani na kupigwa. Wakati huo, ilikuwa ni kama nilisahau kuhusu maumivu yangu. Sikujua ni wakati upi adhabu hiyo ingeisha. Sikuthubutu kulifikiria, na sikuweza hata kutafakari juu ya hilo. Kitu pekee ambacho niliweza kufanya ni kusali bila kukoma na kumlilia Mungu. Maneno ya Mungu pia yalinipa imani ya mfululizo: “Msiogope, Mwenyezi Mungu wa majeshi hakika atakuwa pamoja nawe; Yeye anawasaidia na Yeye ni ngao yenu” (“Tamko la Ishirini na Sita” katika Neno Laonekana katika Mwili). “Msiwe na hofu ya wao wanaoua mwili, lakini hawana uwezo wa kuifisha roho: ila heri uwe na hofu ya yeye anayeweza kuiangamiza roho pamoja na mwili katika kuzimu” (Mathayo 10:28). Nilifikiri kuhusu jinsi joka kubwa jekundu lilikuwa tishio la bure tu lililoandikiwa kushindwa na mikono ya Mungu. Pia liko chini ya miguu ya Mungu. Kama Mungu hakuyaruhusu, mauti hayangenijia; bila ruhusa ya Mungu, hakuna hata unywele wangu mmoja ungepotea. Na kama ninashiriki machungu na Mungu leo, basi ni lazima nishiriki matamu na Mungu. Pia nilifikiria "Wimbo wa Washindani": "Je, umewahi kukubali baraka ambazo ulipewa? Je, umewahi kutafuta ahadi za Mungu ambazo ulipewa? Kwa kweli, kwa sababu ya uongozi wa mwanga Wake, utaweza kuvunja mshiko wa nguvu za giza. Kwa kweli, katikati ya giza, hutapoteza mwangaza unaokuongoza. Kwa kweli utakuwa bwana wa uumbaji wote. Kwa kweli utakuwa mshindi mbele ya Shetani. Kwa kweli utasimama katikati wa umati mkubwa sana ili kutoa ushuhuda kwa ushindi Wake katika kuanguka kwa joka kuu jekundu. Kwa kweli utakuwa na nguvu na imara katika nchi ya dhambi. Utaridhi baraka itokayo kwa Mungu kwa mateso unayovumilia, na kwa kweli utawaangazia wote ulimwenguni mzima kwa utukufu Wake." Nguvu ya neno la Mungu haina mipaka na imesababisha imani yangu kuongezeka; nilikuwa na azimio la kupambana na Shetani hadi mwisho. Yule askari muovu alipochoka kunipiga, aliniuliza tena: "Je, utasema?" Nilisema kikiki: "Hata ukinipiga hadi nife, bado sitajua!" Yule askari muovu aliposikia hayo, hakuweza kufanya chochote. Akatupa kamba na kusema: "Wewe ni mkaidi kweli, kama nyumbu. Kwa kweli wewe ni mzuri, huwezi kusema chochote hata ukifa. Ulipata kutoka wapi nguvu na imani nyingi jinsi hii? Wewe kwa kweli ni Liu Hulan zaidi ya Liu Hulan, wewe ni CCP zaidi ya CCP!" Nilipomsikia akisema haya, ilikuwa ni kama nilimwona Mungu ameketi kwenye kiti Chake cha enzi kwa ushindi, akimwangalia Shetani akifedheheshwa. Nililia nusu na kumtukuza Mungu nusu: Ee Mungu, kwa kuitegemea nguvu Yako, ninaweza kumshinda Shetani, yule pepo! Kwa sababu ya ukweli huo, naona kwamba Wewe ni mwenye kudura na Shetani hana nguvu; Shetani daima atashindwa chini ya udhibiti Wako. Usipomruhusu, Shetani hataweza kunitesa hadi nife. Wakati huu, maneno ya Mungu yalinipa nuru tena: “Tabia ya Mungu ni ile ambayo inamilikiwa na Mtawala wa wale walio hai miongoni mwa vitu vyote, kwa Bwana wa viumbe vyote…. Tabia yake ni ishara ya mamlaka … ni ishara ya namna ambavyo Mungu hawezi[a] kukandamizwa au kushambuliwa na giza na kikosi chochote cha adui …” (“Ni Muhimu Sana Kuelewa Tabia ya Mungu” katika Neno Laonekana katika Mwili). Baada ya kupitia mateso katili ya joka kubwa jekundu, kwa kweli niliona upendo wa Mungu na wokovu kwangu na nilipitia nguvu na mamlaka ya neno la Mungu. Bila neno la Mungu kuniongoza kila hatua ya njia na kwa kutegemea tu nguvu yangu mwenyewe, haingewezekana kwangu kuyashinda mateso na kupigwa kwa joka kubwa jekundu. Vivyo hivyo, lilinifanya nione taswira yenyekuweza kudhuruiwa na iliyopondwapondwa ya joka kubwa jekundu. Nilikielewa kiini cha pepo cha unyama walo na kutojali kwalo kwa uhai na nililichukia na kulilaani ndani ya moyo wangu. Nilipenda kuvunja kabisa uhusiano wote nalo na kumfuata Kristo na kumtumikia Kristo milele.
kutoka kwa Ushuhuda wa Kuipitia Hukumu ya Kristo
Tazama zaidi: ushuhuda wa Umeme wa Mashariki

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni