Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Ivunje-Laana. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Ivunje-Laana. Onyesha machapisho yote

Ijumaa, 23 Februari 2018

Swahili Gospel Movie "Ivunje Laana" | Mungu ni Wokovu Wangu


Swahili Gospel Movie "Ivunje Laana" | Mungu ni Wokovu Wangu


Utambulisho

    Fu Jinhua alikuwa mzee wa kanisa la nyumba nchini China. Kama Wakristo wengine wengi, alijitolea kwa Bwana kwa shauku kubwa, na alifanya kazi kwa bidii katika kazi yake kwa ajili Yake. Alikuwa hasa mwenye kujiamini, na alijiona kuwa mtu ambaye alimpenda Bwana kweli. Baada ya kumfuata Bwana kwa miaka mingi, aliamini kwa moyo wote kwamba Biblia ilikuwa imefunuliwa na Mungu, na kwamba maneno katika Biblia yote yalikuwa maneno ya Mungu. Kwa hivyo, akilini mwake, alilinganisha kuamini katika Bwana na kuamini katika Biblia. Alidhani kwamba wale walioachana na Biblia hawakuweza kuitwa wafuasi wa Bwana. Pia aliamini kwamba alihitaji tu kufuata Biblia ili kuchukuliwa kuenda katika ufalme wa mbinguni Bwana atakaposhuka na mawingu.