Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Jaribio. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Jaribio. Onyesha machapisho yote

Jumamosi, 20 Januari 2018

Kazi ya Mungu, Tabia ya Mungu, na Mungu Mwenyewe II | Ibrahimu

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, neema,
Mungu alibariki Ibrahimu Sara akicheka

Kazi ya Mungu, Tabia ya Mungu, na Mungu Mwenyewe II | Ibrahimu

Mwenyezi Mungu alisema, Kwenye mkutano wetu wa mwisho tuliweza kuzungumzia mada muhimu sana. Je, wakumbuka mada hiyo ilikuwa kuhusu nini? Hebu Niirudie. Mada ya ushirika wetu wa mwisho ilikuwa: Kazi ya Mungu, Tabia ya Mungu, na Mungu Mwenyewe. Je, mada hii ni muhimu kwako? Ni sehemu gani katika mada hii ni muhimu kwako? Kazi ya Mungu, tabia ya Mungu, au Mungu Mwenyewe? Ni sehemu ipi inakuvutia zaidi? Ni sehemu ipi unayotaka kusikiliza kuhusu zaidi? Najua ni vigumu kwako wewe kulijibu swali hilo, kwa sababu tabia ya Mungu inaweza kuonekana katika kila kipengele cha kazi Yake, na tabia Yake inafichuliwa katika kazi Yake siku zote na pahali pote, na, kutokana na hayo, inawakilisha Mungu Mwenyewe; kwenye mpango wa usimamizi wa ujumla wa Mungu, kazi ya Mungu, tabia ya Mungu, na Mungu Mwenyewe vyote hivi haviwezi kutenganishwa.