Na Wang Li, Mkoa wa Zhejiang
Nilimwamini Bwana Yesu pamoja na mama yangu tangu nilipokuwa msichana mdogo; katika siku zangu za kumfuata Bwana Yesu, mara nyingi niliguswa na upendo Wake. Nilihisi kwamba Alitupenda sana hata Akasulibiwa na kumwaga kila tone la damu Yake ili kutukomboa. Wakati huo, ndugu katika kanisa letu wote walikuwa wenye upendo na wenye kusaidiana, lakini kwa bahati mbaya imani yetu katika Bwana ilikutana na mateso na kukandamizwa mikononi mwa serikali ya CCP.

