![]() |
| Umeme wa Mashariki | Matunda Machungu ya Kiburi |
17. Umeme wa Mashariki | Matunda Machungu ya Kiburi
Hu Qing Jijini Suzhou, Mkoani Anhui
Nilipoona maneno ya Mungu yakisema: “Wale miongoni mwenu ambao huhudumu kama viongozi daima hutaka kuwa na ubunifu mkubwa, kuwa wazuri kuliko wengine, kupata hila mpya ili Mungu aweze kuona jinsi kweli mlivyo viongozi wakuu. … Nyinyi daima hutaka kuringa; si huu ni ufunuo kwa usahihi wa asili ya kiburi?” (“Bila Ukweli Ni Rahisi Kumkosea Mungu” katika Kumbukumbu za Maongezi ya Kristo), Nilifikiri mwenyewe: Nani ana ujasiri kama huo kujaribu kupata ujanja mpya ya ubunifu? Nani hajui kuwa tabia ya Mungu haistahimili kosa la mwanadamu? Bila shaka siwezi kuthubutu! Mimi binafsi niliamini kuwa nilikuwa na moyo wa kumcha Mungu, na katika kazi yangu sikuthubutu kujaribu kutafuta mbinu.
