Umeme wa Mashariki | 4. Samehe Sabini Mara Saba | 5. Upendo wa Bwana
4. Samehe Sabini Mara Saba
(Mat 18:21-22) Kisha Petro akamwendea, na akamwambia, Bwana, ndugu yangu anikosee mara ngapi na mimi nimsamehe? Mpaka mara saba? Yesu akamwambia, Sikuambii mpaka mara saba: bali, mpaka sabini mara saba.
5. Upendo wa Bwana
(Mat 22:37-39) Yesu akamwambia, Umpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa akili zako zote. Hii ndiyo amri ya kwanza na iliyo kuu. Na ya pili inafanana nayo, Umpende jirani yako kama nafsi yako.
Mwenyezi Mungu alisema, Kati ya dondoo hizi mbili, moja yazungumzia msamaha na nyingine inazungumzia upendo. Mada hizi mbili zinaangazia kwa kweli kazi ambayo Bwana Yesu alitaka kutekeleza katika Enzi ya Neema.



