Jumamosi, 14 Desemba 2019

Kwa nini ni kwa kupitia na kuitii kazi ya Mungu mwenye mwili pekee ndipo mtu anaweza kumjua Mungu?


Aya za Biblia za Kurejelea:

“Na Neno alifanywa kuwa mwili, na akakaa kati yetu, (nasi tukautazama utukufu wake, utukufu kama ule wa Mwana wa pekee aliyezaliwa na Baba,) aliyejawa neema na ukweli” (Yohana 1:14).

“Mimi ndiye njia, ukweli na uhai: hakuna mwanadamu ayaje kwa Baba, bali kwa njia yangu. Kama ninyi mngelinijua, pia mngelimjua Baba yangu: na kuanzia sasa mnamjua, na mmemwona” (Yohana 14:6-7).

Ijumaa, 13 Desemba 2019

Wimbo wa Maneno ya Mungu Kusudi la Kazi ya Mungu la Usimamizi

Kanisa la Mwenyezi Mungu

I
Mungu ana mpango wa usimamizi wa miaka 6,000,
uliyogawanywa katika hatua tatu,
kila moja inaitwa enzi.
Kwanza ni Enzi ya Sheria, kisha Enzi ya Neema,
na Enzi ya Ufalme ni awamu ya mwisho.
Ingawa kazi ya Mungu ni tofauti katika kila moja,
yote inalingana na kile ambacho binadamu wanahitaji,
ama hasa inalingana na ujanja ambao Shetani anatumia,
anapopigana na Yeye.

Alhamisi, 12 Desemba 2019

"Mazungumzo" – Kwa nini CCP Huwafuatia na Kuwakandamiza Wakristo Sana? | Swahili Christian Video Clip 1/6


Katiba ya China hutamka kwa dhahiri uhuru wa dini, lakini kisirisiri, serikali hutumia rasilimali nyingi mno za binadamu na za kifedha kwa kuikandamiza imani ya dini na kuwatesa Wakristo kikatili. Hata hawajaacha kununua vifaa vya hali ya juu zaidi kuwafuatia, kuwafuma, na kuwakamata Wakristo. Serikali ya China imewanyang'anya raia wake haki ya uhuru wa imani na imewanyima kwa utundu haki ya kuishi. Kwa hiyo kwa kweli ni nini sababu na lengo la CCP kufanya yote haya?

Sikiliza zaidi: 

Jumatano, 11 Desemba 2019

"Utamu katika Shida" – Mbinu ya Chama cha Kikomunisti cha China ya Kuwashurutisha Wakristo kwa Kutishia Familia Zao | Swahili Christian Testimony Video Clip 1/6


Ili kuwashurutisha Wakristo kulighilibu kanisa, wamsaliti Mungu na kuharibu nafasi zao za kuokolewa na Mungu, Chama cha Kikomunisti cha China kwa ufidhuli kinawatishia wanafamilia wa Wakristo na kutumia hisia za familia za Wakristo kuwashurutisha kumsaliti Mungu. Je, njama za Chama cha Kikomunisti cha China zinaweza kuendelea? Katika mapambano haya kati ya mema na mabaya, Wakristo watawezaje kumtegemea Mungu ili kushinda majaribu ya Shetani na kusimama imara na kuwa na ushuhuda kwa Mungu?

Jumanne, 10 Desemba 2019

Nikiongozwa na Maneno ya Mungu, Nilishinda Ukandamizaji wa Nguvu za Giza

Chanzo: Kanisa la Mwenyezi Mungu

Na Wang Li, Mkoa wa Zhejiang

Nilimwamini Bwana Yesu pamoja na mama yangu tangu nilipokuwa msichana mdogo; katika siku zangu za kumfuata Bwana Yesu, mara nyingi niliguswa na upendo Wake. Nilihisi kwamba Alitupenda sana hata Akasulibiwa na kumwaga kila tone la damu Yake ili kutukomboa. Wakati huo, ndugu katika kanisa letu wote walikuwa wenye upendo na wenye kusaidiana, lakini kwa bahati mbaya imani yetu katika Bwana ilikutana na mateso na kukandamizwa mikononi mwa serikali ya CCP.

Jumatatu, 9 Desemba 2019

Sura ya 17

Chanzo: Kanisa la Mwenyezi Mungu

Sauti Yangu inatoka kama radi, ikitia nuru roboduara zote nne na dunia nzima, na katikati ya radi na umeme, binadamu wanaangushwa chini. Hakuna mwanadamu aliyewahi kusimama imara katikati ya radi na umeme: Wanadamu wengi wanaogopa sana kuja kwa mwangaza Wangu na hawajui cha kufanya. Wakati mwangaza hafifu unaanza kuonekana Mashariki, watu wengi, wakiongozwa na huu mng’ao dhaifu, wanaamshwa mara moja kutoka kwa njozi zao. Lakini, hakuna aliyewahi kutambua kwamba siku imewadia mwangaza Wangu unaposhuka duniani. 

Jumapili, 8 Desemba 2019

"Utamu katika Shida" – Kwa nini Chama cha Kikomunisti cha China Kilibuni Tukio la 5/28 la Zhaoyuan? | Swahili Christian Testimony Video Clip 5/6


Baada ya kesi ya hadharani ya Tukio la Shandong Zhaoyuan, watu wenye utambuzi wote walitambua kuwa kesi hii ilibuniwa kabisa na Chama cha Kikomunisti cha China ili kulisingizia na kuliaibisha Kanisa la Mwenyezi Mungu kwa makusudi. Ilikuwa kesi ya kuundwa na utumiaji vibaya wa haki. Sababu ya nia mbaya ya Chama cha Kikomunisti cha China kufanya hivi ni nini?

Sikiliza zaidi: Swahili Christian Movie | Nyendo za Mateso ya Kidini | "Kukaribia Hatari na Kurudi"